< Kutoka 18 >

1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
And he heard Jethro [the] priest of Midian [the] father-in-law of Moses all that he had done God for Moses and for Israel people his that he had brought out Yahweh Israel from Egypt.
2 Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
And he had taken Jethro [the] father-in-law of Moses Zipporah [the] wife of Moses after dismissal her.
3 pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
And [the] two sons her who [the] name of the one [was] Gershom for he had said a sojourner I have become in a land foreign.
4 Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
And [the] name of the one [was] Eliezer for [the] God of father my [has been] help my and he has delivered me from [the] sword of Pharaoh.
5 Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
And he came Jethro [the] father-in-law of Moses and sons his and wife his to Moses into the wilderness where he [was] encamped there [the] mountain of God.
6 Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
And he said to Moses I father-in-law your Jethro [am] coming to you and wife your and [the] two sons her with her.
7 Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
And he went out Moses to meet father-in-law his and he bowed down and he kissed him and they asked each of neighbor his to welfare and they went the tent towards.
8 Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
And he recounted Moses to father-in-law his all that he had done Yahweh to Pharaoh and to Egypt on [the] causes of Israel all the hardship which it had come upon them on the journey and he had delivered them Yahweh.
9 Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
And he rejoiced Jethro on all the good which he had done Yahweh to Israel whom he had delivered it from [the] hand of Egypt.
10 Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
And he said Jethro [be] blessed Yahweh who he has delivered you from [the] hand of Egypt and from [the] hand of Pharaoh who he has delivered the people from under [the] hand of Egypt.
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
Now I know that [is] great Yahweh more than all the gods for in the matter which they have acted presumptuously on them.
12 Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
And he took Jethro [the] father-in-law of Moses a burnt offering and sacrifices to God and he came Aaron and all - [the] elders of Israel to eat food with [the] father-in-law of Moses before God.
13 Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
And it was from [the] next day and he sat Moses to judge the people and it stood the people at Moses from the morning until the evening.
14 Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
And he saw [the] father-in-law of Moses all that he [was] doing for the people and he said what? [is] the thing this which you [are] doing for the people why? [are] you sitting to alone you and all the people [is] standing at you from morning until evening.
15 Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
And he said Moses to father-in-law his thatr it comes to me the people to consult God.
16 Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
For it will be[long] to them a matter [it is] coming to me and I judge between each and between neighbor his and I make known [the] statutes of God and laws his.
17 Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
And he said [the] father-in-law of Moses to him not [is] good the thing which you [are] doing.
18 Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
Certainly you will wear yourself out both you as well as the people this which [is] with you for [is too] heavy for you the thing not you are able to do it to alone you.
19 Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
Now listen to voice my let me advise you and may he be God with you be you for the people in front of God and you will bring you the matters to God.
20 Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
And you will warn them the statutes and the laws and you will make known to them the way [which] they will walk in it and the work which they will do!
21 Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
And you you will provide from all the people men of ability [those] fearing God men of faithfulness [who] hate unjust gain and you will appoint over them officials of thousands officials of hundreds officials of fifties and officials of tens.
22 Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
And they will judge the people at every time and it will be every matter great they will bring to you and every matter small they will judge they and lighten from on yourself and they will bear with you.
23 Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
If the thing this you will do and he will command you God and you will be able to endure and also all the people this to place its it will go in peace.
24 Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
And he listened Moses to [the] voice father-in-law his and he did all that he had said.
25 Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
And he chose Moses men of ability from all Israel and he appointed them chiefs over the people of icials of thousands officials of hundreds officials of fifties and officials of tens.
26 Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
And they judged the people at every time the matter difficult they brought! to Moses and every matter small they judged they.
27 Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.
And he sent off Moses father-in-law his and he went himself to land his.

< Kutoka 18 >