< Esta 9 >
1 Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, yaani mwezi wa Adari, amri iliyoagizwa na mfalme ilikuwa itekelezwe. Siku hii adui wa Wayahudi walikuwa wametumaini kuwashinda, lakini sasa mambo yaliwageukia na Wayahudi wakawashinda wale waliokuwa wanawachukia.
And in the twelfth month—it [is] the month of Adar—on the thirteenth day of it, in which the word of the king, even his law, has come to be done, in the day that the enemies of the Jews had hoped to rule over them, and it is turned that the Jews rule over those hating them—
2 Wayahudi walikusanyika katika miji yao, katika majimbo ya Mfalme Ahasuero kuwashambulia wale waliokuwa wanatafuta kuwaangamiza. Hakuna yeyote aliyeweza kushindana nao, kwa sababu watu wa mataifa mengine yote waliwaogopa.
the Jews have been assembled in their cities, in all provinces of King Ahasuerus, to put forth a hand on those seeking their evil, and no man has stood in their presence, for their fear has fallen on all the peoples.
3 Nao wakuu wote wa majimbo, majemadari, watawala na maafisa wa mfalme wakawasaidia Wayahudi, kwa sababu walimhofu Mordekai.
And all heads of the provinces, and the lieutenants, and the governors, and those doing the work that the king has, are lifting up the Jews, for a fear of Mordecai has fallen on them;
4 Mordekai alikuwa mtu mashuhuri katika jumba la mfalme; sifa zake zilienea katika majimbo yote naye alipata uwezo zaidi na zaidi.
for great [is] Mordecai in the house of the king, and his fame is going into all the provinces, for the man Mordecai is going on and becoming great.
5 Wayahudi waliwaangusha adui zao wote kwa upanga wakiwaua na kuwaangamiza, nao walifanya kile walichotaka kwa wale waliowachukia.
And the Jews strike among all their enemies—a striking of the sword, and slaughter, and destruction—and do with those hating them according to their pleasure,
6 Katika ngome ya Shushani Wayahudi waliua na kuangamiza wanaume 500.
and in Shushan the palace the Jews have slain and destroyed five hundred men;
7 Pia waliwaua Parshendatha, Dalfoni, Aspatha,
and Parshandatha, and Dalphon, and Aspatha,
8 Poratha, Adalia, Ardatha,
and Poratha, and Adalia, and Aridatha,
9 Parmashta, Arisai, Aridai na Waizatha,
and Parmashta, and Arisai, and Aridai, and Vajezatha,
10 wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchukua nyara.
ten sons of Haman son of Hammedatha, adversary of the Jews, they have slain, and on the prey they have not put forth their hand.
11 Mfalme aliarifiwa siku iyo hiyo hesabu ya waliouawa katika ngome ya Shushani.
On that day has come the number of the slain in Shushan the palace before the king,
12 Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wamewaua wanaume 500 na wana kumi wa Hamani ndani ya ngome ya Shushani. Wamefanyaje katika majimbo mengine ya mfalme yaliyobaki? Je, sasa haja yako ni nini? Nayo pia utapewa. Nalo ombi lako ni nini? Nalo utafanyiwa.”
and the king says to Esther the queen, “In Shushan the palace the Jews have slain and destroyed five hundred men, and the ten sons of Haman; in the rest of the provinces of the king what have they done? And what [is] your petition? And it is given to you; and what your request again? And it is done.”
13 Esta akajibu, “Ikimpendeza mfalme, uwape ruhusa Wayahudi walioko Shushani warudie amri ya leo kesho pia, na wana wa Hamani kumi wanyongwe mahali pa kunyongea watu.”
And Esther says, “If [it is] good to the king, let it also be given tomorrow, to the Jews who [are] in Shushan, to do according to the law of today; and the ten sons of Haman they hang on the tree.”
14 Basi mfalme akaamuru kwamba hili litendeke. Amri ilitolewa huko Shushani, nao wakawanyonga wana kumi wa Hamani.
And the king commands [for it] to be done so; and a law is given in Shushan, and they have hanged the ten sons of Haman.
15 Wayahudi huko Shushani wakakusanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, nao wakawaua wanaume 300 huko Shushani, lakini hawakuchukua nyara zao.
And the Jews who [are] in Shushan are also assembled on the fourteenth day of the month of Adar, and they slay three hundred men in Shushan, and they have not put forth their hand on the prey.
16 Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao.
And the rest of the Jews, who [are] in the provinces of the king, have been assembled, even to stand for their life, and to rest from their enemies, and to slay seventy-five thousand among those hating them, and they have not put forth their hand on the prey;
17 Hili lilitendeka siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari na siku ya kumi na nne walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
on the thirteenth day of the month of Adar, even to rest on the fourteenth of it, and to make it a day of banquet and of joy.
18 Wayahudi huko Shushani, hata hivyo, walikuwa wamekusanyika siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne, pia siku ya kumi na tano walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
And the Jews who [are] in Shushan have been assembled, on the thirteenth day of it, and on the fourteenth of it, even to rest on the fifteenth of it, and to make it a day of banquet and of joy.
19 Ndiyo sababu Wayahudi wanaokaa vijijini na katika miji midogo huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu, siku ambayo wao hupeana zawadi mmoja kwa mwingine.
Therefore the Jews of the open places, who are dwelling in cities of the open places, are making the fourteenth day of the month of Adar—joy and banquet, and a good day, and of sending portions to one another.
20 Mordekai aliandika matukio haya, naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote walioko katika majimbo ya Mfalme Ahasuero, majimbo yaliyo mbali na karibu,
And Mordecai writes these things, and sends letters to all the Jews who [are] in all provinces of King Ahasuerus, who are near and who are far off,
21 akiwataka kila mwaka washerehekee siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ya mwezi wa Adari
to establish on them, to be keeping the fourteenth day of the month of Adar, and the fifteenth day of it, in every year and year,
22 kama wakati ambao Wayahudi walipata nafuu kutoka kwa adui zao na kama mwezi ambao huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha na kuomboleza kwao kuwa siku ya kusherehekea. Aliwaandikia kushika siku hizo kama siku za karamu na za furaha na kupeana zawadi za vyakula wao kwa wao na zawadi kwa maskini.
as days on which the Jews have rested from their enemies, and the month that has been turned to them from sorrow to joy, and from mourning to a good day, to make them days of banquet and of joy, and of sending portions to one another, and gifts to the needy.
23 Hivyo Wayahudi walikubali kuendeleza sherehe walizokuwa wamezianza, wakifanya lile Mordekai alilokuwa amewaandikia.
And the Jews have received that which they had begun to do, and that which Mordecai has written to them,
24 Kwa maana Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi, adui wa Wayahudi wote, alikuwa amepanga hila dhidi ya Wayahudi ili kuwaangamiza, na alikuwa amepiga puri (yaani kura) kwa ajili ya maangamizi na uharibifu wao.
because Haman son of Hammedatha the Agagite, adversary of all the Jews, had devised concerning the Jews to destroy them, and had caused to fall Pur—that [is] the lot—to crush them and to destroy them;
25 Lakini wakati shauri hilo baya lilipoarifiwa kwa mfalme, alitoa amri iliyoandikwa kwamba mipango mibaya ambayo Hamani ameipanga dhidi ya Wayahudi inapasa imrudie juu ya kichwa chake mwenyewe, na kwamba yeye na wanawe waangikwe mahali pa kunyongea watu.
and in her coming in before the king, he commanded with the letter, “Let his evil scheme that he devised against the Jews return on his own head,” and they have hanged him and his sons on the tree,
26 (Kwa hiyo siku hizi ziliitwa Purimu, kutokana na neno puri.) Kwa sababu ya kila kitu kilichoandikwa kwenye barua hii na kwa sababu ya yale waliyoyaona na yale yaliyowatokea,
therefore they have called these days Purim—by the name of the lot—therefore, because of all the words of this letter, and what they have seen concerning this, and what has come to them,
27 Wayahudi wakachukua na kuifanya desturi kwamba wao na wazao wao na wote ambao walijiunga nao wangefanya bila kuacha kushika siku hizi mbili kila mwaka, kwa njia ilivyoelekezwa na kwa wakati wake.
the Jews have established and received on them, and on their seed, and on all those joined to them, and it does not pass away, to be keeping these two days according to their writing, and according to their season, in every year and year;
28 Siku hizi zinapasa zikumbukwe na kuadhimishwa katika kila kizazi, kila jamaa na katika kila jimbo na kila jiji. Nazo siku hizi za Purimu kamwe zisikome kusherehekewa na Wayahudi, wala kumbukumbu zake zisipotee miongoni mwa wazao wake.
and these days are remembered and kept in every generation and generation, family and family, province and province, and city and city, and these days of Purim do not pass away from the midst of the Jews, and their memorial is not ended from their seed.
29 Basi Malkia Esta binti Abihaili, pamoja na Mordekai, Myahudi, waliandika kwa mamlaka yote kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
And Esther the queen, daughter of Abihail, writes, and Mordecai the Jew, with all might, to establish this second letter of Purim,
30 Naye Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo 127 ya ufalme wa Ahasuero, barua zenye maneno ya amani na matumaini,
and he sends letters to all the Jews, to the one hundred twenty-seven provinces of the kingdom of Ahasuerus—words of peace and truth—
31 ili kuimarisha siku hizi za Purimu katika majira yake yaliyowekwa, kama Mordekai, Myahudi na Malkia Esta walivyowaamuru, na walivyojiimarisha wenyewe na wazao wao kuhusu nyakati za kufunga na kuomboleza.
to establish these days of Purim, in their seasons, as Mordecai the Jew has established on them, and Esther the queen, and as they had established on themselves, and on their seed—matters of the fastings, and of their cry.
32 Amri ya Esta ilithibitisha taratibu hizi kuhusu Purimu, nayo ikaandikwa katika kumbukumbu.
And a saying of Esther has established these matters of Purim, and it is written in the Scroll.