< Kutoka 17 >
1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
Tedy když se odebralo všecko shromáždění synů Izraelských z pouště Sin, po stanovištích svých vedlé rozkazu Hospodinova, položili se v Rafidim, kdež nebylo vod, kteréž by lid píti mohl.
2 Kwa hiyo wakagombana na Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”
Protož domlouval se lid na Mojžíše, pravě: Dejte nám vody, abychom pili. Jimž odpověděl Mojžíš: Proč se na mne domlouváte? Proč pokoušíte Hospodina?
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanungʼunika dhidi ya Mose, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
I žíznil tu lid pro nedostatek vod, a reptal na Mojžíše a mluvil: Proč jsi vyvedl nás z Egypta, abys mne s syny i dobytky mými žízní zmořil?
4 Kisha Mose akamlilia Bwana, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
Tedy volal Mojžíš k Hospodinu, řka: Což mám činiti s tím lidem? Však již tudíž ukamenují mne.
5 Bwana akamjibu Mose, “Pita mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, ichukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
I řekl Hospodin Mojžíšovi: Jdiž před lidem, pojma s sebou některé z starších Izraelských; hůl také svou, kterouž jsi udeřil v vodu, vezmi do ruky své a jdi.
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Mose akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
Aj, já státi budu před tebou tam na skále, na Orébě; i udeříš v skálu, a vyjdou z ní vody, kteréž bude píti lid. I učinil tak Mojžíš před očima starších Izraelských.
7 Naye akapaita mahali pale Masa, na Meriba kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Bwana wakisema, “Je, Bwana yu pamoja nasi au la?”
A dal jméno místu tomu Massah a Meribah, pro reptání synů Izraelských, a že pokoušeli Hospodina, řkouce: Jest-li Hospodin u prostřed nás, či není?
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
Přitáhl pak Amalech, a bojoval s Izraelem v Rafidim.
9 Mose akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
I řekl Mojžíš k Jozue: Vybeř nám některé muže, a vytáhna, bojuj s Amalechem; já zítra státi budu na vrchu hory, a hůl Boží v ruce své míti budu.
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Mose alivyomwagiza, nao Mose, Aroni na Huri wakapanda juu ya kilima.
Tedy Jozue udělal tak, jakž mu poručil Mojžíš, a bojoval s Amalechem; Mojžíš pak, Aron a Hur vstoupili na vrch hory.
11 Ikawa wakati wote Mose alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
A dokudž Mojžíš vzhůru držel ruce své, vítězil Izrael; ale jakž opouštěl ruku svou, přemáhal Amalech.
12 Mikono ya Mose ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Aroni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Mose, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti mpaka jua lilipozama.
Ale že ruce Mojžíšovy byly obtíženy, protož vzavše kámen, podložili pod něho, a on sedl na něm; Aron pak a Hur podpírali ruce jeho, jeden z jedné, druhý z druhé strany. I byly obě ruce jeho vztažené až do západu slunce.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
A tak porazil Jozue Amalecha i lid jeho mečem.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
Mluvil potom Hospodin k Mojžíšovi: Vpiš to do knih na památku, a pilně to vkládej v uši Jozue, že do konce vyhladím památku Amalechovu všudy pod nebem.
15 Mose akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
Tedy vzdělal Mojžíš oltář a nazval jméno jeho: Hospodin korouhev má.
16 Mose akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa mpaka kwenye kiti cha enzi cha Bwana. Bwana atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kutoka kizazi hata kizazi.”
Nebo řekl: Tak má jmenován býti, proto že ruka nad trůnem Hospodinovým osvědčuje boj Hospodinův proti Amalechovi od národu až do národu.