< Kutoka 17 >

1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
Therfor al the multitude of the sones of Israel yede forth fro the deseert of Syn, bi her dwellyngis, bi the word of the Lord, and settiden tentis in Rafidym, where was not watir to the puple to drynke.
2 Kwa hiyo wakagombana na Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”
Whiche puple chidde ayens Moises, and seide, Yyue thou water to vs, that we drynke. To whiche Moises answeride, What chiden ye ayens me, and whi tempten ye the Lord?
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanungʼunika dhidi ya Mose, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
Therfor the puple thristide there for the scarsnesse of watir, and grutchiden ayens Moises, and seide, Whi madist thou vs to go out of Egipt, to sle vs, and oure fre children, and beestis, for thrist?
4 Kisha Mose akamlilia Bwana, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
Forsothe Moises criede to the Lord, and seide, What schal Y do to this puple? yit a litil, also it schal stone me.
5 Bwana akamjibu Mose, “Pita mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, ichukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
The Lord seide to Moises, Go thou bifore the puple, and take with thee of the eldre men of Israel, and take in thin hond the yerde, `bi which thou hast smyte the flood, and go; lo!
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Mose akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
Y schal stonde there before thee, aboue the stoon of Oreb, and thou schalt smyte the stoon, and water schal go out therof, that the puple drynke. Moises dide so byfore the eldere men of Israel;
7 Naye akapaita mahali pale Masa, na Meriba kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Bwana wakisema, “Je, Bwana yu pamoja nasi au la?”
and he clepide the name of that place Temptacioun, for the chidyng of the sones of Israel, and for thei temptiden the Lord, and seiden, Whether the Lord is in vs, ether nay?
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
Forsothe Amalech cam, and fauyt ayens Israel in Rafidym.
9 Mose akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
And Moises seide to Josue, Chese thou men, and go out, and fiyte to morewe ayens men of Amalech; lo! Y schal stonde in the cop of the hil, and Y schal haue `the yerde of God in myn hond.
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Mose alivyomwagiza, nao Mose, Aroni na Huri wakapanda juu ya kilima.
Josue dide as Moises spak, and fauyt ayens Amalech. Forsothe Moises, and Aaron, and Hur stieden on the cop of the hil;
11 Ikawa wakati wote Mose alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
and whanne Moises reiside the hondis, Israel ouercam; forsothe if he let down a litil, Amalech ouercam.
12 Mikono ya Mose ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Aroni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Mose, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti mpaka jua lilipozama.
Sotheli `the hondis of Moises weren heuy, therfor thei token a stoon, and puttide vndir hym, in which stoon he sat. Forsothe Aaron and Hur susteyneden hise hondis, on euer eithir side; and it was don, that hise hondis weren not maad weri, til to the goyng down of the sunne.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
And Josue droof a wey Amalech and his puple, in `the mouth of swerd, that is, bi the scharpnesse of the swerd.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
Forsothe the Lord seide to Moises, Wryte thou this in a book, for mynde, and take in the eeris of Josue; for Y schal do a wei the mynde of Amalech fro vndur heuene.
15 Mose akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
And Moises bildide an auter, and clepide the name therof The Lord myn enhaunsere,
16 Mose akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa mpaka kwenye kiti cha enzi cha Bwana. Bwana atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kutoka kizazi hata kizazi.”
and seide, For the hond of the Lord aloone, and the bateil of God schal be ayens Amalech, fro generacioun in to generacioun.

< Kutoka 17 >