< Kutoka 16 >
1 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.
And thei yeden forth fro Helym, and al the multitude of the sones of Israel cam in to deseert of Syn, which is bitwixe Helym and Synai, in the fiftenethe dai of the secunde monethe aftir that thei yeden out of the lond of Egipt.
2 Huko jangwani hiyo jumuiya yote wakawanungʼunikia Mose na Aroni.
And al the congregacioun of the sones of Israel grutchide ayens Moises, and ayens Aaron, in the wildirnesse.
3 Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungelikufa kwa mkono wa Bwana huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”
And the sones of Israel seiden to hem, We wolden that we hadden be deed bi the `hoond of the Lord in the lond of Egipt, whanne we saten on the `pottis of fleisch, and eeten looues in plentee; whi leden ye vs in to this deseert, that ye schulden sle al the multitude with hungur?
4 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nitanyesha mikate kutoka mbinguni kwa ajili yenu. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.
Forsothe the Lord seide to Moises, Lo! Y schal reyne to you looues fro heuene; the puple go out, that it gadere tho thingis that sufficen bi ech day; that Y asaie the puple, whethir it goith in my lawe, ether nai.
5 Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”
Sotheli in the sixte dai make thei redi that that thei schulen bere yn, and be it double ouer that thei weren wont to gadere bi ech dai.
6 Kwa hiyo Mose na Aroni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kwamba Bwana ndiye aliwatoa Misri,
And Moises and Aaron seiden to alle the sones of Israel, At euentid ye schulen wite that the Lord ledde you out of the lond of Egipt;
7 kisha asubuhi mtauona utukufu wa Bwana, kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunungʼunikie?”
and in the morewetid ye schulen se the glorie of the Lord; for Y herde youre grutchyng ayens the Lord; sotheli what ben we, for ye grutchen ayens us?
8 Pia Mose akasema, “Mtajua kuwa alikuwa Bwana wakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnungʼuniki dhidi yetu, bali dhidi ya Bwana.”
And Moises seide, The Lord schal yyue to you at euentid fleischis to ete, and looues in the morewetid in plentee, for he herde youre grutchyngis, bi which ye grutchiden ayens hym; for whi, what ben we? youre grutchyng is not ayens vs but ayens the Lord.
9 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zake Bwana, kwa maana amesikia manungʼuniko yenu.’”
And Moises seide to Aaron, Seie thou to al the congregacioun of the sones of Israel, Neiye ye bifore the Lord, for he herde youre grutchyng.
10 Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu wa Bwana ukitokeza katika wingu.
And whanne Aaron spak to al the cumpeny of the sones of Israel, thei bihelden to the wildirnesse, and lo! the glorie of the Lord apperide in a cloude.
11 Bwana akamwambia Mose,
Forsothe the Lord spak to Moises,
12 “Nimesikia manungʼuniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua ya kwamba Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’”
and seide, Y herde the grutchyngis of the sones of Israel; spek thou to hem, At euentid ye schulen ete fleischis, and in the morewtid ye schulen be fillid with looues, and ye schulen wite that Y am `youre Lord God.
13 Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na tabaka la umande kuzunguka kambi.
Therfor euentid was maad, and `curlewes stieden and hiliden the castels; and in the morewtid deew cam bi the face of the castels.
14 Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.
And whanne it hadde hilid the erthe, a litil thing, and as powned with a pestel, in the licnesse of an hoorfrost on erthe, apperide in the wildirnesse.
15 Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani. Mose akawaambia, “Huu ndio mkate ambao Bwana amewapa mle.
And whanne the sones of Israel hadden seyn that, thei seiden to gidere, Man hu? which signyfieth, what is this? for thei wisten not what it was. To whiche Moises seide, This is the breed, which the Lord hath youe to you to ete.
16 Hivi ndivyo Bwana alivyoamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishi moja kwa kila mtu mliye naye katika hema yenu.’”
This is the word which the Lord comaundide, Ech man gadere therof as myche as suffisith to be etun, gomor bi ech heed, bi the noumbre of youre soulis that dwellen in the tabernacle, so ye schulen take.
17 Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa, baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.
And the sones of Israel diden so, and thei gaderiden oon more, another lesse;
18 Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.
and thei metiden at the mesure gomor; nethir he that gaderide more had more, nethir he that made redi lesse fond lesse, but alle gaderiden bi that that thei myyten ete.
19 Kisha Mose akawaambia, “Mtu yeyote asibakize chochote mpaka asubuhi.”
And Moises seide to hem, Noon leeue therof in to the morewtid; whiche herden not him,
20 Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Mose, wakahifadhi kiasi fulani mpaka asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Mose akawakasirikia.
but summe of hem leften til to the morewtid, and it bigan to buyle with wormes, and it was rotun; and Moises was wrooth ayens hem.
21 Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.
Forsothe alle gaderiden in the morewtid as myche as `miyte suffice to be eten; and whanne the sunne was hoot, it was moltun.
22 Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwarifu Mose.
Sotheli in the sixte dai thei gaderiden double metis, that is, `twei gomor by ech man. Forsothe alle the princis of the multitude camen, and telden to Moises, which seide to hem,
23 Mose akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Kesho itakuwa siku ya mapumziko, Sabato takatifu kwa Bwana. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini chochote kinachobaki na mkiweke mpaka asubuhi.’”
This it is that the Lord spak, The reste of the sabot is halewid to the Lord, do ye what euer thing schal be wrouyt to morewe, and sethe ye tho thingis that schulen be sodun; sotheli what euer thing is residue, kepe ye til in to the morewe.
24 Kwa hiyo wakavihifadhi mpaka asubuhi, kama Mose alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.
And thei diden so as Moises comaundide, and it was not rotun, nether a worm was foundun ther ynne.
25 Mose akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwa Bwana. Hamtapata chochote juu ya nchi leo.
And Moises seide, Ete ye that in this dai, for it is the sabat of the Lord, it schal not be foundun to dai in the feeld; gadere ye in sixe daies,
26 Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwepo chochote.”
forsothe the sabat of the Lord is in the seuenthe dai, therfor it schal not be foundun.
27 Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata chochote.
The seuenthe dai cam, and summe of the puple yeden out `to gadire, and thei founden not.
28 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu mpaka lini?
Forsothe the Lord seide to Moises, Hou long `nylen ye kepe my comaundementis, and my lawe?
29 Fahamuni kuwa Bwana amewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”
Se ye that the Lord yaf to you the sabat, and for this he yaf to you in the sixte dai double meetis; ech man dwelle at him silf, noon go out of his place in the seuenthe dai.
30 Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.
And the puple kepte sabat in the seuenthe dai.
31 Watu wa Israeli wakaita ile mikate mana Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.
And the hous of Israel clepide the name therof man, which was whijt as the seed of coriandre, and the taast therof was as of flour with hony.
32 Mose akasema, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’”
Forsothe Moises seide, This is the word which the Lord comaundide, Fille thou a gomor therof, and be it kept in to generaciouns to comynge aftirward, that thei knowe the breed bi which Y fedde you in the wildirnesse, whanne ye weren led out of the lond of Egipt.
33 Kwa hiyo Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele za Bwana ili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”
And Moises seide to Aaron, Take thou o vessel, and putte therinne man, as myche as gomor mai take, and putte bifore the Lord, to be kept in to youre generaciouns,
34 Kama Bwana alivyomwagiza Mose, hatimaye Aroni alikuja kuihifadhi ndani ya Sanduku la Ushuhuda.
as the Lord comaundide to Moises; and Aaron puttide that to be kept in the tabernacle.
35 Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana hadi walipofika mpakani mwa Kanaani.
Forsothe the sones of Israel eeten manna in fourti yeer, til thei camen in to the lond abitable; thei weren fed with this mete til thei touchiden the endis of the lond of Canaan.
36 (Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)
Forsothe gomor is the tenthe part of efy.