< Kutoka 16 >

1 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.
Et ils partirent d’Elim, et toute la multitude des enfants d’Israël vint au désert de Sin, qui est entre Elim et Sinaï, le quinzième jour du second mois après qu’ils furent sortis de la terre d’Egypte.
2 Huko jangwani hiyo jumuiya yote wakawanungʼunikia Mose na Aroni.
Et toute l’assemblée des enfants d’Israël murmura contre Moïse et Aaron dans le désert.
3 Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungelikufa kwa mkono wa Bwana huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”
Et les enfants d’Israël leur dirent: Plût à Dieu que nous fussions morts par la main du Seigneur dans la terre d’Egypte, quand nous étions assis près des marmites de viandes, et que nous mangions du pain à satiété! Pourquoi nous avez-vous amenés dans ce désert, pour faire mourir toute cette multitude de faim?
4 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nitanyesha mikate kutoka mbinguni kwa ajili yenu. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.
Or le Seigneur dit à Moïse: Voici que moi, je ferai pleuvoir pour vous du pain du ciel; que le peuple sorte, et qu’il en amasse ce qui lui suffira pour chaque jour, afin que j’éprouve s’il marche en ma loi, ou non.
5 Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”
Mais qu’au sixième jour ils apprêtent ce qu’ils auront apporté, et que ce soit le double de ce qu’ils avaient coutume d’amasser chaque jour.
6 Kwa hiyo Mose na Aroni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kwamba Bwana ndiye aliwatoa Misri,
Et Moïse et Aaron dirent à tous les enfants d’Israël: Ce soir vous saurez que c’est le Seigneur qui vous a retirés de la terre d’Egypte;
7 kisha asubuhi mtauona utukufu wa Bwana, kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunungʼunikie?”
Et au matin vous verrez la gloire du Seigneur; car il a entendu votre murmure contre lui; mais nous, qui sommes-nous, pour que vous murmuriez contre nous?
8 Pia Mose akasema, “Mtajua kuwa alikuwa Bwana wakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnungʼuniki dhidi yetu, bali dhidi ya Bwana.”
Et Moïse ajouta: Le Seigneur vous donnera ce soir de la chair à manger, et au matin du pain à satiété, parce qu’il a entendu vos murmures par lesquels vous avez murmuré contre lui; car, nous, que sommes-nous? ce n’est donc pas contre nous qu’est votre murmure, mais contre le Seigneur.
9 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zake Bwana, kwa maana amesikia manungʼuniko yenu.’”
Moïse dit aussi à Aaron: Dis à toute l’assemblée des enfants d’Israël: Approchez-vous devant le Seigneur car il a entendu votre murmure.
10 Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu wa Bwana ukitokeza katika wingu.
Et lorsque Aaron parlait à toute l’assemblée des enfants d’Israël, ils regardèrent vers le désert, et voilà que la gloire du Seigneur apparut dans la nuée.
11 Bwana akamwambia Mose,
Or le Seigneur parla à Moïse, disant:
12 “Nimesikia manungʼuniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua ya kwamba Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’”
J’ai entendu les murmures des enfants d’Israël, dis-leur: Ce soir vous mangerez de la chair, et au matin vous serez rassasiés de pain, et vous saurez que je suis le Seigneur votre Dieu.
13 Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na tabaka la umande kuzunguka kambi.
Le soir vint donc, et les cailles montant couvrirent le camp: le matin aussi la rosée se trouva répandue autour du camp.
14 Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.
Et lorsqu’elle eut couvert la surface de la terre, il apparut dans le désert quelque chose de menu et comme pilé au mortier, ressemblant à la gelée blanche sur la terre.
15 Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani. Mose akawaambia, “Huu ndio mkate ambao Bwana amewapa mle.
Ce qu’ayant vu les enfants d’Israël, ils se dirent les uns aux autres: Manhu, ce qui signifie: Qu’est-ceci? ils ignoraient, en effet, ce que c’était. Moïse leur dit: C’est le pain que le Seigneur vous a donné à manger.
16 Hivi ndivyo Bwana alivyoamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishi moja kwa kila mtu mliye naye katika hema yenu.’”
Voici les paroles que le Seigneur a ordonnées: Que chacun en amasse autant qu’il suffit pour manger: un gomor pour chaque tête, selon le nombre de vos âmes qui habitent dans leur tente; voilà ce que vous recueillerez.
17 Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa, baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.
Et les enfants d’Israël firent ainsi, et ils en amassèrent, l’un plus, l’autre moins.
18 Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.
Et ils la mesurèrent à la mesure du gomor: or celui qui en avait plus amassé, n’en eut pas davantage, et celui qui en avait moins amassé, n’en trouva pas moins, car chacun en recueillit selon ce qu’il pouvait manger.
19 Kisha Mose akawaambia, “Mtu yeyote asibakize chochote mpaka asubuhi.”
Moïse leur dit aussi: Que nul n’en laisse pour le malin.
20 Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Mose, wakahifadhi kiasi fulani mpaka asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Mose akawakasirikia.
Tous ne l’écoutèrent pas, mais quelques-uns d’entre eux en laissèrent jusqu’au matin; or elle commença par fourmiller de vers, puis elle se corrompit; et Moïse fut irrité contre eux.
21 Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.
Chacun en amassait donc le matin autant qu’il pouvait suffire pour manger; et lorsque le soleil était devenu chaud, elle se fondait.
22 Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwarifu Mose.
Mais, au sixième jour, ils amassèrent le double de cette nourriture, c’est-à-dire, deux gomors pour chaque personne: tous les chefs de la multitude vinrent, et l’annoncèrent à Moïse,
23 Mose akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Kesho itakuwa siku ya mapumziko, Sabato takatifu kwa Bwana. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini chochote kinachobaki na mkiweke mpaka asubuhi.’”
Qui leur dit: Voici ce qu’a dit le Seigneur: C’est demain le repos du sabbat, consacré au Seigneur; ce qui doit être fait, faites-le aujourd’hui; et ce qui doit être cuit, faites-le cuire, mais tout ce qui sera de reste, serrez-le jusqu’au matin.
24 Kwa hiyo wakavihifadhi mpaka asubuhi, kama Mose alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.
Ils firent donc selon qu’avait ordonné Moïse, et la manne ne se corrompit point; et on n’y trouva pas de ver.
25 Mose akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwa Bwana. Hamtapata chochote juu ya nchi leo.
Et Moïse dit: Mangez-la aujourd’hui, parce que c’est le sabbat du Seigneur; il ne s’en trouvera pas aujourd’hui dans la campagne.
26 Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwepo chochote.”
Pendant six jours ramassez-en, car au septième jour, c’est le sabbat du Seigneur; c’est pourquoi on n’en trouvera pas.
27 Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata chochote.
Or vint le septième jour, et quelques-uns du peuple étant sortis pour en amasser, ils n’en trouvèrent point.
28 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu mpaka lini?
Alors le Seigneur dit à Moïse: Jusqu’à quand ne voudrez vous point garder mes commandements et ma loi?
29 Fahamuni kuwa Bwana amewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”
Voyez que le Seigneur vous a donné le sabbat, et à cause de cela au sixième jour il vous a accordé le double de nourriture: que chacun demeure chez soi, et que nul ne sorte de son lieu au septième jour.
30 Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.
Ainsi le peuple sabbatisa au septième jour.
31 Watu wa Israeli wakaita ile mikate mana Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.
Et la maison d’Israël appela cette nourriture du nom de Man; elle était blanche comme une graine de coriandre, et son goût, celui de la fleur de farine mêlée avec du miel.
32 Mose akasema, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’”
Or Moïse dit: Voici les paroles qu’a ordonnées le Seigneur: Emplis-en un gomor, et qu’il soit gardé dans les générations qui doivent venir dans la suite, afin qu’elles connaissent le pain dont je vous ai nourris dans le désert, quand vous avez été retirés de la terre d’Egypte.
33 Kwa hiyo Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele za Bwana ili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”
Et Moïse dit à Aaron: Prends un vase et mets-y de la Manne, autant que peut en contenir un gomor; et place-le devant le Seigneur, afin de le conserver en vos générations,
34 Kama Bwana alivyomwagiza Mose, hatimaye Aroni alikuja kuihifadhi ndani ya Sanduku la Ushuhuda.
Comme a ordonné le Seigneur à Moïse. Et Aaron le plaça dans le tabernacle pour être réservé.
35 Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana hadi walipofika mpakani mwa Kanaani.
Or, les enfants d’Israël mangèrent la Manne pendant quarante ans, jusqu’à ce qu’ils vinrent en une terre habitable; c’est de cet aliment qu’ils furent nourris, jusqu’à ce qu’ils touchèrent aux confins de la terre de Chanaan.
36 (Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)
Or, le gomor est la dixième partie de l’éphi.

< Kutoka 16 >