< Kutoka 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
»Posvéti mi vse prvorojeno, karkoli odpre maternico med Izraelovimi otroki, tako od ljudi in od živali. To je moje.«
3 Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
Mojzes je rekel ljudstvu: »Spominjajte se tega dne, na katerega ste prišli iz Egipta, iz hiše sužnosti; kajti z močjo roke vas je Gospod privedel iz tega kraja. Tam se ne bo jedlo nič kvašenega kruha.
4 Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
Ta dan ste prišli ven v mesecu abíbu.
5 Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
Zgodilo se bo, ko vas bo Gospod privedel v deželo Kánaancev, Hetejcev, Amoréjcev, Hivéjcev in Jebusejcev, ki jo je prisegel vašim očetom, da vam jo da, deželo, kjer tečeta mleko in med, da se boš v tem mesecu držal te službe.
6 Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
Sedem dni boš jedel nekvašeni kruh in na sedmi dan bo praznik Gospodu.
7 Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
Nekvašeni kruh se bo jedel sedem dni in tam pri tebi naj ne bo videti nobenega kvašenega kruha niti ne bo kvasa s teboj v vseh tvojih četrtih.
8 Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
Tistega dne boš svojemu sinu pokazal, rekoč: › To je storjeno zaradi tega, kar mi je storil Gospod, ko sem izšel iz Egipta.‹
9 Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
To ti bo za znamenje na tvoji roki in za spomin med tvojimi očmi, da bo lahko Gospodova postava v tvojih ustih, kajti z močno roko te je Gospod privedel iz Egipta.
10 Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
Držal se boš torej te odredbe v njenem času iz leta v leto.
11 “Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
Zgodilo se bo, ko te bo Gospod pripeljal v deželo Kánaancev, kakor je prisegel tebi in tvojim očetom in ti jo bo dal,
12 inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
da boš oddvojil Gospodu vse, kar odpre maternico in vsak prvenec, ki pride iz živali, ki jo imaš; samci bodo Gospodovi.
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
Vsakega prvenca osla pa boš odkupil z jagnjetom. Če pa ga ne boš odkupil, potem mu boš zlomil tilnik. Med svojimi otroki boš odkupil vsakega moškega prvorojenca.
14 “Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
Zgodilo se bo, ko te tvoj sin vpraša, v času, ki pride, rekoč: ›Kaj je to?‹ da mu boš rekel: ›Z močjo roke nas je Gospod privedel iz Egipta, iz hiše sužnosti.
15 Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
Pripetilo se je, ko nas je faraon komajda odpustil, da je Gospod usmrtil vse prvorojene v egiptovski deželi, tako prvorojene od človeka, kakor prvorojene od živali.‹ Zato žrtvujem Gospodu vse, kar odpre maternico in so samci. Toda vse prvorojene izmed svojih otrok odkupim.
16 Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
To bo za simbol na tvoji roki in za načelek med tvojimi očmi, kajti z močjo roke nas je Gospod privedel iz Egipta.«
17 Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
Pripetilo se je, ko je faraon ljudstvu pustil oditi, da jih Bog ni vodil po poti dežele Filistejcev, čeprav je bila ta blizu, kajti Bog je rekel: »Da se ne bi morda ljudstvo pokesalo, ko zagleda vojno in se vrnejo v Egipt, «
18 Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
ampak je Bog ljudstvo vodil naokoli, po poti divjine Rdečega morja in Izraelovi otroci so se postrojeni dvignili iz egiptovske dežele.
19 Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
Mojzes je s seboj vzel Jožefove kosti, kajti ta je strogo zaprisegel Izraelove otroke, rekoč: »Bog vas bo zagotovo obiskal; in vi boste s seboj odnesli moje kosti proč od tod.«
20 Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
In napotili so se na svoje potovanje iz Sukóta in se utaborili v Etámu, na robu divjine.
21 Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
In Gospod je hodil podnevi pred njimi v oblačnem stebru, da jih vodi po poti, ponoči pa v ognjenem stebru, da jim daje svetlobo, da bi hodili podnevi in ponoči.
22 Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.
Izpred ljudstva ni vzel proč oblačnega stebra podnevi niti ognjenega stebra ponoči.

< Kutoka 13 >