< Kutoka 11 >

1 Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Nitaleta pigo moja zaidi kwa Farao na katika nchi ya Misri. Baada ya hilo, atawaacha mwondoke hapa na atakapofanya hivyo, atawafukuza mtoke kabisa.
Yahweh disse a Moisés: “Eu trarei ainda mais uma praga sobre o Faraó e sobre o Egito; depois ele o deixará ir”. Quando ele te deixar ir, certamente te expulsará por completo”.
2 Waambie watu wote waume kwa wake wawaombe majirani zao vitu vya fedha na vya dhahabu.”
Fale agora aos ouvidos do povo, e deixe cada homem pedir ao seu próximo, e cada mulher do seu próximo, jóias de prata, e jóias de ouro”.
3 (Bwana akawafanya Wamisri wawe na moyo wa ukarimu kwa Waisraeli, naye Mose mwenyewe akaheshimiwa sana na maafisa wa Farao na watu wote katika nchi ya Misri.)
Yahweh deu ao povo um favor aos olhos dos egípcios. Além disso, o homem Moisés era muito grande na terra do Egito, aos olhos dos servos do Faraó, e aos olhos do povo.
4 Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.
Moisés disse: “Isto é o que diz Javé: 'Por volta da meia-noite irei para o meio do Egito,
5 Kila mwanaume kifungua mimba katika Misri atakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Farao, aketiye penye kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mtumwa wa kike, anayesaga nafaka kwa jiwe, pamoja na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.
e todos os primogênitos na terra do Egito morrerão, desde o primogênito do Faraó que se senta em seu trono, até o primogênito da criada que está atrás do moinho, e todos os primogênitos do gado.
6 Patakuwepo kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, kilio kibaya ambacho hakijakuwepo wala kamwe hakitakuwepo tena.
Haverá um grande grito em toda a terra do Egito, como não houve, nem haverá mais.
7 Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna hata mbwa atakayembwekea mwanadamu wala mnyama yeyote.’ Ndipo mtakapojua kuwa Bwana huweka tofauti kati ya Misri na Israeli.
Mas contra qualquer um dos filhos de Israel um cão não ladrará nem moverá sua língua, contra o homem ou animal, para que você saiba que Javé faz uma distinção entre os egípcios e Israel.
8 Maafisa hawa wako wote watanijia, wakisujudu mbele yangu, wakisema, ‘Ondoka, wewe pamoja na watu wako wote wanaokufuata!’ Baada ya haya nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa amewaka hasira, akamwacha Farao.
Todos esses seus servos virão até mim, e se curvarão diante de mim, dizendo: “Saia, com todas as pessoas que o seguirem;” e depois disso eu sairei”. Saiu do Faraó em fúria quente.
9 Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Farao atakataa kukusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka katika nchi ya Misri.”
Yahweh disse a Moisés: “O Faraó não lhe dará ouvidos, para que minhas maravilhas se multipliquem na terra do Egito”.
10 Mose na Aroni wakafanya maajabu haya yote mbele ya Farao, lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke katika nchi yake.
Moisés e Arão fizeram todas essas maravilhas diante do Faraó, mas Javé endureceu o coração do Faraó e não deixou os filhos de Israel saírem de sua terra.

< Kutoka 11 >