< Kutoka 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse, et dit:
2 “Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
« Sanctifie-moi tout premier-né, tout ce qui ouvre le ventre des enfants d'Israël, tant des hommes que des animaux. Il est à moi. »
3 Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
Moïse dit au peuple: « Souvenez-vous de ce jour où vous êtes sortis d'Égypte, de la maison de servitude, car c'est par la force de sa main que Yahvé vous a fait sortir de ce lieu. On ne mangera pas de pain levé.
4 Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
Aujourd'hui, vous sortez au mois d'Abib.
5 Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
Lorsque Yahvé vous fera entrer dans le pays des Cananéens, des Héthiens, des Amoréens, des Héviens et des Jébusiens, qu'il a juré à vos pères de vous donner, un pays où coulent le lait et le miel, vous célébrerez cet office pendant ce mois.
6 Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
Pendant sept jours, vous mangerez des pains sans levain, et le septième jour, vous ferez une fête en l'honneur de l'Éternel.
7 Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
On mangera des pains sans levain pendant les sept jours; on ne verra pas avec vous de pain levé. On ne verra pas de levure avec vous, dans tout votre territoire.
8 Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
En ce jour-là, tu diras à ton fils: « C'est à cause de ce que Yahvé a fait pour moi, quand je suis sorti d'Égypte ».
9 Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
Ce sera pour toi un signe sur ta main et un souvenir entre tes yeux, afin que la loi de l'Éternel soit dans ta bouche; car c'est d'une main forte que l'Éternel t'a fait sortir d'Égypte.
10 Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
Tu observeras donc cette ordonnance en son temps, d'année en année.
11 “Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
« Lorsque Yahvé vous fera entrer dans le pays des Cananéens, comme il l'a juré à vous et à vos pères, et qu'il vous le donnera,
12 inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
vous réserverez à Yahvé tout ce qui ouvre le ventre et tout premier-né d'un animal que vous avez. Les mâles appartiendront à Yahvé.
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
Tout premier-né d'un âne, tu le rachèteras avec un agneau; si tu ne le rachètes pas, tu lui briseras le cou; et tu rachèteras tous les premiers-nés de l'homme parmi tes fils.
14 “Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
Lorsque ton fils te demandera un jour: « Qu'est-ce que cela? », tu lui diras: « C'est par la force de sa main que Yahvé nous a fait sortir d'Égypte, de la maison de servitude.
15 Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
Lorsque Pharaon s'est obstiné à ne pas nous laisser partir, Yahvé a tué tous les premiers-nés du pays d'Égypte, aussi bien les premiers-nés des hommes que ceux du bétail. C'est pourquoi je sacrifie à Yahvé tout ce qui ouvre les entrailles, c'est-à-dire les mâles; mais je rachète tous les premiers-nés de mes fils'.
16 Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
Ce sera un signe sur ta main et des symboles entre tes yeux, car c'est par la force de la main que Yahvé nous a fait sortir d'Égypte. »
17 Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
Lorsque Pharaon eut laissé partir le peuple, Dieu ne le conduisit pas par le chemin du pays des Philistins, qui était pourtant tout proche, car Dieu dit: « De peur que le peuple ne change d'avis en voyant la guerre, et qu'il ne retourne en Égypte »;
18 Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
mais Dieu conduisit le peuple par le chemin du désert, près de la mer Rouge; et les enfants d'Israël montèrent armés hors du pays d'Égypte.
19 Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
Moïse prit avec lui les ossements de Joseph, car il avait fait jurer les enfants d'Israël en disant: « Dieu vous visitera et vous emporterez avec vous mes ossements loin d'ici. »
20 Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
Ils partirent de Succoth et campèrent à Étham, à l'extrémité du désert.
21 Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
L'Éternel marchait devant eux, le jour dans une colonne de nuée, pour les conduire sur leur chemin, et la nuit dans une colonne de feu, pour les éclairer, afin qu'ils pussent marcher de jour et de nuit.
22 Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.
La colonne de nuée, le jour, et la colonne de feu, la nuit, ne s'écartaient pas de devant le peuple.

< Kutoka 13 >