< Kutoka 10 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
Et le Seigneur dit à Moïse: Entre auprès de Pharaon; car c’est moi qui ai endurci son cœur et celui de ses serviteurs, afin que je fasse sur lui ces signes de ma puissance,
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
Et que tu racontes aux oreilles de ton fils et de tes neveux, combien de fois j’ai brisé les Egyptiens et j’ai fait mes signes au milieu d’eux, et que vous sachiez que je suis le Seigneur.
3 Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Moïse et Aaron entrèrent donc auprès de Pharaon, et lui dirent: Voici ce que dit le Seigneur Dieu des Hébreux: Jusqu’à quand ne voudras-tu pas te soumettre à moi? Laisse aller mon peuple, afin qu’il me sacrifie.
4 Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
Que si tu résistes encore, et si tu ne veux pas le laisser aller, voilà que moi, je ferai venir demain des sauterelles dans tes confins;
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
Pour qu’elles couvrent la surface de la terre; en sorte qu’il n’en paraisse rien; mais que ce qui sera resté après la grêle, soit mangé; car elles rongeront tous les arbres qui poussent dans les champs.
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
Et elles rempliront tes maisons, et celles de tes serviteurs et de tous les Egyptiens; ni tes pères, ni tes aïeux n’en ont vu autant depuis qu’ils sont nés sur la terre, jusqu’au présent jour. Et il se retira, et il sortit d’avec Pharaon.
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
Mais les serviteurs de Pharaon lui dirent: Jusqu’à quand souffrirons-nous ce scandale? Laissez aller ces hommes, afin qu’ils sacrifient au Seigneur leur Dieu: ne voyez-vous pas que l’Egypte est perdue?
8 Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
Ils rappelèrent donc Moïse et Aaron auprès de Pharaon, qui leur dit: Allez, sacrifiez au Seigneur votre Dieu: qui sont ceux qui doivent y aller?
9 Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
Moïse répondit: Nous irons avec nos petits enfants et nos vieillards, avec nos fils et nos filles, avec nos brebis et notre gros bétail; car c’est une solennité du Seigneur notre Dieu.
10 Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
Et Pharaon repartit: Que le Seigneur soit avec vous de la même manière que moi, je vous laisserai aller, vous et vos petits enfants: qui doute que vous ne formiez de très mauvais desseins?
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
Non, il n’en sera pas ainsi; mais allez, vous autres hommes seulement, et sacrifiez au Seigneur; car c’est ce que vous-mêmes avez demandé. Et aussitôt ils furent renvoyés de la présence de Pharaon.
12 Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
Mais le Seigneur dit à Moïse: Etends ta main sur la terre d’Egypte vers les sauterelles, afin qu’elles montent sur la terre, et qu’elles dévorent toute l’herbe qui est restée après la grêle.
13 Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
Et Moïse étendit sa verge sur la terre d’Egypte, et le Seigneur fit venir un vent brûlant, qui souffla tout ce jour-là et toute la nuit; et, le matin venu, le vent brûlant fit lever les sauterelles;
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
Qui montèrent sur toute la terre d’Egypte; et elles s’arrêtèrent dans tous les confins des Egyptiens en nombre infini, telles qu’avant ce temps-là il n’y en avait pas eu, et qu’à l’avenir il ne doit pas y en avoir
15 Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
Ainsi, elles couvrirent la surface entière de la terre, ravageant tout. Toute l’herbe de la terre fut donc dévorée, et tout ce qui se trouva de fruits sur les arbres, fruits que la grêle avait laissés; de sorte qu’il ne resta absolument rien de vert sur les arbres ni dans les herbes de la terre, dans toute l’Egypte.
16 Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
C’est pourquoi Pharaon se hâtant appela Moïse et Aaron, et leur dit: J’ai péché contre le Seigneur votre Dieu, et contre vous.
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
Mais maintenant pardonnez-moi mon péché encore cette fois, et priez le Seigneur votre Dieu, afin qu’il retire de moi cette mort.
18 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
Moïse donc, sorti de la présence de Pharaon, pria le Seigneur,
19 Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
Qui fit souffler de l’occident un vent très violent, qui, ayant enlevé les sauterelles, les jeta dans la mer Rouge; il n’en demeura pas même une seule dans tous les confins de l’Egypte.
20 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
Mais le Seigneur endurcit le cœur de Pharaon, et il ne laissa pas aller les enfants d’Israël.
21 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
Alors le Seigneur dit à Moïse: Etends ta main vers le ciel, et qu’il y ait sur la terre d’Egypte des ténèbres si épaisses, qu’on puisse les toucher.
22 Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
Et Moïse étendit sa main vers le ciel, et il se forma des ténèbres horribles sur l’Egypte entière pendant trois jours.
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
Personne ne vit son frère, ni ne se remua du lieu où il était: mais la lumière était partout où habitaient les enfants d’Israël.
24 Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
Alors Pharaon appela Moïse et Aaron et leur dit: Allez, sacrifiez au Seigneur: que vos brebis seulement et votre gros bétail demeurent, et que vos petits enfants aillent avec vous.
25 Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
Moïse répondit: Tu nous donneras aussi des hosties et des holocaustes que nous puissions offrir au Seigneur notre Dieu.
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
Tous nos troupeaux iront avec nous, et il ne demeurera pas une corne de leurs pieds; c’est nécessaire pour le culte du Seigneur notre Dieu; d’autant plus que nous ignorons ce qui doit être immolé, jusqu’à ce que nous parvenions au lieu même.
27 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
Mais le Seigneur endurcit le cœur de Pharaon, et il ne voulut pas les laisser aller.
28 Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
Et Pharaon dit à Moïse: Retire-toi de moi, et garde-toi de voir désormais ma face: car en quelque jour que ce soit que tu paraisses de vaut moi, tu mourras.
29 Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
Moïse répondit: Il sera fait ainsi que tu las dit, je ne verrai plus ta face.