< Kutoka 10 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
and to say LORD to(wards) Moses to come (in): come to(wards) Pharaoh for I to honor: heavy [obj] heart his and [obj] heart servant/slave his because to set: make I sign: miraculous my these in/on/with entrails: among his
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
and because to recount in/on/with ear: hearing son: child your and son: child son: descendant/people your [obj] which to abuse in/on/with Egypt and [obj] sign: miraculous my which to set: make in/on/with them and to know for I LORD
3 Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
and to come (in): come Moses and Aaron to(wards) Pharaoh and to say to(wards) him thus to say LORD God [the] Hebrew till how to refuse to/for to afflict from face: before my to send: let go people my and to serve: minister me
4 Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
that if: except if: except refusing you(m. s.) to/for to send: let go [obj] people my look! I to come (in): bring tomorrow locust in/on/with border: area your
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
and to cover [obj] eye: before(the eyes) [the] land: country/planet and not be able to/for to see: see [obj] [the] land: country/planet and to eat [obj] remainder [the] survivor [the] to remain to/for you from [the] hail and to eat [obj] all [the] tree [the] to spring to/for you from [the] land: country
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
and to fill house: home your and house: home all servant/slave your and house: home all Egyptian which not to see: see father your and father father your from day to be they upon [the] land: planet till [the] day [the] this and to turn and to come out: come from from with Pharaoh
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
and to say servant/slave Pharaoh to(wards) him till how to be this to/for us to/for snare to send: let go [obj] [the] human and to serve: minister [obj] LORD God their before to know for to perish Egypt
8 Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
and to return: return [obj] Moses and [obj] Aaron to(wards) Pharaoh and to say to(wards) them to go: went to serve: minister [obj] LORD God your who? and who? [the] to go: went
9 Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
and to say Moses in/on/with youth our and in/on/with old our to go: went in/on/with son: child our and in/on/with daughter our in/on/with flock our and in/on/with cattle our to go: went for feast LORD to/for us
10 Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
and to say to(wards) them to be so LORD with you like/as as which to send: let go [obj] you and [obj] child your to see: behold! for distress: evil before face: before your
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
not so to go: went please [the] great man and to serve: minister [obj] LORD for [obj] her you(m. p.) to seek and to drive out: drive out [obj] them from with face Pharaoh
12 Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
and to say LORD to(wards) Moses to stretch hand your upon land: country/planet Egypt in/on/with locust and to ascend: rise upon land: country/planet Egypt and to eat [obj] all vegetation [the] land: country/planet [obj] all which to remain [the] hail
13 Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
and to stretch Moses [obj] tribe: rod his upon land: country/planet Egypt and LORD to lead spirit: breath east in/on/with land: country/planet all [the] day [the] he/she/it and all [the] night [the] morning to be and spirit: breath [the] east to lift: bear [obj] [the] locust
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
and to ascend: rise [the] locust upon all land: country/planet Egypt and to rest in/on/with all border: area Egypt heavy much to/for face: before his not to be so locust like him and after him not to be so
15 Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
and to cover [obj] eye: before(the eyes) all [the] land: country/planet and to darken [the] land: country/planet and to eat [obj] all vegetation [the] land: country/planet and [obj] all fruit [the] tree which to remain [the] hail and not to remain all green in/on/with tree and in/on/with vegetation [the] land: country in/on/with all land: country/planet Egypt
16 Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
and to hasten Pharaoh to/for to call: call to to/for Moses and to/for Aaron and to say to sin to/for LORD God your and to/for you
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
and now to lift: forgive please sin my surely [the] beat and to pray to/for LORD God your and to turn aside: remove from upon me except [obj] [the] death [the] this
18 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
and to come out: come from from with Pharaoh and to pray to(wards) LORD
19 Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
and to overturn LORD spirit: breath sea: west strong much and to lift: raise [obj] [the] locust and to blow him sea [to] Red (Sea) not to remain locust one in/on/with all border: area Egypt
20 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
and to strengthen: strengthen LORD [obj] heart Pharaoh and not to send: let go [obj] son: descendant/people Israel
21 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
and to say LORD to(wards) Moses to stretch hand your upon [the] heaven and to be darkness upon land: country/planet Egypt and to feel darkness
22 Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
and to stretch Moses [obj] hand his upon [the] heaven and to be darkness darkness in/on/with all land: country/planet Egypt three day
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
not to see: see man: anyone [obj] brother: compatriot his and not to arise: rise man: anyone from underneath: stand him three day and to/for all son: descendant/people Israel to be light in/on/with seat their
24 Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
and to call: call to Pharaoh to(wards) Moses and to say to go: went to serve: minister [obj] LORD except flock your and cattle your to set also child your to go: went with you
25 Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
and to say Moses also you(m. s.) to give: allow in/on/with hand: power our sacrifice and burnt offering and to make: offer to/for LORD God our
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
and also livestock our to go: went with us not to remain hoof for from him to take: take to/for to serve: minister [obj] LORD God our and we not to know what? to serve: minister [obj] LORD till to come (in): come we there [to]
27 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
and to strengthen: strengthen LORD [obj] heart Pharaoh and not be willing to/for to send: let go them
28 Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
and to say to/for him Pharaoh to go: went from upon me to keep: careful to/for you to(wards) to add: again to see: see face my for in/on/with day to see: see you face my to die
29 Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
and to say Moses right to speak: speak not to add: again still to see: see face your

< Kutoka 10 >