< Esta 7 >
1 Basi mfalme na Hamani wakaenda kula chakula pamoja na Malkia Esta.
Therfor the kyng and Aaman entriden to the feeste, to drynke with the queen.
2 Walipokuwa wakinywa mvinyo katika siku ya pili, mfalme akauliza tena, “Malkia Esta, ni nini haja yako? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”
And the kyng seide to hir, yhe, in the secounde dai, aftir that he was hoot of the wiyn, Hester, what is thin axyng, that it be youun to thee, and what wolt thou be doon? Yhe, thouy thou axist the half part of my rewme, thou schalt gete.
3 Kisha Malkia Esta akajibu, “Kama nimepata kibali kwako, ee mfalme, tena kama inapendeza utukufu wako, nijalie maisha yangu, hii ndiyo haja yangu. Pia uokoe watu wangu, hili ndilo ombi langu.
To whom sche answeride, A! king, if Y haue founde grace in thin iyen, and if it plesith thee, yyue thou my lijf to me, for which Y preie, and my puple, for which Y biseche.
4 Kwa kuwa mimi na watu wangu tumeuzwa kwa kuangamizwa, kuchinjwa na kuharibiwa. Kama tungalikuwa tumeuzwa tu kuwa watumwa wa kiume na wa kike, ningalinyamaza kimya, kwa sababu shida kama hii isingalitosha kumsumbua mfalme.”
For Y and my puple ben youun, that we be defoulid, and stranglid, and that we perische; `and Y wolde, that we weren seeld in to seruauntis and seruauntessis, `and the yuel `were suffrable, and Y `were stille weilynge; but now oure enemy is, whos cruelte turneth `in to the kyng.
5 Mfalme Ahasuero akamuuliza Malkia Esta, “Ni nani huyu? Yuko wapi mtu huyu aliyethubutu kufanya jambo kama hili?”
And kyng Assuerus answeride, and seide, Who is this, and of what power, that he be hardi to do these thingis?
6 Esta akasema, “Mtesi na adui ni huyu mwovu Hamani.” Hamani alifadhaika mbele ya mfalme na malkia.
And Hester seide, Oure worste aduersarie and enemy is this Aaman. Which thing he herde, and was astonyde anoon, and `suffride not to bere the semelaunt of the kyng and of the queen.
7 Mfalme akainuka kwa ghadhabu, akaacha mvinyo wake, akaenda kwenye bustani ya jumba la kifalme. Lakini Hamani, akitambua kwamba mfalme ameshaamua hatima yake, alibaki nyuma kumsihi Malkia Esta aokoe maisha yake.
Forsothe the kyng roos wrooth, and fro the place of the feeste he entride in to a gardyn biset with trees. And Aaman roos for to preie Hester, the queen, for his lijf; for he vndurstood yuel maad redi of the kyng to hym.
8 Mara mfalme aliporudi kutoka bustani ya jumba la kifalme na kuja kwenye ukumbi wa karamu, Hamani alikuwa akijitupa juu ya kiti mahali ambapo Esta alikuwa akiegemea. Mfalme akasema kwa nguvu, “Je, atamdhalilisha malkia hata huku nyumbani akiwa pamoja nami!” Mara neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, walifunika uso wa Hamani.
And whanne the kyng turnede ayen fro the gardyn `biset with wode, and hadde entrid in to the place of feeste he foond that Aaman felde doun on the bed, wherynne Hester lai. And the king seide, `Also he wole oppresse the queen, while Y am present, in myn hows. The word was not yit goon out of the kyngis mouth, and anoon thei hiliden his face.
9 Kisha Harbona, mmoja wa matowashi wanaomtumikia mfalme, akasema, “Mahali pa kuangika watu penye urefu wa mita ishirini na mbili pako nyumbani mwa Hamani. Alikuwa amepatengeneza kwa ajili ya Mordekai, ambaye alizungumza ili kumsaidia mfalme.” Mfalme akasema, “Mwangikeni juu yake!”
And Arbona seide, oon of the onest seruauntis and chast, that stoden in the seruyce of the kyng, Lo! the tre hauynge fifti cubitis of heiythe stondith in the hows of Aaman, which tre he hadde maad redi to Mardochee, that spak for the kyng. To whom the kyng seide, Hange ye Aaman in that tre.
10 Kwa hiyo wakamtundika Hamani mahali alipokuwa ameandaa kwa ajili ya Mordekai. Ndipo ghadhabu ya mfalme ikatulia.
Therfor Aaman was hangid in the iebat, which he hadde maad redi to Mardochee, and the ire of the kyng restide.