< Kutoka 13 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh said to Moses/me,
2 “Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
“Set apart all the firstborn males in order that they may belong to me. The firstborn males of the Israeli people and of their animals will be mine.”
3 Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
Moses/I said to the people, “Do not forget this day! This is the day that you are leaving Egypt. This is the day you [are freed from] being their slaves. Yahweh has brought you out of Egypt by his great power [MTY]. Do not eat any bread that has yeast in it [whenever you celebrate] this day.
4 Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
You are leaving Egypt on this day, which is the first day of the month that is [named] Abib.
5 Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
Later, when Yahweh brings you into the land where the descendants of Canaan, Heth, Amor, Hiv, and Jebus [now live], the land that he solemnly promised to give to you, a land that will be very good for raising livestock and growing crops [MTY], you must celebrate this festival during this month [every year].
6 Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
For seven days the bread that you eat must not have any yeast in it. On the seventh day there must be a festival to [honor] Yahweh.
7 Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
For seven days do not eat bread that has yeast in it. You should not have any yeast or bread made with yeast anywhere in your land.
8 Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
On the day [the festival starts], you must tell your children, ‘[We are doing this to remember] what Yahweh did for our ancestors when they left Egypt.
9 Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
This ritual will remind you how Yahweh brought your ancestors out of Egypt with his great power [MTY]. [The ritual will be like something] you tie on your forehead or on your wrist. It will remind you to recite to others what Yahweh has instructed you.
10 Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
So you must celebrate this festival every year at the time [Yahweh] has appointed.’
11 “Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
Yahweh will bring you into the land where the descendants of Canaan live, just as he promised you and your ancestors that he would do. When he gives that land to you,
12 inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
you must dedicate to Yahweh the firstborn males of all your animals. These all will belong to Yahweh.
13 Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
You may keep the firstborn male donkeys, but you must buy them back by sacrificing a lamb as a substitute for the donkey. If you do not want to buy back the donkey, you must [kill it by] breaking its neck. You must also buy back every one of your own firstborn sons.
14 “Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
In the future, when one of your children asks, ‘What does this mean?’, you must say to him, ‘Yahweh brought our ancestors out of Egypt with his great power [MTY], and freed us from being slaves there.
15 Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
The king of Egypt stubbornly refused to let them leave his country, so Yahweh killed all the firstborn males in Egypt, both the boys and the firstborn of their livestock. That is why we now sacrifice to Yahweh all the firstborn of our livestock, but we buy back our own firstborn sons.’
16 Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
I repeat that this ritual will remind you about how Yahweh brought our [ancestors] out of Egypt by his great power [MTY]; it will be like something you tie on your wrist or on your forehead [to remind you of that].”
17 Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
When the king [of Egypt] let the [Israeli] people go, God did not lead them to go through the land of the Philistines. That was a shorter way, but God said, “It would be bad if my people change their minds when they realize that they will have to fight [the Philistines to take their land], and then [decide to] return to Egypt.”
18 Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
Instead, God led them to go around through the desert toward the Red Sea (OR, the Gulf of Suez). When the Israeli people left Egypt, they were carrying weapons to fight [their enemies].
19 Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
Moses/I [had them] take along the bones of Joseph with them/us, because Joseph long ago had made the Israeli people promise solemnly that they would do that. He had said to them, “God will enable your descendants to leave Egypt. When that happens, you must carry my bones with you.”
20 Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
The Israeli people left Succoth and traveled to Etham, at the edge of the desert, and they set up their tents there.
21 Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
[When they traveled] during the daytime, Yahweh went in front of them in a tall [white] cloud to show them the way. During the night, he went in front of them in a tall cloud that looked like a fire. By doing that, he enabled them to travel in the daytime and also at nighttime.
22 Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.
The tall cloud did not leave them. It was always in front of them, as a bright white cloud in the daytime and like a fire at night.

< Kutoka 13 >