< Kutoka 17 >

1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
Ainsi toute la multitude des enfants d’Israël étant partie du désert de Sin, et ayant fait des séjours, selon les paroles du Seigneur, ils campèrent à Raphidim, où il n’y avait pas d’eau à boire pour le peuple,
2 Kwa hiyo wakagombana na Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”
Qui querellant Moïse, dit: Donne-nous de l’eau, afin que nous buvions. Moïse leur répondit: Pourquoi me querellez-vous? pourquoi tentez-vous le Seigneur?
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanungʼunika dhidi ya Mose, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
Là donc le peuple eut soif à cause de la pénurie d’eau, et il murmura contre Moïse, disant: Pourquoi nous as-tu fait sortir de l’Egypte, pour nous faire mourir de soif, nous, nos enfants et nos bêtes?
4 Kisha Mose akamlilia Bwana, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
Or Moïse cria au Seigneur, disant: Que ferai-je à ce peuple-ci? encore un peu, et il me lapidera.
5 Bwana akamjibu Mose, “Pita mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, ichukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
Et le Seigneur répondit à Moïse: Marche devant le peuple, et prends avec toi des anciens d’Israël; et la verge dont tu as frappé le fleuve, prends-la en ta main, et va.
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Mose akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
Voilà que moi, je me tiendrai là devant toi sur la pierre d’Horeb; et tu frapperas la pierre, et il en sortira de l’eau, afin que le peuple boive. Moïse fit ainsi devant les anciens d’Israël:
7 Naye akapaita mahali pale Masa, na Meriba kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Bwana wakisema, “Je, Bwana yu pamoja nasi au la?”
Et il appela ce lieu du nom de Tentation, à cause de la querelle des enfants d’Israël, et parce qu’ils avaient tenté le Seigneur, disant: Le Seigneur est-il parmi nous, ou non?
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
Or Amalec vint, et il combattait contre Israël à Raphidim.
9 Mose akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
Et Moïse dit à Josué: Choisis des hommes, et étant sorti, combats contre Amalec; demain moi, je me tiendrai au sommet de la colline, ayant la verge de Dieu en ma main.
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Mose alivyomwagiza, nao Mose, Aroni na Huri wakapanda juu ya kilima.
Josué fit comme avait dit Moïse, et il combattait contre Amalec: mais Moïse et Aaron et Hur montèrent sur le sommet de la colline.
11 Ikawa wakati wote Mose alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
Et lorsque Moïse élevait les mains, Israël était victorieux; mais s’il les abaissait un peu, Amalec l’emportait.
12 Mikono ya Mose ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Aroni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Mose, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti mpaka jua lilipozama.
Or, les mains de Moïse étaient appesanties; prenant donc une pierre, ils la mirent sous lui; il s’y assit; mais Aaron et Hur soutenaient ses mains des deux côtés. Et il arriva que ses mains ne se lassèrent pas jusqu’au coucher du soleil.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
Et Josué mit en fuite Amalec et son peuple, par le tranchant du glaive.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
Or le Seigneur dit à Moïse: Écris ceci pour souvenir dans le livre, et fais-le entendre à Josué; car j’effacerai la mémoire d’Amalec sous le ciel.
15 Mose akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
Et Moïse bâtit un autel et rappela du nom de: Le Seigneur est mon exaltation, disant:
16 Mose akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa mpaka kwenye kiti cha enzi cha Bwana. Bwana atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kutoka kizazi hata kizazi.”
La main du trône du Seigneur et la guerre du Seigneur seront contre Amalec de génération en génération.

< Kutoka 17 >