< Kutoka 12 >

1 Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
Also the Lord seide to Moises and Aaron in the lond of Egipt,
2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
This monethe, the bigynnyng of monethis to you, schal be the firste in the monethis of the yeer.
3 Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
Speke ye to al the cumpanye of the sones of Israel, and seie ye to hem, In the tenthe dai of this monethe ech man take a lomb by hise meynees and housis;
4 Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
but if the noumbre is lesse, that it may not suffice to ete the lomb, he schal take his neiybore, which is ioyned to his hows, bi the noumbre of soulis, that moun suffice to the etyng of the lomb.
5 Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
Forsothe the lomb schal be a male of o yeer, without wem; bi which custom ye schulen take also a kide;
6 Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
and ye schulen kepe hym til to the fouretenthe dai of this monethe; and al the multitude of the sones of Israel schal offre hym at euentid.
7 Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
And thei schulen take of his blood, and schulen put on euer either post, and in lyntels, `ether hiyer threschfoldis, of the housis, in whiche thei schulen ete hym;
8 Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
and in that niyt thei schulen ete fleischis, roostid with fier, and therf looues, with letusis of the feeld.
9 Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
Ye schulen not ete therof ony raw thing, nether sodun in watir, but roostid oneli by fier; ye schulen deuoure the heed with feet and entrailis therof;
10 Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
nether ony thing therof schal abide til the morewtid; if ony thing is residue, ye schulen brenne in the fier.
11 Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
Forsothe thus ye schulen ete hym; ye schulen girde youre reynes, and ye schulen haue schoon in the feet, and ye schulen holde stauys in hondis, and ye schulen ete hastili; for it is fase, that is, the passyng of the Lord.
12 “Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
And Y schal passe thorou the lond of Egipt in that niyt, and Y schal smyte al the firste gendrid thing in the lond of Egipt, fro man til to beeste; and Y the Lord schal make domes in alle the goddis of Egipt.
13 Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
Forsothe blood schal be to you in to signe, in the housis in whiche ye schulen be; and Y schal se the blood, and Y schal passe you; nether a wounde distriynge schal be in you, whanne Y schal smyte the lond of Egipt.
14 “Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
Forsothe ye schulen haue this dai in to mynde, and `ye schulen make it solempne to the Lord in youre generaciouns bi euerlastynge worschipyng.
15 Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
In seuene daies ye schulen ete therf breed; in the firste dai no thing diyt with sour douy schal be in youre housis; who euer schal ete ony thing diyt with sour douy, fro the firste dai til the seuenthe dai, that soule schal perische fro Israel.
16 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
The firste day schal be hooli and solempne, and the seuenthe dai schal be worschipful bi the same halewyng; ye schulen not do ony werk in tho daies, outakun these thingis that perteynen to mete;
17 “Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
and ye schulen kepe therf breed. For in that same dai Y schal lede out of the lond of Egipt youre oost; and ye schulen kepe this dai in youre generaciouns bi euerlastynge custom.
18 Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
In the first monethe, in the fouretenthe dai of the monethe, at euentid, ye schulen ete therf breed, til to the oon and twentithe dai of the same monethe at euentid.
19 Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
In seuene dayes no thing `diyt with sour douy schal be foundun in youre housis; if ony etith ony thing diyt with sour dow, his soule schal perische fro the cumpeny of Israel, as wel of comelyngis, as of hem that ben borun in the lond.
20 Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
Ye schulen not ete ony thing diyt with sour dow, and ye schulen ete therf breed in alle youre dwellyng placis.
21 Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
Forsothe Moises clepide alle the eldre men of the sones of Israel, and seide to hem, Go ye, and take a beeste by youre meynees, and offre ye fase; and dippe ye a bundel of isope,
22 Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
in the blood which `is in the threisfold, and sprynge ye therof the lyntel, and euer either post; noon of you schal go out at the dore of his hows til the morewtid.
23 Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
For the Lord schal passe smytynge Egipcians; and whanne he schal se the blood in the lyntel, and in euer either post, he schal passe the dore of the hows; and he schal not suffre the smytere to entre in to youre housis, and to hirte.
24 “Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
Kepe thou this word; it schal be a lawful thing to thee and to thi sones til in to with outen ende.
25 Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
And whanne ye schulen entre in to the lond which the Lord schal yyue to you, as he bihiyte, ye schulen kepe these cerymonyes;
26 Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
and whanne youre sones schulen seie to you, What is this religioun? ye schulen seie to hem,
27 Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
It is the sacrifice of the passyng of the Lord, whanne he passide ouer the housis of the sones of Israel in Egipt, and smoot Egipcians, and delyueride oure housis. And the puple was bowid, and worschipide.
28 Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
And the sones of Israel yeden out, and diden as the Lord comaundide to Moises and to Aaron.
29 Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
Forsothe it was doon in the myddis of the nyyt, the Lord smoot al the firste gendrid thing in the lond of Egipt, fro the firste gendrid of Farao, that sat in the trone of hym, til to the first gendrid of the caitif womman, that was in the prisoun, and alle the first gendrid of beestis.
30 Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
And Farao roos in the nyyt, and alle hise seruauntis, and al Egipt; and a greet cry was maad in Egipt, for noon hows was, in which a deed man lay not.
31 Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
And whanne Moises and Aaron weren clepid in the nyyt, Farao seide, Rise ye, go ye out fro my puple, bothe ye and the sones of Israel; go ye, offre ye to the Lord, as ye seien;
32 Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
take ye youre scheep and greete beestis, as ye axiden; and go ye, and blesse ye me.
33 Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
And Egipcians constreyneden the puple to go out of the lond swiftli, and seiden, All we schulen die!
34 Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
Therfor the puple took meele spreynd togidere, bifor that it was diyt with sour douy; and boond in mentils, and puttide on her schuldris.
35 Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
And the sones of Israel diden as the Lord comaundide to Moises; and thei axiden of Egipcians siluerne vesselis and goldun, and ful myche clooth.
36 Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
Forsothe the Lord yaf grace to the puple bifor Egipcians, that the Egipcians lenten to hem; and thei maden bare Egipcians.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
And the sones of Israel yeden forth fro Ramasses in to Socoth, almest sixe hundrid thousind of foot men, with out litle children and wymmen;
38 Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
but also comyn puple of malis and femalis vnnoumbrable stieden with hem; scheep, and oxun, and ful many beestis of diuerse kynde, stieden with hem.
39 Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
And thei bakiden meele, which spreynd to gidere `a while ago thei token fro Egipt, and maden therf looues bakun vnder the aischis; for the looues miyten not be diyt with sour dow, for Egipcians compelliden to go out, and suffriden not to make ony tariyng, nether it was leiser to make ony seew.
40 Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
Forsothe the dwellyng of the sones of Israel, bi which thei dwelliden in Egipt, was of foure hundrid and thretti yeer;
41 Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
and whanne tho weren fillid, al the oost of the Lord yede out of the lond of Egipt in the same dai.
42 Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
This nyyt is worthi to be kept in the worschipyng of the Lord, whanne he ladde hem out of the lond of Egipt; alle the sones of Israel owen to kepe this in her generaciouns.
43 Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
Also the Lord seide to Moises and Aaron, This is the religioun of fase; ech alien schal not ete therof;
44 Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
sotheli ech seruaunt bouyt schal be circumcidid, and so he schal ete;
45 lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
a comelyng and hirid man schulen not ete therof;
46 “Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
it schal be etun in oon hows; nether ye schulen bere out of the fleischis therof; nether ye schulen breke a boon therof.
47 Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
Ech company of the sones of Israel schal make that fase;
48 “Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
that if ony pilgrym wole passe into youre feith and worschipyng, and make fase of the Lord, ech male kynde of hym schal be circumcidid bifore, and thanne he schal make lawfuli, and he schal be to gidere as a man borun of the lond; forsothe if ony man is not circumcidid, he schal not ete therof.
49 Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
The same lawe schal be to a man borun of the lond, and to a comelyng, that takith youre feith, which is a pilgrym anentis you.
50 Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
And alle the sones of Israel diden as the Lord comaundide to Moises and Aaron.
51 Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.
And in the same dai the Lord ladde out of `the lond of Egipt the sones of Israel, bi her cumpanies.

< Kutoka 12 >