< Kutoka 10 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
Og Herren sagde til Mose: Gak ind til Farao; thi jeg har forhærdet hans Hjerte og hans Tjeneres Hjerte for at gøre disse mine Tegn iblandt dem,
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
og for at du skal forkynde det for dine Børns og dine Børnebørns Øren, hvad jeg har udrettet i Ægypten, og mine Tegn, som jeg har sat iblandt dem; og I skulle fornemme, at jeg er Herren.
3 Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Saa gik Mose og Aron ind til Farao og sagde til ham: Saa siger Herren, Hebræernes Gud: Hvor længe vægrer du dig ved at ydmyge dig for mit Ansigt? lad mit Folk fare, at de maa tjene mig.
4 Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
Thi dersom du vægrer dig ved at lade mit Folk fare, se, da vil jeg i Morgen lade Græshopper komme i dit Landemærke.
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
Og de skulle skjule Synet af Jorden, at man ikke skal kunne se Jorden, og de skulle opæde det øvrige, som er reddet, og hvad der er blevet eder tilovers fra Hagelen, og de skulle æde hvert Træ, som vokser op hos eder af Marken.
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
Og dine Huse skulle fyldes og alle dine Tjeneres Huse og alle Ægypternes Huse, hvilket hverken dine Fædre eller dine Forfædre have set, fra den Tid de bleve til paa Jorden indtil denne Dag; saa vendte han sig og gik ud fra Farao.
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
Da sagde Faraos Tjenere til ham: Hvor længe skal denne være os til en Snare? lad de Mænd fare, at de maa tjene Herren deres Gud; mon du endnu ikke ved, at Ægypten er ødelagt?
8 Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
Og Mose og Aron bleve hentede tilbage til Farao, og han sagde til dem: Gaar, tjener Herren, eders Gud; hvilke ere de, som gaa bort?
9 Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
Og Mose sagde: Vi ville gaa med vore unge og vore gamle, med vore Sønner og vore Døtre, med vore Faar og med vore Øksne ville vi gaa; thi det er os Herrens Højtid.
10 Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
Da sagde han til dem: Saa vist være Herren med eder, som jeg vil lade eder og eders smaa Børn fare, ser der, at I have ondt i Sinde.
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
Ikke saa! I Mænd, farer nu hen og tjener Herren, thi det have I begæret; og man drev dem ud fra Faraos Ansigt.
12 Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
Da sagde Herren til Mose: Ræk din Haand ud over Ægyptens Land efter Græshopper, og de skulle komme op over Ægyptens Land og æde alle Urter i Landet, ja alt det, som Hagelen lod blive tilovers.
13 Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
Saa rakte Mose sin Stav over Ægyptens Land, og Herren lod komme Østenvejr i Landet den samme hele Dag og hele Nat; det skete om Morgenen, at Østenvejret bragte Græshopperne op.
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
Og der kom Græshopper op over hele Ægyptens Land og lode sig ned i hele Ægyptens Landemærke; de vare i svær Mængde; før dem havde der ikke været Græshopper saaledes, og efter dem skulde der ikke blive saaledes;
15 Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
thi de skjulte Synet af hele Jorden, og Jorden blev formørket, og de aade alle Urter i Landet og al Frugt paa Træerne, som Hagelen lod blive tilovers; og der blev intet grønt tilovers paa Træer eller paa Urter i Marken i hele Ægyptens Land.
16 Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
Da skyndte Farao sig at kalde ad Mose og Aron, og han sagde: Jeg har syndet imod Herren eders Gud og imod eder.
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
Og kære, forlad mig nu min Synd aleneste denne Gang, og beder til Herren eders Gud, at han dog vil borttage denne Død fra mig.
18 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
Og han gik ud fra Farao, og han bad til Herren.
19 Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
Og Herren vendte Vejret om til en saare stærk Vestenvind, som førte Græshopperne bort og kastede dem i det røde Hav; der blev ikke een Græshoppe tilovers i hele Ægyptens Landemærke.
20 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
Men Herren forhærdede Faraos Hjerte, og han lod ikke Israels Børn fare.
21 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
Og Herren sagde til Mose: Ræk din Haand op mod Himmelen, at der bliver Mørke over Ægyptens Land, at man kan føle paa Mørket.
22 Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
Og Mose rakte sin Haand op mod Himmelen; da blev der tykt Mørke i hele Ægyptens Land i tre Dage.
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
Ikke een saa den anden, og ingen stod op fra sit Sted i tre Dage; men hos alle Israels Børn var det lyst i deres Boliger.
24 Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
Da kaldte Farao ad Mose og sagde: Gaar, tjener Herren, kun skulle I lade eders Faar og Øksne blive; ogsaa eders smaa Børn maa fare med eder.
25 Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
Og Mose sagde: Du skal og medgive os Slagtoffere og Brændoffere, at vi kunne ofre til Herren, vor Gud.
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
Og endogsaa vort Fæ skal gaa med os, der skal ikke en Klov blive tilbage; thi vi skulle tage deraf til at tjene Herren, vor Gud; thi vi vide ikke, hvormed vi skulle tjene Herren, førend vi komme derhen.
27 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
Men Herren forhærdede Faraos Hjerte, og han vilde ikke lade dem fare.
28 Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
Og Farao sagde til ham: Gak fra mig, vogt dig, at du ikke mere ser mit Ansigt; thi paa hvilken Dag du ser mit Ansigt, skal du dø.
29 Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
Og Mose sagde: Du talede ret; jeg vil herefter ikke mere se dit Ansigt.

< Kutoka 10 >