< Kutoka 14 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Forsothe the Lord spak to Moises, and seide, Speke thou to the sones of Israel;
2 “Waambie Waisraeli wageuke nyuma na wapige kambi karibu na Pi-Hahirothi, kati ya Migdoli na bahari. Watapiga kambi kando ya bahari, mkabala na Baal-Sefoni.
turne thei ayen, and sette thei tentis euene ayens Fiayroth, which is bitwixe Magdalum and the see, ayens Beelsefon; in the siyt therof ye schulen sette tentis ouer the see.
3 Farao atafikiri kwamba, ‘Hao Waisraeli wanatangatanga katika nchi kwa kuchanganyikiwa, nalo jangwa limewafungia.’
And Farao schal seie on the sones of Israel, Thei ben maad streit in the lond, the deseert hath closid hem to gidere.
4 Nami nitaufanya moyo wa Farao mgumu, naye atawafuatilia. Lakini nitajipatia utukufu kwa ajili yangu mwenyewe kupitia Farao na jeshi lake lote, nao Wamisri watajua kuwa mimi ndimi Bwana.” Kwa hiyo Waisraeli wakafanya hivyo.
And Y schal make hard his herte, and he schal pursue you, and Y schal be glorified in Farao, and in al his oost; and Egipcians schulen wite that Y am the Lord; and thei diden so.
5 Mfalme wa Misri alipoambiwa kuwa Waisraeli wamekimbia, Farao na maafisa wake wakabadili nia zao kuhusu Waisraeli, wakasema, “Tumefanya nini? Tumewaachia Waisraeli waende zao na tumeukosa utumishi wao!”
And it was teld to the kyng of Egipcians, that the puple hadde fled; and the herte of Farao and of hise seruauntis was chaungid on the puple, and thei seiden, What wolden we do, that we leften Israel, that it schulde not serue us?
6 Kwa hiyo akaandaliwa gari lake la vita, naye akaenda pamoja na jeshi lake.
Therfor Farao ioynede the chare, and took with him al his puple;
7 Akachukua magari bora mia sita, pamoja na magari mengine yote ya Misri, pamoja na maafisa wa magari hayo yote.
and he took sixe hundrid chosyn charis, and what euer thing of charis was in Egipt, and duykis of al the oost.
8 Bwana akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, kwa hiyo akawafuatia Waisraeli, waliokuwa wakiondoka Misri kwa ujasiri.
And the Lord made hard `the herte of Farao, kyng of Egipt, and he pursuede the sones of Israel; and thei weren go out in an hiy hond.
9 Nao Wamisri, yaani farasi wote wa Farao na magari ya vita, wapanda farasi na vikosi vya askari, wakawafuatia Waisraeli, wakawakuta karibu na Pi-Hahirothi, mkabala na Baal-Sefoni walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari.
And whanne Egipcians pursueden the steppis of the sones of Israel bifor goynge, thei founden hem in tentis on the see; al the chyualrye and charis of Farao, and al the oost weren in Fiayroth, ayens Beelsefon.
10 Farao alipokaribia, Waisraeli wakainua macho yao, wakawaona Wamisri wakija nyuma yao. Wakashikwa na hofu, wakamlilia Bwana.
And whanne Farao hadde neiyed the sones of Israel, reisiden her iyen, and thei sien Egipcians bihynde hem, and dredden greetli; and thei crieden to the Lord,
11 Wakamwambia Mose, “Je, ni kwamba hayakuwako makaburi huko Misri hata umetuleta tufe huku jangwani? Umetufanyia nini kututoa Misri?
and seiden to Moises, In hap sepulcris weren not in Egipt, therfor thou hast take vs awei, that we schulen die in wildirnesse? what woldist thou do this, that thou leddist vs out of Egipt?
12 Hatukukuambia tulipokuwa huko Misri, tuache tuwatumikie Wamisri? Ingekuwa vyema zaidi kwetu kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani!”
Whether this is not the word which we spaken to thee in Egipt, `and seiden, Go awei fro vs, that we serue Egipcians? for it is myche betere to serue hem, than to die in wildirnesse.
13 Mose akawajibu Waisraeli, “Msiogope. Simameni imara, nanyi mtauona wokovu Bwana atakaowapatia leo. Hao Wamisri mnaowaona leo kamwe hamtawaona tena.
And Moises seide to the puple, Nyle ye drede, stonde ye, and `se ye the grete werkys of God, whiche he schal do to dai; for ye schulen no more se Egipcians, whiche ye seen now, til in to with outen ende;
14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mnatakiwa kutulia tu.”
the Lord schal fiyte for you, and ye schulen be stille.
15 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Kwa nini wewe unanililia? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
And the Lord seide to Moises, What criest thou to me? Speke thou to the sones of Israel, that thei go forth; forsothe reise thou thi yerde,
16 Inua fimbo yako na unyooshe mkono wako juu ya bahari ili kuyagawa maji, hivyo kwamba Waisraeli wapate kupita mahali pakavu baharini.
and stretche forth thin hond on the see, and departe thou it, that the sones of Israel go in the myddis of the see, by drie place.
17 Nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu kusudi waingie baharini wakiwafuatia. Nami nitajipatia utukufu kupitia Farao pamoja na jeshi lake lote, kupitia magari yake ya vita na wapanda farasi wake.
Forsothe Y schal make hard the herte of Egipcians, that thei pursue you, and Y schal be glorified in Farao, and in al the oost of hym, and in the charis, and in the knyytis of hym;
18 Nao Wamisri watajua kwamba Mimi ndimi Bwana nitakapojipatia utukufu kupitia Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake.”
and Egipcians schulen wite that Y am the Lord God, whanne Y schal be glorified in Farao, and in the charis, and in the knyytis of hym.
19 Ndipo malaika wa Mungu, aliyekuwa akisafiri mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akakaa nyuma yao. Pia ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao na kusimama nyuma,
And the aungel of the Lord, that yede bifore the castellis of Israel, took hym silf, and yede bihynde hem; and the piler of cloude yede to gidir with hym, and lefte the formere thingis aftir the bak,
20 ikakaa kati ya majeshi ya Misri na Israeli. Usiku kucha wingu likaleta giza upande mmoja na nuru kwa upande mwingine, kwa hiyo hakuna aliyemkaribia mwenzake usiku kucha.
and stood bitwixe the `castels of Egipcians and castels of Israel; and the cloude was derk toward Egipcians, and liytnynge `the nyyt toward `the children of Israel, so that in al the tyme of the niyt thei miyten not neiy togidere to hem silf.
21 Ndipo Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika,
And whanne Moises hadde stretchid forth the hond on the see, the Lord took it awei, the while a greet wynde and brennynge blew in al the niyt, and turnede in to dryenesse; and the watir was departid.
22 nao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
And the sones of Israel entriden by the myddis of the drye see; for the watir was as a wal at the riyt side and left side of hem.
23 Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi.
And Egipcians pursueden, and entriden aftir hem, al the ridyng of Farao, hise charis, and knyytis, bi the myddis of the see.
24 Karibia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha.
And the wakyng of the morewtid cam thanne, and lo! the Lord bihelde on the castels of Egipcians, bi a piler of fier, and of cloude, and killide the oost of hem; and he destriede the wheelis of charis,
25 Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”
and tho weren borun in to the depthe. Therfor Egipcians seiden, Fle we Israel; for the Lord fiytith for hem ayenus vs.
26 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.”
And the Lord seide to Moises, Holde forth thin hond on the see, that the watris turne ayen to Egipcians, on the charis, and knyytis of hem.
27 Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari.
And whanne Moises hadde hold forth the hoond ayens the see, it turnede ayen first in the morewtid to the formere place; and whanne Egipcians fledden, the watris camen ayen, and the Lord wlappide hem in the myddis of the floodis.
28 Maji yakarudiana na kuyafunika magari ya vita na wapanda farasi pamoja na jeshi lote la Farao lililokuwa limewafuata Waisraeli ndani ya bahari. Hakuna hata mmoja wao aliyenusurika.
And the watris turneden ayen, and hiliden the charis, and knyytis of al the oost of Farao, which sueden, and entriden in to the see; sotheli not oon of hem was alyue.
29 Lakini Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, ukiwepo ukuta wa maji upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.
Forsothe the sones of Israel yeden thorouy the myddis of the drye see, and the watris weren to hem as for a wal, on the riyt side and left side.
30 Siku ile Bwana akawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri, nao Waisraeli wakawaona Wamisri wamelala ufuoni mwa bahari wakiwa wamekufa.
And in that dai the Lord delyuerede Israel fro the hond of Egipcians, and thei sien Egipcians deed on the brynke of the see,
31 Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa Bwana aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa Bwana na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Mose mtumishi wake.
and thei seiyen the greet hond which the Lord hadde vsid ayens hem; and the puple dredde the Lord, and thei bileueden to the Lord, and to Moises his seruaunt.

< Kutoka 14 >