< Kutoka 11 >

1 Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Nitaleta pigo moja zaidi kwa Farao na katika nchi ya Misri. Baada ya hilo, atawaacha mwondoke hapa na atakapofanya hivyo, atawafukuza mtoke kabisa.
Then Yahweh said to Moses/me, “I will cause one more disaster to strike the king of Egypt and all his people [MTY]. After that, he will let you leave. In fact, he will expel you all.
2 Waambie watu wote waume kwa wake wawaombe majirani zao vitu vya fedha na vya dhahabu.”
So now speak to all the [Israeli] people. Tell them to ask all their [Egyptian] neighbors, both men and women, to give them some silver and gold jewelry.”
3 (Bwana akawafanya Wamisri wawe na moyo wa ukarimu kwa Waisraeli, naye Mose mwenyewe akaheshimiwa sana na maafisa wa Farao na watu wote katika nchi ya Misri.)
Yahweh made the Egyptians highly respect the Israeli people. In particular, the Egyptian officials and all [the rest of] the people considered Moses/me to be a very great man.
4 Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.
Then Moses/I [went to the king and] said, “This is what Yahweh says: ‘About midnight [tonight] I will go throughout Egypt,
5 Kila mwanaume kifungua mimba katika Misri atakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Farao, aketiye penye kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mtumwa wa kike, anayesaga nafaka kwa jiwe, pamoja na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.
and I will cause all the firstborn/oldest [sons] to die. That will include your oldest son, the oldest sons of the slave women who grind grain, [and the oldest sons of everyone else]. I will also kill the oldest males of the Egyptians’ livestock.
6 Patakuwepo kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, kilio kibaya ambacho hakijakuwepo wala kamwe hakitakuwepo tena.
When that happens, people all over Egypt will wail loudly. They have never wailed like that before, and they will never wail like that again.
7 Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna hata mbwa atakayembwekea mwanadamu wala mnyama yeyote.’ Ndipo mtakapojua kuwa Bwana huweka tofauti kati ya Misri na Israeli.
But among the Israeli people [it will be so quiet that] not even a dog will bark! Then you will know for sure that I, Yahweh, distinguish [how I act toward] the Egyptians and [how I act toward] the Israeli people.
8 Maafisa hawa wako wote watanijia, wakisujudu mbele yangu, wakisema, ‘Ondoka, wewe pamoja na watu wako wote wanaokufuata!’ Baada ya haya nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa amewaka hasira, akamwacha Farao.
Then all these officials of yours will come and bow down before me and will say, “Please get out [of Egypt], you and all the Israeli people!”’ After that, I will leave Egypt!” [After Moses/I said that], he/I very angrily left the king.
9 Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Farao atakataa kukusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka katika nchi ya Misri.”
Then Yahweh said to Moses/me, “The king will not pay any attention to what you say. The result will be that I will perform more plagues in the land of Egypt.”
10 Mose na Aroni wakafanya maajabu haya yote mbele ya Farao, lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke katika nchi yake.
Aaron and Moses/I performed all these miracles in front of the king, but Yahweh made the king stubborn, and he did not let the Israeli people leave his country.

< Kutoka 11 >