< Kutoka 10 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
Gospod je rekel Mojzesu: »Pojdi noter k faraonu, kajti zakrknil sem njegovo srce in srce njegovih služabnikov, da lahko ta svoja znamenja pokažem pred njim,
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
in da ti lahko poveš v ušesa svojih sinov in sinov svojih sinov, kakšne stvari sem storil v Egiptu in moja znamenja, ki sem jih storil med njimi, da boste lahko spoznali, kako [to], da sem jaz Gospod.«
3 Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Mojzes in Aron sta vstopila k faraonu ter mu rekla: »Tako govori Gospod, Bog Hebrejcev: ›Doklej boš odklanjal, da se ponižaš pred menoj? Pusti moje ljudstvo oditi, da mi bodo lahko služili.
4 Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
Ali pa, če odkloniš, da pustiš moje ljudstvo oditi, glej, bom jutri v tvojo pokrajino privedel leteče kobilice.
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
Pokrile bodo obličje zemlje, da nekdo ne bo mogel videti zemlje. Pojedle bodo preostanek tega, kar je ušlo, kar vam ostaja od toče in pojedle bodo vsako drevo, ki vam raste zunaj polja.
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
Napolnile bodo tvoje hiše in hiše vseh tvojih služabnikov in hiše vseh Egipčanov, kar niti tvoji očetje niti očetje tvojih očetov niso videli od dneva, ko so bili na zemlji, do današnjega dne.‹« In obrnil se je ter odšel ven od faraona.
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
Faraonovi služabniki so mu rekli: »Doklej nam bo ta človek zanka? Pusti ljudi oditi, da bodo lahko služili Gospodu, svojemu Bogu. Mar še ne veš, da je Egipt uničen?«
8 Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
Mojzes in Aron sta bila ponovno privedena k faraonu. Rekel jima je: »Pojdite, služite Gospodu, svojemu Bogu, toda kdo so tisti, ki bodo šli?«
9 Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
Mojzes je rekel: »Šli bomo s svojimi mladimi in s svojimi starimi, s svojimi sinovi in s svojimi hčerami in s svojimi tropi in s svojimi čredami bomo šli, kajti imeti moramo praznik Gospodu.«
10 Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
Rekel jima je: »Naj bo Gospod tako z vami, kakor bom jaz pustil oditi vam in vašim malčkom. Glejta na to, kajti zlo je pred vami.
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
Ne tako. Pojdite sedaj vi, ki ste možje in služite Gospodu, kajti to ste si želeli.« In izgnana sta bila izpred faraonove prisotnosti.
12 Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
Gospod je rekel Mojzesu: »Iztegni svojo roko nad egiptovsko deželo zaradi letečih kobilic, da bodo lahko prišle nad egiptovsko deželo in pojedle vsako zemeljsko zelišče, celó vse, kar je pustila toča.«
13 Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
Mojzes je iztegnil svojo palico nad egiptovsko deželo in Gospod je ves ta dan prinašal vzhodnik nad deželo in vso to noč, in ko je bilo jutro, je vzhodnik prinesel leteče kobilice.
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
Leteče kobilice so se dvignile nad vso egiptovsko deželo in počivale po vseh egiptovskih pokrajinah. Bile so zelo nadležne. Pred njimi ni bilo takšnih letečih kobilic kakor te niti takšnih ne bo za njimi.
15 Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
Kajti pokrile so obličje celotne zemlje, tako da je bila dežela temna. Pojedle so vsa zelišča dežele in vse sadje dreves, ki jih je pustila toča. Niti ena zelena stvar ni preostala na drevesih ali na poljskih zeliščih po vsej egiptovski deželi.
16 Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
Potem je faraon v naglici dal poklicati Mojzesa in Arona ter rekel: »Grešil sem zoper Gospoda, svojega Boga in zoper vaju.
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
Zdaj torej oprostita, prosim vaju, moj greh, samo še tokrat in rotita Gospoda, svojega Boga, da mi lahko odvzame samo to smrt.«
18 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
In odšel je ven od faraona in rotil Gospoda.
19 Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
Gospod je [veter] obrnil [v] mogočen močan zahodnik, ki je odnesel leteče kobilice in jih vrgel v Rdeče morje. Tam ni ostala niti ena leteča kobilica po vseh egiptovskih pokrajinah.
20 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
Toda Gospod je zakrknil faraonovo srce, tako da ta ni hotel pustiti Izraelovih otrok oditi.
21 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
Gospod je rekel Mojzesu: »Iztegni svojo roko proti nebu, da bo lahko tam tema nad egiptovsko deželo, celó tema, ki se jo bo lahko čutilo.«
22 Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
Mojzes je iztegnil svojo roko proti nebu in tri dni je bila gosta tema po vsej egiptovski deželi.
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
Drug drugega niso videli niti tri dni ni nihče vstal iz svojega kraja, toda vsi Izraelovi otroci so imeli v svojih prebivališčih svetlobo.
24 Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
Faraon je klical k Mojzesu ter rekel: »Pojdite, služite Gospodu. Samo vaši tropi in vaše črede naj ostanejo; naj gredo z vami tudi vaši malčki.«
25 Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
Mojzes je rekel: »Moraš nam dati tudi klavne daritve in žgalne daritve, da bomo lahko darovali Gospodu, svojemu Bogu.
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
Tudi naša živina bo šla z nami. Niti kopito ne bo ostalo zadaj, kajti od nje moramo vzeti, da služimo Gospodu, svojemu Bogu in ne vemo s čim moramo služiti Gospodu, dokler ne pridemo tja.«
27 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
Toda Gospod je zakrknil faraonovo srce in ta jim ni hotel pustiti oditi.
28 Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
Faraon mu je rekel: »Spravi se od mene, pazi se, da ne vidiš več mojega obraza, kajti na ta dan, [ko] zagledaš moj obraz, boš umrl.«
29 Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
Mojzes je rekel: »Dobro si govoril, tvojega obraza ne bom več ponovno videl.«

< Kutoka 10 >