< Esta 9 >

1 Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, yaani mwezi wa Adari, amri iliyoagizwa na mfalme ilikuwa itekelezwe. Siku hii adui wa Wayahudi walikuwa wametumaini kuwashinda, lakini sasa mambo yaliwageukia na Wayahudi wakawashinda wale waliokuwa wanawachukia.
And in the twelfth month, that is, the month Adar, on the thirteenth day thereof, when the king's command with his law drew near to he put into execution, on the day that the enemies of the Jews had hoped to have power over them, which had been changed nevertheless, so that the Jews had power over those that hated them,
2 Wayahudi walikusanyika katika miji yao, katika majimbo ya Mfalme Ahasuero kuwashambulia wale waliokuwa wanatafuta kuwaangamiza. Hakuna yeyote aliyeweza kushindana nao, kwa sababu watu wa mataifa mengine yote waliwaogopa.
The Jews assembled together in their cities, throughout all the provinces of king Achashverosh, to stretch out their hand against those that had sought their injury: and no man could keep standing before them; for the dread of them had fallen upon all the nations.
3 Nao wakuu wote wa majimbo, majemadari, watawala na maafisa wa mfalme wakawasaidia Wayahudi, kwa sababu walimhofu Mordekai.
And all the rulers of the provinces, and the lieutenants, and the governors, and the superintendents of the affairs of the king, elevated the Jews; because the dread of Mordecai had fallen upon them.
4 Mordekai alikuwa mtu mashuhuri katika jumba la mfalme; sifa zake zilienea katika majimbo yote naye alipata uwezo zaidi na zaidi.
For Mordecai was great in the king's house, and his fame went throughout all the provinces; for the man Mordecai became greater and greater.
5 Wayahudi waliwaangusha adui zao wote kwa upanga wakiwaua na kuwaangamiza, nao walifanya kile walichotaka kwa wale waliowachukia.
And the Jews smote all their enemies with the stroke of the sword, and slaughter, and extermination; and they acted with those that hated them according to their pleasure.
6 Katika ngome ya Shushani Wayahudi waliua na kuangamiza wanaume 500.
And in Shushan the capital the Jews slew and exterminated five hundred men.
7 Pia waliwaua Parshendatha, Dalfoni, Aspatha,
And Parshandatha, and Dalphon, and Aspatha,
8 Poratha, Adalia, Ardatha,
And Poratha, and Adalya, and Aridatha,
9 Parmashta, Arisai, Aridai na Waizatha,
And Parmashtha, and Arissai, and Aridai, and Vayzatha,
10 wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchukua nyara.
The ten sons of Haman the son of Hammedatha, the adversary of the Jews, did they slay; but to the spoil did they not stretch forth their hand.
11 Mfalme aliarifiwa siku iyo hiyo hesabu ya waliouawa katika ngome ya Shushani.
On that same day came the number of those that were slain in Shushan the capital before the king.
12 Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wamewaua wanaume 500 na wana kumi wa Hamani ndani ya ngome ya Shushani. Wamefanyaje katika majimbo mengine ya mfalme yaliyobaki? Je, sasa haja yako ni nini? Nayo pia utapewa. Nalo ombi lako ni nini? Nalo utafanyiwa.”
Then said the king unto Esther the queen, In Shushan the capital have the Jews slain and exterminated five hundred men, and the ten sons of Haman: what have they done in the rest of the king's provinces? Now what is thy petition? and it shall be granted thee: and what is thy request farther? and it shall be done.
13 Esta akajibu, “Ikimpendeza mfalme, uwape ruhusa Wayahudi walioko Shushani warudie amri ya leo kesho pia, na wana wa Hamani kumi wanyongwe mahali pa kunyongea watu.”
Then said Esther, If it please the king, let it tomorrow also be granted to the Jews who are in Shushan to do according to the law of this day, and let the ten sons of Haman be hanged on the gallows.
14 Basi mfalme akaamuru kwamba hili litendeke. Amri ilitolewa huko Shushani, nao wakawanyonga wana kumi wa Hamani.
And the king ordered that it should be done so; and the law was given out at Shushan; and the ten sons of Haman were hanged.
15 Wayahudi huko Shushani wakakusanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, nao wakawaua wanaume 300 huko Shushani, lakini hawakuchukua nyara zao.
And the Jews that were in Shushan assembled together also on the fourteenth day of the month Adar, and slew at Shushan three hundred men; but to the spoil they did not stretch forth their hand.
16 Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao.
And the remaining Jews that were in the king's provinces assembled together, and stood forward for their life, and procured rest from their enemies, and slew of those that hated them seventy and five thousand; but to the spoil did they not stretch forth their hand,
17 Hili lilitendeka siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari na siku ya kumi na nne walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
On the thirteenth day of the month Adar, and they rested on the fourteenth day thereof, and made it a day of entertainment and joy.
18 Wayahudi huko Shushani, hata hivyo, walikuwa wamekusanyika siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne, pia siku ya kumi na tano walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
But the Jews that were at Shushan assembled together on the thirteenth day thereof, and on the fourteenth thereof, and rested on the fifteenth thereof, and made it a day of entertainment and joy.
19 Ndiyo sababu Wayahudi wanaokaa vijijini na katika miji midogo huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu, siku ambayo wao hupeana zawadi mmoja kwa mwingine.
Therefore do the Jews of the villages, that dwell in the unwalled towns, make the fourteenth day of the month Adar as one of joy and entertainment, and a feast-day, and of sending portions one to another.
20 Mordekai aliandika matukio haya, naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote walioko katika majimbo ya Mfalme Ahasuero, majimbo yaliyo mbali na karibu,
And Mordecai wrote down these events; and he sent letters unto all the Jews that were in all the provinces of king Achashverosh, those nigh and those far away,
21 akiwataka kila mwaka washerehekee siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ya mwezi wa Adari
To take it on themselves as a duty, that they should celebrate the fourteenth day of the month Adar, and the fifteenth day of the same in each and every year,
22 kama wakati ambao Wayahudi walipata nafuu kutoka kwa adui zao na kama mwezi ambao huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha na kuomboleza kwao kuwa siku ya kusherehekea. Aliwaandikia kushika siku hizo kama siku za karamu na za furaha na kupeana zawadi za vyakula wao kwa wao na zawadi kwa maskini.
Like those days whereon the Jews had rest from their enemies, and the month which was changed unto them from sorrow to joy, and from mourning into a feast-day: to make them days of entertainment and joy, and of sending portions one to the other, and gifts to the needy.
23 Hivyo Wayahudi walikubali kuendeleza sherehe walizokuwa wamezianza, wakifanya lile Mordekai alilokuwa amewaandikia.
And the Jews took upon themselves that which they had begun already to do, and that which Mordecai had written unto them.
24 Kwa maana Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi, adui wa Wayahudi wote, alikuwa amepanga hila dhidi ya Wayahudi ili kuwaangamiza, na alikuwa amepiga puri (yaani kura) kwa ajili ya maangamizi na uharibifu wao.
Because Haman the son of Hammedatha, the Agagite, the adversary of all the Jews, had devised against the Jews to exterminate them, and had cast the Pur, that is, the lot, to destroy them, and to exterminate them.
25 Lakini wakati shauri hilo baya lilipoarifiwa kwa mfalme, alitoa amri iliyoandikwa kwamba mipango mibaya ambayo Hamani ameipanga dhidi ya Wayahudi inapasa imrudie juu ya kichwa chake mwenyewe, na kwamba yeye na wanawe waangikwe mahali pa kunyongea watu.
But when [Esther] came before the king, he ordered by that letter that his wicked device, which he had devised against the Jews, should return upon his own head: and they hanged him and his sons on the gallows.
26 (Kwa hiyo siku hizi ziliitwa Purimu, kutokana na neno puri.) Kwa sababu ya kila kitu kilichoandikwa kwenye barua hii na kwa sababu ya yale waliyoyaona na yale yaliyowatokea,
Therefore did they call these days Purim, after the name of Pur: therefore, because of all the words of this letter, both for that which they had experienced thereby, and for that which had occurred unto them,
27 Wayahudi wakachukua na kuifanya desturi kwamba wao na wazao wao na wote ambao walijiunga nao wangefanya bila kuacha kushika siku hizi mbili kila mwaka, kwa njia ilivyoelekezwa na kwa wakati wake.
The Jews confirmed it as a duty, and took upon themselves, and upon their seed, and upon all such as join themselves unto them, so that no one should fail therein, that they would celebrate these two days according to their prescription, and at their appointed time, in each and every year.
28 Siku hizi zinapasa zikumbukwe na kuadhimishwa katika kila kizazi, kila jamaa na katika kila jimbo na kila jiji. Nazo siku hizi za Purimu kamwe zisikome kusherehekewa na Wayahudi, wala kumbukumbu zake zisipotee miongoni mwa wazao wake.
And these days are remembered and celebrated throughout each and every generation, every family, every province, and every city; and these days of Purim will not pass away from the midst of the Jews, nor will their memorial cease from their seed.
29 Basi Malkia Esta binti Abihaili, pamoja na Mordekai, Myahudi, waliandika kwa mamlaka yote kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
Then wrote Esther the queen, the daughter of Abichayil, with Mordecai the Jew, with all due strength, to confirm this letter of Purim the second time.
30 Naye Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo 127 ya ufalme wa Ahasuero, barua zenye maneno ya amani na matumaini,
And he sent letters unto all the Jews, to the hundred and twenty-seven provinces of the kingdom of Achashverosh, word's of peace and truth,
31 ili kuimarisha siku hizi za Purimu katika majira yake yaliyowekwa, kama Mordekai, Myahudi na Malkia Esta walivyowaamuru, na walivyojiimarisha wenyewe na wazao wao kuhusu nyakati za kufunga na kuomboleza.
To confirm these days of Purim in their times, just as Mordecai the Jew and Esther the queen had enjoined on them, and as they had confirmed for themselves and for their seed, the matters of the fastings and their prayers.
32 Amri ya Esta ilithibitisha taratibu hizi kuhusu Purimu, nayo ikaandikwa katika kumbukumbu.
And the order of Esther confirmed these matters of Purim; and it was written in the book.

< Esta 9 >