< Kutoka 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Also the Lord spak to Moises, and seide,
2 “Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
Halewe thou to me ech firste gendrid thing that openeth the wombe among the sones of Israel, as wel of men as of beestis, for whi alle ben myn.
3 Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
And Moises seide to the puple, Haue ye mynde of this dai, in which ye yeden out of Egipt, and of the hows of seruage, for in strong hond the Lord ledde you out of this place, that ye ete not breed diyt with sour dow.
4 Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
To dai ye gon out, in the monethe of new fruytis;
5 Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
and whanne the Lord hath led thee in to the lond of Cananey, and of Ethei, and of Amorrei, and of Euei, and of Jebusei, which lond he swoor to thi fadris, that he schulde yyue to thee, a lond flowynge with mylk and hony, thou schalt halowe this custom of holy thingis in this monethe.
6 Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
In seuene daies thou schalt ete therf looues, and the solempnete of the Lord schal be in the seuenthe dai;
7 Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
ye schulen ete therf looues seuene daies, no thing diyt with sour dow schal appere at thee, nether in alle thi coostis.
8 Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
And thou schalt telle to thi sone in that dai, and schalt seie, This it is that the Lord dide to me, whanne Y yede out of Egipt.
9 Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
And it schal be as a signe in thin hond, and as a memorial before thin iyen, and that the lawe of the Lord be euere in thi mouth; for in a strong hond the Lord ledde thee out of Egipt, and of the hows of seruage.
10 Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
Thou schalt kepe siche a worschipyng in tyme ordeined, `fro daies in to daies.
11 “Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
And whanne the Lord hath brouyt thee in to the lond of Cananey, as he swoor to thee, and to thi fadris, and hath youe it to thee,
12 inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
thou schalt departe to the Lord al the thing that openeth the wombe, and that that is the firste in thi beestis; what euer thing thou hast of male kynde, thou schalt halewe to the Lord.
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
Thou schalt chaunge the firste gendrid of an asse for a scheep, that if thou ayen biest not, thou schalt sle; forsothe thou schalt ayen bie with prijs al the firste gendrid of man of thi sones.
14 “Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
And whanne thi sone schal axe thee to morewe, and seie, What is this? thou schalt answere to hym, In a strong hond the Lord ladde vs out of the lond of Egipt, of the hows of seruage; for whanne Farao was maad hard,
15 Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
and nolde delyuere vs, the Lord killide alle the firste gendrid thing in the lond of Egipt, fro the firste gendrid of man til to the firste gendrid of beestis; therfor Y offre to the Lord al thing of male kynde that openeth the wombe, and Y ayen bie alle the firste gendrid thingis of my sones.
16 Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
Therfor it schal be as a signe in thin hond, and as a thing hangid for mynde bifore thin iyen, for in a strong hond the Lord ledde vs out of Egipt.
17 Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
Therfor whanne Farao hadde sent out the puple, God ledde not hem out bi the weie of `the lond of Filisteis, which is niy; and arettid lest perauenture it wolde repente the puple, if he had seyn batelis rise ayens hym, and `the puple wolde turn ayen in to Egipt;
18 Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
but God ledde aboute by the weie of deseert, which weie is bisidis the reed see. And the sones of Israel weren armed, and stieden fro the lond of Egipte.
19 Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
And Moises took the boonus of Joseph with hym, for he hadde chargid the sones of Israel, and hadde seid, God schal visite you, and bere ye out `fro hennus my boonus with you.
20 Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
And thei yeden forth fro Socoth, and settiden tentis in Etham, in the laste endis of wildirnesse.
21 Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
Forsothe the Lord yede bifore hem to schewe the weie, bi dai in a piler of clowde, and bi nyyt in a piler of fier, that he schulde be ledere of the weie in euer either time;
22 Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.
the piler of clowde failide neuere bi dai, nether the piler of fier bi niyt, bifor the puple.

< Kutoka 13 >