< Kutoka 18 >
1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
Now Jethro [Abundance], the priest of Midian [Strife], Moses [Drawn out]’ father-in-law, sh'ma ·heard obeyed· of all that God had done for Moses [Drawn out], and for Israel [God prevails] his people, how that Adonai had brought Israel [God prevails] out of Egypt [Abode of slavery].
2 Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
Jethro [Abundance], Moses [Drawn out]’ father-in-law, received Zipporah, Moses [Drawn out]’ wife, after he had sent her away,
3 pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
and her two sons. The name of one son was Gershom, for Moses [Drawn out] said, “I have lived as a foreigner in a foreign land”.
4 Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
The name of the other was Eliezer, for he said, “My father’s God was my help and delivered me from Pharaoh’s sword.”
5 Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
Jethro [Abundance], Moses [Drawn out]’ father-in-law, came with his sons and his wife to Moses [Drawn out] into the wilderness where he was encamped, at the Mountain of God.
6 Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
He said to Moses [Drawn out], “I, your father-in-law Jethro [Abundance], have come to you with your wife, and her two sons with her.”
7 Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
Moses [Drawn out] went out to meet his father-in-law, and bowed and kissed him. They asked each other of their welfare, and they came into the tent.
8 Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
Moses [Drawn out] told his father-in-law all that Adonai had done to Pharaoh and to the Egyptians [people from Abode of slavery] for Israel [God prevails]’s sake, all the hardships that had come on them on the way, and how Adonai delivered them.
9 Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
Jethro [Abundance] rejoiced for all the goodness which Adonai had done to Israel [God prevails], in that he had delivered them out of the hand of the Egyptians [people from Abode of slavery].
10 Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
Jethro [Abundance] said, “Blessed be Adonai, who has delivered you out of the hand of the Egyptians [people from Abode of slavery], and out of the hand of Pharaoh; who has delivered the people from under the hand of the Egyptians [people from Abode of slavery].
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
Now I know that Adonai is greater than all deities because of the thing in which they dealt arrogantly against them.”
12 Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
Jethro [Abundance], Moses [Drawn out]’ father-in-law, took a burnt offering and sacrifices for God. Aaron [Light-bringer] came with all the elders of Israel [God prevails], to eat bread with Moses [Drawn out]’ father-in-law before God.
13 Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
On the next day, Moses [Drawn out] sat to judge the people, and the people stood around Moses [Drawn out] from the morning to the evening.
14 Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
When Moses [Drawn out]’ father-in-law saw all that he did to the people, he said, “What is this thing that you do for the people? Why do you sit alone, and all the people stand around you from morning to evening?”
15 Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
Moses [Drawn out] said to his father-in-law, “Because the people come to me to inquire of God.
16 Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
When they have a matter, they come to me, and I judge between a man and his neighbor, and I make them know the statutes of God, and his torot ·teachings·.”
17 Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
Moses [Drawn out]’ father-in-law said to him, “The thing that you do is not good.
18 Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
You will surely wear away, both you, and this people that is with you; for the thing is too heavy for you. You are not able to perform it yourself alone.
19 Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
Sh'ma ·Hear obey· now to my voice. I will give you counsel, and God be with you. You represent the people before God, and bring the causes to God.
20 Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
You shall teach them the statutes and the torot ·teachings·, and shall show them the way in which they must walk, and the work that they must do.
21 Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
Moreover you shall provide out of all the people able men which fear God: men of truth, hating unjust gain; and place such over them, to be rulers of thousands, rulers of hundreds, rulers of fifties, and rulers of tens.
22 Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
Let them judge the people at all times. It shall be that every great matter they shall bring to you, but every small matter they shall judge themselves. So shall it be easier for you, and they shall share the load with you.
23 Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
If you will do this thing, and God enjoins you to do so, then you will be able to endure, and all these people also will go to their place in peace.”
24 Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
So Moses [Drawn out] sh'ma ·heard obeyed· the voice of his father-in-law, and did all that he had said.
25 Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
Moses [Drawn out] chose able men out of all Israel [God prevails], and made them heads over the people, rulers of thousands, rulers of hundreds, rulers of fifties, and rulers of tens.
26 Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
They judged the people at all times. They brought the hard causes to Moses [Drawn out], but every small matter they judged themselves.
27 Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.
Moses [Drawn out] let his father-in-law depart, and he went his way into his own land.