< Kutoka 12 >

1 Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
Hina Gode da Idibidi soge ganodini, Mousese amola Elane elama amane sia: i,
2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
“Wali oubi da dilima oubi age ode huluane amoga ganumu.
3 Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
Isala: ili dunu gilisisu amoma agoane olelema, ‘Wali oubi amoga eso nabuane amoga diasu afae afae esalebe sosogo fi eda da sibi mano o goudi mano afae ilegema: ma.
4 Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
Be ea sosogo fi da fonobahadi amola ohe afae huluane manu hamedei ba: sea, defea, e amola ea dafulisu na: iyado sosogo fi da amo ohe fifili, dunu ilia idi amola ilia manu defele, gilisili manu.
5 Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
Sibi o goudi ilegema. Be gawali amo da noga: idafa, aiya amola nigima: amola wadela: i hame galu amo fawane ilegema.
6 Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
Amasea, eso 14 (ge), age oubiga, daeya, Isala: ili dunu huluane da amo ilegei ohe medole legema: mu.
7 Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
Isala: ili dunu da maga: me mogili lale, diasu amo ganodini ohe ilia da manu, amo diasu logo holei mimogoa gadodili, la: ididili amola la: ididili maga: mega ulasima: mu.
8 Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
Amo gasia, sibi o goudi ea hu amo gobele, mola: agoane amola agi (yisidi hame sali) gilisili moma.
9 Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
Hu da hame gobei (gahea) o hano ganodini egei mae moma. Be ohe mae dadega: le, dialuma, emo amola iga huluane gilisili gogo gobema.
10 Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
Hahabe doaga: sea, hu huluane da na dagoi ba: ma: mu. Be fonobahadi hame mae dialebe ba: sea, amo laluga gobele salima.
11 Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
Dilia amo hedolowane moma. Dilia gadili masa: ne defele, abula salawane, emo salasu salawane amola dagulu dilia lobo ganodini gaguiwane ouesaloma. Amo lolo nabe da Na Hina Godema nodoma: ne Baligisu (Gadodili Baligisu) Lolo Nabe.
12 “Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
Amo gasi ganodini Na da Idibidi soge huluane amo ganodini masunu. Na da dunu amola ohe fi magobo mano huluane fanelegemu. Amola Na da Idibidi ogogosu ‘gode’ huluanema se nabasu imunu. Na da Hina Godedafa!
13 Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
Maga: me amo dilia logo holei mimogodiga ulasi da dilia Isala: ili dunu dilia esalebe diasu ilegei gala. Na da maga: me ba: sea, Na da dili gadodili baligimu amola Na da Idibidi dunuma se nabasu iasia Na da dilima se hame imunu.
14 “Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
Dilia da amo Lolo Nasu amo da hadigi gilisisu hamoma: mu. Na, Hina Gode, da hou bagadedafa hamoi. Amo dilia mae gogolema: ne amo Baligisu Lolo Nasu ode huluane mae yolesili hamonanoma.”
15 Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
Hina Gode da amane sia: i, “Eso fesu ganodini dilia agi amo yisidi da ganodini sali, amo mae moma. Yisidi hame sali agi fawane moma. Eso agega, dilia yisidi huluane dilia diasu ganodini diala amo ha: digima. Amo eso fesuale ganodini nowa da yisidi sali agi nasea, e da Na fi amoga fadegai dagoi ba: mu.
16 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
Eso age amo ganodini dilia da nodone sia: ne gadomusa: gilisima. Amo eso fesuale amoga dilia mae hawa: hamoma. Be ha: i manu hahamomu da defea.
17 “Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
Amo gilisisu mae yolesili ode huluane amoga hamoma. Bai amo esoga, Na da dili Idibidi soge fisimusa: , gadili oule asi, amo dawa: ma.
18 Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
Eso 14 oubi age amo daeya asili eso 21 daeya, amo eso fesualega, dilia da agi yisidi sali amo mae moma.
19 Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
Amo eso fesualega, yisidi dilia diasu ganodini ba: mu da sema bagade. Bai nowa dunu amo Isala: ili o ga fi dunu da yisidi sali agi nasea, e da Na fi amoga fadegai dagoi ba: mu.”
20 Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
Mousese da Isala: ili ouligisu dunu huluane ema misa: ne sia: i. E da ilima amane sia: i, “Dilia huluane da sibi mano o goudi mano ilegele, amo medole legema. Dilia sosogo fi da Baligisu Lolo Nasu hamoma: ne,
22 Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
dilia ohe medole legei amo ea maga: me ofodo ganodini salima. Amasea, hisobe lubi amo maga: me ganodini gele, dilia diasu logo holei amo gadodili amola mimogodi la: didili amola eno la: didili ulasima. Amola dilia da diasu ganodini gagili sali agoane esaloma. Dunu huluane da daeya asili hahabe, diasu mae yolesili amo ganodini ouesaloma: mu.
23 Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
Hina Gode da Idibidi sogega magobo mano fanelegemusa: ahoasea, E da maga: me dilia logo holei gadodili amola mimogodi la: didili la: didili ulasi ba: sea, E da Gugunufinisisu A: igele ema dilia diasu ganodini dili medoma: ne mae golili sa: ima: ne sia: mu.
24 “Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
Dilia amola dilia mano da amo hamoma: ne sia: i eso huluane nabawane hamoma.
25 Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
Dilia da soge amo Hina Gode da dilima imunu ilegele sia: i, amoga golili dasea, dilia da Baligisu (Gadodili Baligisu) Lolo Nasu hamoma.
26 Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
Dilia mano da dilima, amane adole ba: sea, ‘Amo hou ea bai da adi baila: ?’
27 Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
Dilia bu adole ima, ‘Amo da Baligisu Lolo Nasu gobele salasu, Hina Godema nodomusa: nini hamosa. E da Idibidi soge ganodini, Isala: ili dunu diasu amo gadodili baligi dagoi. E da Idibidi dunu medole legei be E da nini gaga: i dagoi,’” Mousese da amane sia: i. Isala: ili dunu da muguni bugili, Hina Godema nodone sia: ne gadoi.
28 Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
Amalalu, ilia da asili, Hina Gode da Mousese amola Elane elama adoi defele hamoi dagoi.
29 Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
Gasimogoa, Hina Gode da magobo mano huluane Idibidi soge ganodini esalu, amo medole lelegei. Felou ea magobo mano (amo da hina bagade hamomu galu) amola se iasu diasu ganodini sali dunu ilia magobo mano huluane, E da medole lelegei. Amola ohe fi ilia magobo mano huluane da medole legei dagoi ba: i.
30 Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
Amo gasia, Felou, ea eagene ouligisu dunu amola Idibidi dunu huluane da didilisi dagoi ba: i. Idibidi soge huluane amo ganodini da didigia: su bagade nabi. Bai diasu huluanedafa afae mae fisili, amo ganodini da dunu bogoi dagoi ba: i.
31 Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
Amo gasia, Felou da Mousese amola Elane elama misa: ne sia: i. E elama amane sia: i, “Gadili masa! Ali amola Isala: ili fi masa! Na soge yolesili masa! Dilia adole ba: i defele, Hina Godema nodomusa: masa!
32 Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
Dilia sibi, goudi amola bulamagau lale, gadili masa! Amola Gode da na hahawane dogolegema: ne, Ema sia: ne gadoma.”
33 Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
Idibidi dunu da Isala: ili dunuma hedolowane masa: ne sia: i. Ilia amane sia: i, “Dilia ga hame ahoasea, ninia huluane da bogogia: i dagoi ba: mu.”
34 Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
Amaiba: le, Isala: ili dunu da yisidi hame sali hame gobei agi amo ilia gobele nasu ofodo ganodini sali, amo abulaga dedebole gisa asi.
35 Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
Isala: ili dunu da Mousese ea sia: defele Idibidi dunuma gouli, silifa amola abula edegei dagoi.
36 Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
Hina Gode da Idibidi dunu ilia hou afadeneiba: le, ilia da Isala: ili dunuma esega beda: i galu. Amaiba: le, ilia da Isala: ili dunuma ilia edegei liligi iasu. Amola Isala: ili dunu da Idibidi dunu ilia noga: i liligi huluane gaguli asi dagoi.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
Isala: ili dunu da La: misisi moilai bai bagade yolesili, emoga asili, Sagode moilaiga doaga: musa: asi. Dunu ilia idi da 600,000 agoane. Amola uda amola mano bagohame gadili asi, be ilia defei hame idi.
38 Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
Dunu eno bagohame, sibi, goudi amola bulamagau osea: idafa ilia da oule asi.
39 Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
Ilia da yisidi hame sali agi amo logoga gobei. Ilia da Idibidi soge amoga hedolowane sefasiba: le, ilia Idibidi soge ganodini ha: i manu logoga manusa: hahamomu amola yisidi ilia falaua ganodini salimu hamedei ba: i.
40 Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
Isala: ili dunu da Idibidi soge ganodini ode 430 esalu.
41 Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
Eso amoga ode 430 da gidigi ba: loba, Hina Gode Ea fi huluane da Idibidi yolesili gadili asi.
42 Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
Amo gasia, Hina Gode da mae golale, Ea fi dunu Idibidi soge amoga fadegale ga oule masa: ne sosodo aligi ba: i. Amo gasia, ode huluane ganodini Isala: ili dunu da Hina Godema nodone dawa: ma: ne, sosodo aligilalebe ligiagasa.
43 Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
Hina Gode da Mousese amola Elane elama amane sia: i, “Baligisu hamoma: ne sia: da amo: - Ga fi dunu da Baligisu Lolo hame manu.
44 Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
Be dilia da udigili bidi hame lasu hawa: hamosu dunu lasea, e da Baligisu manu da defea. Be hidadea ea gadofo damuma: mu.
45 lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
Sofe misi o bidi lamu hawa: hamosu dunu da hame manu.
46 “Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
Dilia Lolo Nasu ha: i manu amo huluanedafa da diasu afadafa fawane amo ganodini moma. Gadili mae gaguli masa. Amola, ohe gobei amo ea gasa mae fima.
47 Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
Isala: ili fi huluane da gilisisu hamone, amo lolo manu.
48 “Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
Be gadofo hame damui dunu da hame manu. Be ga fi dunu da dilia soge ganodini esalea, amola e da Hina Godema nodomusa: Baligisu Lolo manu hanai galea, dilia hidadea dunu huluane ea sosogo fi amo ganodini ilia gadofo damuma. Amasea, amo dunu da Isala: ili dunu lalelegei defele ba: ma. Amasea, e da Baligisu lolo manu da defea.
49 Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
Be Isala: ili dunudafa amola ga fi dunu dilima gilisi, amo huluane da defele Baligisu Lolo Nasu hamoma: ne sia: i nabawane hamoma: mu.
50 Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
Isala: ili dunu huluane da nabasu hou hamosu. Ilia da Hina Gode Ea Mousese amola Elane elama adoi defele hamosu.
51 Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.
Amo esoga Hina Gode da Isala: ili fi huluane Idibidi sogega fisili masa: ne, gadili oule asi.

< Kutoka 12 >