< Kutoka 16 >

1 Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.
And they journey from Elim, and all the congregation of the sons of Israel come to the wilderness of Sin, which [is] between Elim and Sinai, on the fifteenth day of the second month of their going out from the land of Egypt.
2 Huko jangwani hiyo jumuiya yote wakawanungʼunikia Mose na Aroni.
And all the congregation of the sons of Israel murmur against Moses and against Aaron in the wilderness;
3 Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungelikufa kwa mkono wa Bwana huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”
and the sons of Israel say to them, “Oh that we had died by the hand of YHWH in the land of Egypt, in our sitting by the flesh-pot, in our eating bread to satiety—for you have brought us out to this wilderness to put all this assembly to death with hunger.”
4 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nitanyesha mikate kutoka mbinguni kwa ajili yenu. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.
And YHWH says to Moses, “Behold, I am raining bread from the heavens for you—and the people have gone out and gathered the matter of a day in its day—so that I try them whether they walk in My law or not;
5 Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”
and it has been on the sixth day, that they have prepared that which they bring in, and it has been double above that which they gather day [by] day.”
6 Kwa hiyo Mose na Aroni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kwamba Bwana ndiye aliwatoa Misri,
And Moses says—Aaron also—to all the sons of Israel, “Evening—and you have known that YHWH has brought you out from the land of Egypt;
7 kisha asubuhi mtauona utukufu wa Bwana, kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunungʼunikie?”
and morning—and you have seen the glory of YHWH, in His hearing your murmurings against YHWH, and what [are] we, that you murmur against us?”
8 Pia Mose akasema, “Mtajua kuwa alikuwa Bwana wakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manungʼuniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnungʼuniki dhidi yetu, bali dhidi ya Bwana.”
And Moses says, “In YHWH’s giving to you flesh to eat in the evening, and bread in the morning to satiety—in YHWH’s hearing your murmurings, which you are murmuring against Him, and what [are] we? Your murmurings [are] not against us, but against YHWH.”
9 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zake Bwana, kwa maana amesikia manungʼuniko yenu.’”
And Moses says to Aaron, “Say to all the congregation of the sons of Israel, Come near before YHWH, for He has heard your murmurings”;
10 Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu wa Bwana ukitokeza katika wingu.
and it comes to pass, when Aaron is speaking to all the congregation of the sons of Israel, that they turn toward the wilderness, and behold, the glory of YHWH is seen in the cloud.
11 Bwana akamwambia Mose,
And YHWH speaks to Moses, saying,
12 “Nimesikia manungʼuniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua ya kwamba Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.’”
“I have heard the murmurings of the sons of Israel; speak to them, saying, Between the evenings you eat flesh, and in the morning you are satisfied [with] bread, and you have known that I [am] your God YHWH.”
13 Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na tabaka la umande kuzunguka kambi.
And it comes to pass in the evening, that the quail comes up, and covers the camp, and in the morning there has been the lying of dew around the camp,
14 Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.
and the lying of the dew goes up, and behold, on the face of the wilderness [is] a thin, bare thing, thin as hoarfrost on the earth.
15 Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani. Mose akawaambia, “Huu ndio mkate ambao Bwana amewapa mle.
And the sons of Israel see, and say to one another, “What [is] it?” For they have not known what it [is]; and Moses says to them, “It [is] the bread which YHWH has given to you for food.
16 Hivi ndivyo Bwana alivyoamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishi moja kwa kila mtu mliye naye katika hema yenu.’”
This [is] the thing which YHWH has commanded: Gather of it, each according to his eating, an omer for the counted head; and the number of your persons, take, each, for those in his tent.”
17 Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa, baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.
And the sons of Israel do so, and they gather, he who is [gathering] much, and he who is [gathering] little;
18 Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.
and they measure with an omer, and he who is [gathering] much has nothing over, and he who is [gathering] little has no lack, each according to his eating they have gathered.
19 Kisha Mose akawaambia, “Mtu yeyote asibakize chochote mpaka asubuhi.”
And Moses says to them, “Let no man leave of it until morning”;
20 Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Mose, wakahifadhi kiasi fulani mpaka asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Mose akawakasirikia.
and they have not listened to Moses, and some of them leave of it until morning, and it brings up worms and stinks; and Moses is angry with them.
21 Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.
And they gather it morning by morning, each according to his eating; when the sun has been warm, then it has melted.
22 Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwarifu Mose.
And it comes to pass on the sixth day, they have gathered a second bread, two omers for one, and all the princes of the congregation come in, and declare [it] to Moses.
23 Mose akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Kesho itakuwa siku ya mapumziko, Sabato takatifu kwa Bwana. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini chochote kinachobaki na mkiweke mpaka asubuhi.’”
And he says to them, “It [is] that which YHWH has spoken: A rest—a holy Sabbath to YHWH—[is] tomorrow; that which you bake, bake; and that which you boil, boil; and all that is remaining, let [it] rest for yourselves for preservation until the morning.”
24 Kwa hiyo wakavihifadhi mpaka asubuhi, kama Mose alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.
And they let it rest until the morning, as Moses has commanded, and it has not stunk, and a worm has not been in it.
25 Mose akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwa Bwana. Hamtapata chochote juu ya nchi leo.
And Moses says, “Eat it today, for today [is] a Sabbath to YHWH; today you do not find it in the field:
26 Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwepo chochote.”
six days you gather it, and in the seventh day—the Sabbath—there is none in it.”
27 Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata chochote.
And it comes to pass on the seventh day, some of the people have gone out to gather, and have not found.
28 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu mpaka lini?
And YHWH says to Moses, “How long have you refused to keep My commands and My laws?
29 Fahamuni kuwa Bwana amewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”
See, because YHWH has given the Sabbath to you, therefore He is giving to you on the sixth day bread of two days; each abide [in] his place, no one goes out from his place on the seventh day.”
30 Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.
And the people rest on the seventh day,
31 Watu wa Israeli wakaita ile mikate mana Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.
and the house of Israel calls its name Manna, and it [is] as white coriander seed; and its taste [is] as a cake with honey.
32 Mose akasema, “Hivi ndivyo alivyoagiza Bwana: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’”
And Moses says, “This [is] the thing which YHWH has commanded: Fill the omer with it, for a charge for your generations, so that they see the bread which I have caused you to eat in the wilderness, in My bringing you out from the land of Egypt.”
33 Kwa hiyo Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele za Bwana ili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”
And Moses says to Aaron, “Take one pot, and put the fullness of the omer of manna [in] there, and let it rest before YHWH, for a charge for your generations”;
34 Kama Bwana alivyomwagiza Mose, hatimaye Aroni alikuja kuihifadhi ndani ya Sanduku la Ushuhuda.
as YHWH has given command to Moses, so Aaron lets it rest before the Testimony, for a charge.
35 Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana hadi walipofika mpakani mwa Kanaani.
And the sons of Israel have eaten the manna [for] forty years, until their coming to the land to be inhabited; they have eaten the manna until their coming to the extremity of the land of Canaan.
36 (Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)
And the omer is a tenth of the ephah.

< Kutoka 16 >