< Esta 9 >

1 Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, yaani mwezi wa Adari, amri iliyoagizwa na mfalme ilikuwa itekelezwe. Siku hii adui wa Wayahudi walikuwa wametumaini kuwashinda, lakini sasa mambo yaliwageukia na Wayahudi wakawashinda wale waliokuwa wanawachukia.
Potom dvanáctého měsíce, (jenž jest měsíc Adar), třináctého dne téhož měsíce, když přišel čas poručení královského a výpovědi jeho, aby se vyplnila, v ten den, v kterýž se nadáli nepřátelé Židovští, že budou panovati nad nimi, stalo se na odpor, že panovali Židé nad těmi, kteříž je v nenávisti měli.
2 Wayahudi walikusanyika katika miji yao, katika majimbo ya Mfalme Ahasuero kuwashambulia wale waliokuwa wanatafuta kuwaangamiza. Hakuna yeyote aliyeweza kushindana nao, kwa sababu watu wa mataifa mengine yote waliwaogopa.
Nebo se byli shromáždili Židé v městech svých, po všech krajinách krále Asvera, aby vztáhli ruku na ty, kteříž hledali jejich zlého. A žádný před nimi neostál, nebo připadl strach jejich na všecky národy.
3 Nao wakuu wote wa majimbo, majemadari, watawala na maafisa wa mfalme wakawasaidia Wayahudi, kwa sababu walimhofu Mordekai.
A všickni hejtmané krajin, i knížata a vývodové, i správcové díla královského v poctivosti měli Židy; nebo strach Mardocheův na ně připadl.
4 Mordekai alikuwa mtu mashuhuri katika jumba la mfalme; sifa zake zilienea katika majimbo yote naye alipata uwezo zaidi na zaidi.
Byl zajisté Mardocheus veliký v domě královském, a rozcházela se pověst o něm po všech krajinách; nebo muž ten Mardocheus vždy více rostl.
5 Wayahudi waliwaangusha adui zao wote kwa upanga wakiwaua na kuwaangamiza, nao walifanya kile walichotaka kwa wale waliowachukia.
A tak zbili Židé všecky nepřátely své, mečem hubíce, mordujíce a vyhlazujíce je, a nakládajíce s těmi, kteříž je v nenávisti měli, podlé líbosti své.
6 Katika ngome ya Shushani Wayahudi waliua na kuangamiza wanaume 500.
Ano i v Susan městě královském zmordovali Židé a vyhladili pět set mužů.
7 Pia waliwaua Parshendatha, Dalfoni, Aspatha,
A Parsandata, Dalfona i Aspata,
8 Poratha, Adalia, Ardatha,
A Porata, Adalia i Aridata,
9 Parmashta, Arisai, Aridai na Waizatha,
I Parimasta, Arisai i Aridai a Vajezata,
10 wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchukua nyara.
Deset synů Amana syna Hammedatova, nepřítele Židovského, zmordovali. Ale k loupeži nevztáhli ruky své.
11 Mfalme aliarifiwa siku iyo hiyo hesabu ya waliouawa katika ngome ya Shushani.
Dne toho, když se donesl krále počet zmordovaných v Susan městě královském,
12 Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wamewaua wanaume 500 na wana kumi wa Hamani ndani ya ngome ya Shushani. Wamefanyaje katika majimbo mengine ya mfalme yaliyobaki? Je, sasa haja yako ni nini? Nayo pia utapewa. Nalo ombi lako ni nini? Nalo utafanyiwa.”
Řekl král Esteře královně: V Susan městě královském zmordovali Židé a vyhladili pět set mužů, a deset synů Amanových. Co pak učinili v jiných krajinách královských? Již tedy jaká jest žádost tvá? A dánoť bude. Aneb která prosba tvá ještě? A staneť se.
13 Esta akajibu, “Ikimpendeza mfalme, uwape ruhusa Wayahudi walioko Shushani warudie amri ya leo kesho pia, na wana wa Hamani kumi wanyongwe mahali pa kunyongea watu.”
Odpověděla Ester: jestliže se králi za dobré vidí, nechť jest dopuštěno ještě zítra Židům, kteříž jsou v Susan, učiniti podlé výpovědi dnešní, a deset synů Amanových zvěšeti na šibenici.
14 Basi mfalme akaamuru kwamba hili litendeke. Amri ilitolewa huko Shushani, nao wakawanyonga wana kumi wa Hamani.
I přikázal král, aby se tak stalo. Tedy vyhlášena jest výpověd v Susan, a tak deset synů Amanových zvěšeli.
15 Wayahudi huko Shushani wakakusanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, nao wakawaua wanaume 300 huko Shushani, lakini hawakuchukua nyara zao.
A shromáždivše se Židé, kteříž byli v Susan, také i čtrnáctého dne měsíce Adar, zmordovali v Susan tři sta mužů. Ale k loupeži nevztáhli ruky své.
16 Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao.
Jiní také Židé, kteříž byli v krajinách královských, shromáždivše se, a zastávajíce života svého, tak odpočinuli od nepřátel svých. Zmordovali pak těch, jenž je v nenávisti měli, sedmdesáte pět tisíc. Ale k loupeži nevztáhli ruky své.
17 Hili lilitendeka siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari na siku ya kumi na nne walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
Stalo se to dne třináctého měsíce Adar. I odpočinuli čtrnáctého dne téhož měsíce, a učinili sobě v ten den hody a veselé.
18 Wayahudi huko Shushani, hata hivyo, walikuwa wamekusanyika siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne, pia siku ya kumi na tano walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
Ale Židé, kteříž byli v Susan, shromáždili se třináctého dne téhož měsíce a též čtrnáctého, a odpočinuli patnáctého, a učinili sobě na ten den hody a veselé.
19 Ndiyo sababu Wayahudi wanaokaa vijijini na katika miji midogo huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu, siku ambayo wao hupeana zawadi mmoja kwa mwingine.
Protož Židé, kteříž bydlí ve vsech a v městečkách nehrazených, světí den čtrnáctý měsíce Adar, majíce veselé, hody a dobrou vůli, a posílajíce částky pokrmů jedni druhým.
20 Mordekai aliandika matukio haya, naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote walioko katika majimbo ya Mfalme Ahasuero, majimbo yaliyo mbali na karibu,
Nebo rozepsal Mardocheus ty věci, a rozeslal listy ke všem Židům, kteříž byli ve všech krajinách krále Asvera, blízkým i dalekým,
21 akiwataka kila mwaka washerehekee siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ya mwezi wa Adari
Ustavuje jim, aby slavili den čtrnáctý měsíce Adar, a den patnáctý téhož měsíce každého roku,
22 kama wakati ambao Wayahudi walipata nafuu kutoka kwa adui zao na kama mwezi ambao huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha na kuomboleza kwao kuwa siku ya kusherehekea. Aliwaandikia kushika siku hizo kama siku za karamu na za furaha na kupeana zawadi za vyakula wao kwa wao na zawadi kwa maskini.
Podlé dnů těch, v nichž odpočinuli Židé od nepřátel svých, a měsíce toho, kterýž se jim obrátil z zámutku v radost, a z kvílení v dobrou vůli, aby ty dni slavili, hodujíce a veselíce se, a posílajíce částky pokrmů jeden druhému, i dary chudým.
23 Hivyo Wayahudi walikubali kuendeleza sherehe walizokuwa wamezianza, wakifanya lile Mordekai alilokuwa amewaandikia.
I přijali to všickni Židé, že budou činiti to, což začali, a což jim psal Mardocheus:
24 Kwa maana Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi, adui wa Wayahudi wote, alikuwa amepanga hila dhidi ya Wayahudi ili kuwaangamiza, na alikuwa amepiga puri (yaani kura) kwa ajili ya maangamizi na uharibifu wao.
Jak Aman syn Hammedatův Agagský, protivník všech Židů, ukládal o Židech, aby je vyhubil a uvrhl pur, totiž los, k setření a zahlazení jejich.
25 Lakini wakati shauri hilo baya lilipoarifiwa kwa mfalme, alitoa amri iliyoandikwa kwamba mipango mibaya ambayo Hamani ameipanga dhidi ya Wayahudi inapasa imrudie juu ya kichwa chake mwenyewe, na kwamba yeye na wanawe waangikwe mahali pa kunyongea watu.
Ale jak ona vešla před oblíčej krále, poručil král v listech, aby obráceni byli úkladové jeho nešlechetní, kteréž vymyslil proti Židům, na hlavu jeho, a aby ho oběsili i syny jeho na šibenici.
26 (Kwa hiyo siku hizi ziliitwa Purimu, kutokana na neno puri.) Kwa sababu ya kila kitu kilichoandikwa kwenye barua hii na kwa sababu ya yale waliyoyaona na yale yaliyowatokea,
I nazvali ty dny Purim, totiž losů, od jména toho pur. A tak z příčiny všech slov listu toho, a což viděli při tom, i což přišlo k nim,
27 Wayahudi wakachukua na kuifanya desturi kwamba wao na wazao wao na wote ambao walijiunga nao wangefanya bila kuacha kushika siku hizi mbili kila mwaka, kwa njia ilivyoelekezwa na kwa wakati wake.
Ustavili a přijali Židé na sebe i na símě své, i na všecky připojené k sobě, aby to nepominulo, že budou slaviti ty dva dni podlé vypsání jejich, a podlé určitého času jejich každého roku.
28 Siku hizi zinapasa zikumbukwe na kuadhimishwa katika kila kizazi, kila jamaa na katika kila jimbo na kila jiji. Nazo siku hizi za Purimu kamwe zisikome kusherehekewa na Wayahudi, wala kumbukumbu zake zisipotee miongoni mwa wazao wake.
A že ti dnové budou pamětní a slavní v každém věku, rodině, krajině a městě; k tomu, že ti dnové Purim nepominou z prostředku Židů, a památka jejich nepřestane u potomků jejich.
29 Basi Malkia Esta binti Abihaili, pamoja na Mordekai, Myahudi, waliandika kwa mamlaka yote kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
Psala také Ester královna, dcera Abichailova, i Mardocheus Žid pro větší upevnění psání z strany dnů Purim po druhé.
30 Naye Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo 127 ya ufalme wa Ahasuero, barua zenye maneno ya amani na matumaini,
A on rozeslal to psání ke všem Židům, do sta dvadcíti sedmi krajin království Asverova, vzkazuje jim pozdravení,
31 ili kuimarisha siku hizi za Purimu katika majira yake yaliyowekwa, kama Mordekai, Myahudi na Malkia Esta walivyowaamuru, na walivyojiimarisha wenyewe na wazao wao kuhusu nyakati za kufunga na kuomboleza.
Aby tuze drželi dny ty Purim v určité časy jich, jakž je nařídil jim Mardocheus Žid a Ester královna, a jakž to přijali na sebe a na símě své, na pamět postů a křiku jejich.
32 Amri ya Esta ilithibitisha taratibu hizi kuhusu Purimu, nayo ikaandikwa katika kumbukumbu.
A tak výpověd Estery potvrdila ustanovení dnů Purim, což zapsáno jest v knize této.

< Esta 9 >