< Esta 7 >

1 Basi mfalme na Hamani wakaenda kula chakula pamoja na Malkia Esta.
I tako doðe car i Aman na objed carici Jestiri.
2 Walipokuwa wakinywa mvinyo katika siku ya pili, mfalme akauliza tena, “Malkia Esta, ni nini haja yako? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”
I reèe car Jestiri opet drugi dan napivši se vina: šta želiš, carice Jestiro? daæe ti se; i šta moliš? ako je i do polovine carstva, biæe.
3 Kisha Malkia Esta akajibu, “Kama nimepata kibali kwako, ee mfalme, tena kama inapendeza utukufu wako, nijalie maisha yangu, hii ndiyo haja yangu. Pia uokoe watu wangu, hili ndilo ombi langu.
Tada odgovori carica Jestira i reèe: ako sam našla milost pred tobom, care, i ako je caru ugodno, neka mi se pokloni život moj na moju želju i narod moj na moju molbu.
4 Kwa kuwa mimi na watu wangu tumeuzwa kwa kuangamizwa, kuchinjwa na kuharibiwa. Kama tungalikuwa tumeuzwa tu kuwa watumwa wa kiume na wa kike, ningalinyamaza kimya, kwa sababu shida kama hii isingalitosha kumsumbua mfalme.”
Jer smo prodani ja i moj narod da nas potru, pobiju i istrijebe. Da smo prodani da budemo sluge i sluškinje, muèala bih, premda neprijatelj ne bi mogao naknaditi štete caru.
5 Mfalme Ahasuero akamuuliza Malkia Esta, “Ni nani huyu? Yuko wapi mtu huyu aliyethubutu kufanya jambo kama hili?”
A car Asvir progovori i reèe carici Jestiri: ko je taj? i gdje je taj koji se usudio tako èiniti?
6 Esta akasema, “Mtesi na adui ni huyu mwovu Hamani.” Hamani alifadhaika mbele ya mfalme na malkia.
A Jestira reèe: protivnik i neprijatelj ovaj je zlikovac Aman. A Aman se uplaši od cara i od carice.
7 Mfalme akainuka kwa ghadhabu, akaacha mvinyo wake, akaenda kwenye bustani ya jumba la kifalme. Lakini Hamani, akitambua kwamba mfalme ameshaamua hatima yake, alibaki nyuma kumsihi Malkia Esta aokoe maisha yake.
Tada car gnjevan usta od vina i otide u vrt kod dvora, a Aman osta da moli za život svoj caricu Jestiru, jer vidje da je car naumio zlo po nj.
8 Mara mfalme aliporudi kutoka bustani ya jumba la kifalme na kuja kwenye ukumbi wa karamu, Hamani alikuwa akijitupa juu ya kiti mahali ambapo Esta alikuwa akiegemea. Mfalme akasema kwa nguvu, “Je, atamdhalilisha malkia hata huku nyumbani akiwa pamoja nami!” Mara neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, walifunika uso wa Hamani.
Potom se car vrati iz vrta dvorskoga u kuæu gdje bješe pio vino; a Aman bješe pao na odar gdje sjeðaše Jestira. I car reèe: eda li æe i caricu osramotiti kod mene u kuæi? Èim ta rijeè izide iz usta carevijeh, pokriše lice Amanu.
9 Kisha Harbona, mmoja wa matowashi wanaomtumikia mfalme, akasema, “Mahali pa kuangika watu penye urefu wa mita ishirini na mbili pako nyumbani mwa Hamani. Alikuwa amepatengeneza kwa ajili ya Mordekai, ambaye alizungumza ili kumsaidia mfalme.” Mfalme akasema, “Mwangikeni juu yake!”
I Arvona, jedan od dvorana carevijeh, reèe: evo i vješala što je naèinio Aman za Mardoheja koji je govorio dobro po cara stoje kod kuæe Amanove, visoka pedeset lakata. I reèe car: objesite ga na njih.
10 Kwa hiyo wakamtundika Hamani mahali alipokuwa ameandaa kwa ajili ya Mordekai. Ndipo ghadhabu ya mfalme ikatulia.
I tako objesiše Amana na vješala koja bješe pripravio Mardoheju. I gnjev carev utiša se.

< Esta 7 >