< Kutoka 17 >

1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
And all the assembly of the children of Israel journeyed from the wilderness of Sin, according to their journeys, at the command of Jehovah; and they encamped in Rephidim; and there was no water for the people to drink.
2 Kwa hiyo wakagombana na Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”
And the people contended with Moses, and said, Give us water, that we may drink! And Moses said to them, Why do ye dispute with me? Why do ye tempt Jehovah?
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanungʼunika dhidi ya Mose, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
And the people thirsted there for water; and the people murmured against Moses, and said, Why is it that thou hast brought us up out of Egypt, to kill us and our children and our cattle with thirst?
4 Kisha Mose akamlilia Bwana, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
And Moses cried to Jehovah, saying, What shall I do with this people? Yet a little, and they will stone me!
5 Bwana akamjibu Mose, “Pita mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, ichukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
And Jehovah said to Moses, Go on before the people, and take with thee of the elders of Israel, and thy staff with which thou didst smite the river, take in thy hand, and go.
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Mose akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
Behold, I will stand before thee there upon the rock on Horeb; and thou shalt strike the rock, and there shall come water out of it, that the people may drink. And Moses did so before the eyes of the elders of Israel.
7 Naye akapaita mahali pale Masa, na Meriba kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Bwana wakisema, “Je, Bwana yu pamoja nasi au la?”
And he called the name of the place Massah, and Meribah, because of the contention of the children of Israel, and because they had tempted Jehovah, saying, Is Jehovah among us, or not?
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
And Amalek came and fought with Israel in Rephidim.
9 Mose akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
And Moses said to Joshua, Choose us men, and go out, fight with Amalek; to-morrow I will stand on the top of the hill with the staff of God in my hand.
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Mose alivyomwagiza, nao Mose, Aroni na Huri wakapanda juu ya kilima.
And Joshua did as Moses had said to him, to fight with Amalek; and Moses, Aaron and Hur went up to the top of the hill.
11 Ikawa wakati wote Mose alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
And it came to pass when Moses raised his hand, that Israel prevailed; and when he let down his hand, Amalek prevailed.
12 Mikono ya Mose ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Aroni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Mose, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti mpaka jua lilipozama.
And Moses' hands were heavy; then they took a stone, and put [it] under him, and he sat on it; and Aaron and Hur supported his hands, one on this side, and one on that side; and his hands were steady until the going down of the sun.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
And Joshua broke the power of Amalek and his people with the edge of the sword.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
And Jehovah said to Moses, Write this [for] a memorial in the book, and rehearse [it] in the ears of Joshua, that I will utterly blot out the remembrance of Amalek from under the heavens.
15 Mose akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
And Moses built an altar, and called the name of it Jehovah-nissi.
16 Mose akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa mpaka kwenye kiti cha enzi cha Bwana. Bwana atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kutoka kizazi hata kizazi.”
And he said, For the hand is on the throne of Jah; Jehovah will have war with Amalek from generation to generation!

< Kutoka 17 >