< Kutoka 12 >
1 Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
Yahweh spoke to Moses and Aaron in the land of Egypt. He said,
2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
“For you, this month will be the start of months, the first month of the year to you.
3 Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
Tell the assembly of Israel, 'On the tenth day of this month they must each take a lamb or young goat for themselves, each family doing this, a lamb for each household.
4 Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
If the household is too small for a lamb, the man and his next door neighbor are to take lamb or young goat meat that will be enough for the number of the people. It should be enough for everyone to eat, so they must take enough meat to feed them all.
5 Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
Your lamb or young goat must be without blemish, a one-year-old male. You may take one of the sheep or goats.
6 Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
You must keep it until the fourteenth day of that month. Then the whole assembly of Israel must kill these animals at twilight.
7 Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
You must take some of the blood and put it on the two side doorposts and on the tops of the doorframes of the houses in which you will eat the meat.
8 Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
You must eat the meat that night, after first roasting it over a fire. Eat it with bread made without yeast, along with bitter herbs.
9 Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
Do not eat it raw or boiled in water. Instead, roast it over fire with its head, legs and inner parts.
10 Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
You must not let any of it be left over until morning. You must burn whatever is left over in the morning.
11 Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
This is how you must eat it: with your belt fastened, your shoes on your feet, and your staff in your hand. You must eat it hurriedly. It is Yahweh's Passover.
12 “Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
Yahweh says this: I will go through the land of Egypt in that night and attack all the firstborn of man and animal in the land of Egypt. I will bring punishment on all the gods of Egypt. I am Yahweh.
13 Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
The blood will be a sign on your houses for my coming to you. When I see the blood, I will pass over you when I attack the land of Egypt. This plague will not come on you and destroy you.
14 “Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
This day will become a memorial day for you, which you must observe as a festival for Yahweh. It will always be a law for you, throughout your people's generations, that you must observe this day.
15 Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
You will eat bread without yeast during seven days. On the first day you will remove the yeast from your houses. Whoever eats leavened bread from the first day until the seventh day, that person must be cut off from Israel.
16 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
On the first day there will be an assembly that is set apart to me, and on the seventh day there will be another such gathering. No work will be done on these days, except the cooking for everyone to eat. That must be the only work that may be done by you.
17 “Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
You must observe this Festival of Unleavened Bread because it is on this day that I will have brought your people, armed group by armed group, out of the land of Egypt. So you must observe this day throughout your people's generations. This will always be a law for you.
18 Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
You must eat unleavened bread from twilight of the fourteenth day in the first month of the year, until twilight of the twenty-first day of the month.
19 Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
During these seven days, no yeast must be found in your houses. Whoever eats bread made with yeast must be cut off from the community of Israel, whether that person is a foreigner or someone born in your land.
20 Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
You must eat nothing made with yeast. Wherever you live, you must eat bread made without yeast.'”
21 Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
Then Moses summoned all the elders of Israel and said to them, “Go and select lambs or kids that will be enough to feed your families and kill the Passover lamb.
22 Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
Then take a bunch of hyssop and dip it in the blood that will be in a basin. Apply the blood in the basin to the top of the doorframe and the two doorposts. None of you is to go out of the door of his house until the morning.
23 Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
For Yahweh will pass through to attack the Egyptians. When he sees the blood on the top of the doorframe and on the two doorposts, he will pass over your door and not permit the destroyer to come into your houses to attack you.
24 “Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
You must observe this event. This will always be a law for you and your descendants.
25 Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
When you enter the land that Yahweh will give you, just as he has promised to do, you must observe this act of worship.
26 Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
When your children ask you, 'What does this act of worship mean?'
27 Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
then you must say, 'It is the sacrifice of Yahweh's Passover, because Yahweh passed over the Israelites' houses in Egypt when he attacked the Egyptians. He set our households free.'” Then the people bowed down and worshiped Yahweh.
28 Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
The Israelites went and did exactly as Yahweh had commanded Moses and Aaron.
29 Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
It happened at midnight that Yahweh attacked all the firstborn in the land of Egypt, from the firstborn of Pharaoh, who sat on his throne, to the firstborn of the person in prison and all the firstborn of cattle.
30 Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
Pharaoh got up in the night—he, all his servants, and all the Egyptians. There was loud lamenting in Egypt, for there was not a house where there was not someone dead.
31 Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
Pharaoh summoned Moses and Aaron in the night and said, “Get up, get out from among my people, you and the Israelites. Go, worship Yahweh, as you have said you wanted to do.
32 Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
Take your flocks and your herds, as you have said, and go, and also bless me.”
33 Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
The Egyptians were in a great hurry to send them out of the land, for they said, “We will all die.”
34 Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
So the people took their dough without adding any yeast. Their kneading bowls were already tied up in their clothes and on their shoulders.
35 Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
Now the people of Israel did as Moses told them. They asked the Egyptians for articles of silver, articles of gold, and clothing.
36 Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
Yahweh made the Egyptians eager to please the Israelites. So the Egyptians gave them whatever they asked for. In this way, the Israelites plundered the Egyptians.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
The Israelites journeyed from Rameses to Succoth. They numbered about 600,000 men on foot, in addition to the women and children.
38 Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
A mixed multitude also went with them, together with flocks and herds, a very large number of livestock.
39 Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
They baked bread without yeast in the dough that they brought from Egypt. It was without yeast because they had been driven out of Egypt and could not delay to prepare food.
40 Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
The Israelites had lived in Egypt for 430 years.
41 Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
At the end of 430 years, on that very day, all of Yahweh's armed groups went out from the land of Egypt.
42 Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
This was a night to stay awake, for Yahweh to bring them out from the land of Egypt. This was Yahweh's night to be observed by all the Israelites throughout their people's generations.
43 Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
Yahweh said to Moses and Aaron, “Here is the rule for the Passover: No foreigner may share in eating it.
44 Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
However, every Israelite's slave, bought with money, may eat it after you have circumcised him.
45 lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
Foreigners and hired servants must not eat any of the food.
46 “Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
The food must be eaten in one house. You must not carry any of the meat out of the house, and you must not break any bone of it.
47 Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
All the community of Israel must observe the festival.
48 “Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
If a foreigner lives with you and wants to observe the Passover to Yahweh, all his male relatives must be circumcised. Then he may come and observe it. He will become like the people who were born in the land. However, no uncircumcised person may eat any of the food.
49 Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
This same law will apply to both the native born and to the foreigner who lives among you.”
50 Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
So all the Israelites did exactly as Yahweh had commanded Moses and Aaron.
51 Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.
It came about that very day that Yahweh brought Israel out of the land of Egypt by their armed groups.