< Kutoka 14 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse, et dit:
2 “Waambie Waisraeli wageuke nyuma na wapige kambi karibu na Pi-Hahirothi, kati ya Migdoli na bahari. Watapiga kambi kando ya bahari, mkabala na Baal-Sefoni.
Parle aux enfants d'Israël, pour qu'ils fassent demi-tour et campent devant Pihahiroth, entre Migdol et la mer, devant Baal Zephon. Vous camperez en face d'elle, près de la mer.
3 Farao atafikiri kwamba, ‘Hao Waisraeli wanatangatanga katika nchi kwa kuchanganyikiwa, nalo jangwa limewafungia.’
Pharaon dira des enfants d'Israël: « Ils sont empêtrés dans le pays. Le désert les a enfermés.
4 Nami nitaufanya moyo wa Farao mgumu, naye atawafuatilia. Lakini nitajipatia utukufu kwa ajili yangu mwenyewe kupitia Farao na jeshi lake lote, nao Wamisri watajua kuwa mimi ndimi Bwana.” Kwa hiyo Waisraeli wakafanya hivyo.
J'endurcirai le cœur de Pharaon, et il les suivra; je m'assurerai la gloire sur Pharaon et sur toutes ses armées, et les Égyptiens sauront que je suis Yahvé. » C'est ce qu'ils firent.
5 Mfalme wa Misri alipoambiwa kuwa Waisraeli wamekimbia, Farao na maafisa wake wakabadili nia zao kuhusu Waisraeli, wakasema, “Tumefanya nini? Tumewaachia Waisraeli waende zao na tumeukosa utumishi wao!”
On apprit au roi d'Égypte que le peuple s'était enfui; le cœur de Pharaon et de ses serviteurs fut changé à l'égard du peuple, et ils dirent: « Qu'avons-nous donc fait, pour laisser Israël s'enfuir loin de nous? »
6 Kwa hiyo akaandaliwa gari lake la vita, naye akaenda pamoja na jeshi lake.
Il prépara son char et prit avec lui son armée;
7 Akachukua magari bora mia sita, pamoja na magari mengine yote ya Misri, pamoja na maafisa wa magari hayo yote.
il prit six cents chars d'élite et tous les chars d'Égypte, avec des chefs sur chacun d'eux.
8 Bwana akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, kwa hiyo akawafuatia Waisraeli, waliokuwa wakiondoka Misri kwa ujasiri.
Yahvé endurcit le cœur de Pharaon, roi d'Égypte, et il poursuivit les enfants d'Israël, car les enfants d'Israël sortaient avec une main levée.
9 Nao Wamisri, yaani farasi wote wa Farao na magari ya vita, wapanda farasi na vikosi vya askari, wakawafuatia Waisraeli, wakawakuta karibu na Pi-Hahirothi, mkabala na Baal-Sefoni walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari.
Les Égyptiens les poursuivirent. Tous les chevaux et les chars de Pharaon, ses cavaliers et son armée les rattrapèrent en campant près de la mer, à côté de Pihahiroth, devant Baal Zephon.
10 Farao alipokaribia, Waisraeli wakainua macho yao, wakawaona Wamisri wakija nyuma yao. Wakashikwa na hofu, wakamlilia Bwana.
Lorsque Pharaon s'approcha, les enfants d'Israël levèrent les yeux, et voici que les Égyptiens marchaient à leur poursuite; ils eurent très peur. Les enfants d'Israël crièrent à Yahvé.
11 Wakamwambia Mose, “Je, ni kwamba hayakuwako makaburi huko Misri hata umetuleta tufe huku jangwani? Umetufanyia nini kututoa Misri?
Ils dirent à Moïse: « Parce qu'il n'y avait pas de tombeaux en Égypte, nous as-tu emmenés mourir dans le désert? Pourquoi nous as-tu traités de la sorte, pour nous faire sortir d'Égypte?
12 Hatukukuambia tulipokuwa huko Misri, tuache tuwatumikie Wamisri? Ingekuwa vyema zaidi kwetu kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani!”
N'est-ce pas là la parole que nous t'avons adressée en Égypte, en te disant: « Laisse-nous tranquilles, pour que nous servions les Égyptiens »? Car il aurait mieux valu pour nous servir les Égyptiens que de mourir dans le désert. »
13 Mose akawajibu Waisraeli, “Msiogope. Simameni imara, nanyi mtauona wokovu Bwana atakaowapatia leo. Hao Wamisri mnaowaona leo kamwe hamtawaona tena.
Moïse dit au peuple: « N'ayez pas peur. Restez immobiles et voyez le salut de l'Éternel, qu'il va opérer pour vous aujourd'hui, car vous ne verrez plus jamais les Égyptiens que vous avez vus aujourd'hui.
14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mnatakiwa kutulia tu.”
L'Éternel combattra pour vous, et vous resterez tranquilles. »
15 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Kwa nini wewe unanililia? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
Yahvé dit à Moïse: « Pourquoi cries-tu vers moi? Parle aux enfants d'Israël, pour qu'ils avancent.
16 Inua fimbo yako na unyooshe mkono wako juu ya bahari ili kuyagawa maji, hivyo kwamba Waisraeli wapate kupita mahali pakavu baharini.
Lève ta verge, étends ta main sur la mer et divise-la. Les enfants d'Israël entreront à sec au milieu de la mer.
17 Nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu kusudi waingie baharini wakiwafuatia. Nami nitajipatia utukufu kupitia Farao pamoja na jeshi lake lote, kupitia magari yake ya vita na wapanda farasi wake.
Voici, je vais moi-même endurcir le cœur des Égyptiens, et ils entreront après eux. Je me rendrai maître de Pharaon et de toutes ses armées, de ses chars et de ses cavaliers.
18 Nao Wamisri watajua kwamba Mimi ndimi Bwana nitakapojipatia utukufu kupitia Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake.”
Les Égyptiens sauront que je suis Yahvé, quand je me serai acquis la gloire sur Pharaon, sur ses chars et sur ses cavaliers. »
19 Ndipo malaika wa Mungu, aliyekuwa akisafiri mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akakaa nyuma yao. Pia ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao na kusimama nyuma,
L'ange de Dieu, qui marchait devant le camp d'Israël, se déplaça et alla derrière eux; et la colonne de nuée se déplaça de devant eux, et se tint derrière eux.
20 ikakaa kati ya majeshi ya Misri na Israeli. Usiku kucha wingu likaleta giza upande mmoja na nuru kwa upande mwingine, kwa hiyo hakuna aliyemkaribia mwenzake usiku kucha.
Elle se plaça entre le camp d'Égypte et le camp d'Israël. Il y avait la nuée et les ténèbres, et pourtant elle donnait de la lumière pendant la nuit. L'un ne s'approchait pas de l'autre de toute la nuit.
21 Ndipo Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika,
Moïse étendit sa main sur la mer, et Yahvé fit reculer la mer par un fort vent d'est toute la nuit; il mit la mer à sec, et les eaux se partagèrent.
22 nao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
Les enfants d'Israël entrèrent au milieu de la mer à sec, et les eaux formaient pour eux une muraille à droite et à gauche.
23 Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi.
Les Égyptiens les poursuivirent et entrèrent après eux au milieu de la mer: tous les chevaux de Pharaon, ses chars et ses cavaliers.
24 Karibia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha.
A la veille du matin, Yahvé regarda l'armée égyptienne à travers la colonne de feu et de nuée, et il confondit l'armée égyptienne.
25 Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”
Il enleva les roues de leurs chars et les fit rouler lourdement, si bien que les Égyptiens dirent: « Fuyons devant Israël, car Yahvé combat pour eux contre les Égyptiens! ».
26 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.”
Yahvé dit à Moïse: « Étends ta main sur la mer, afin que les eaux reviennent sur les Égyptiens, sur leurs chars et sur leurs cavaliers. »
27 Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari.
Moïse étendit sa main sur la mer, et la mer reprit sa force à l'apparition du matin; les Égyptiens s'enfuirent devant elle. Yahvé renversa les Égyptiens au milieu de la mer.
28 Maji yakarudiana na kuyafunika magari ya vita na wapanda farasi pamoja na jeshi lote la Farao lililokuwa limewafuata Waisraeli ndani ya bahari. Hakuna hata mmoja wao aliyenusurika.
Les eaux revinrent et couvrirent les chars et les cavaliers, toute l'armée de Pharaon qui entra après eux dans la mer. Il n'en resta pas un seul.
29 Lakini Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, ukiwepo ukuta wa maji upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
Mais les enfants d'Israël marchaient à sec au milieu de la mer, et les eaux leur servaient de muraille à droite et à gauche.
30 Siku ile Bwana akawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri, nao Waisraeli wakawaona Wamisri wamelala ufuoni mwa bahari wakiwa wamekufa.
Ce jour-là, Yahvé sauva Israël de la main des Égyptiens, et Israël vit les Égyptiens morts au bord de la mer.
31 Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa Bwana aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa Bwana na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Mose mtumishi wake.
Israël vit la grande œuvre que Yahvé avait faite aux Égyptiens, et le peuple craignit Yahvé; et ils crurent en Yahvé et en son serviteur Moïse.

< Kutoka 14 >