< Esta 6 >

1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
Cette nuit-là le sommeil fuyait le roi, et il dit qu'on lui apportât le livre mémorial, les annales; et il en fut fait, lecture devant le roi.
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
Là se trouvait consignée la révélation faite par Mardochée au sujet de Bigthan et Thérès, les deux eunuques du roi d'entre les gardes du seuil, qui avaient cherché à porter la main sur le roi Assuérus.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
Et le roi dit: Quel prix et quel honneur Mardochée a-t-il obtenus pour cela? Et les écuyers du roi qui étaient de service auprès de lui, dirent: Il n'a rien reçu.
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
Et le roi dit: Qui est dans la cour? Or Aman arrivait dans la cour extérieure du palais royal, pour proposer au roi de faire pendre Mardochée au poteau qu'il avait préparé pour lui.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
Et les écuyers du roi lui dirent: Voilà, c'est Aman qui est dans la cour. Et le roi dit: Qu'il entre.
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
Et Aman entra, et le roi lui dit: Que faut-il faire à un homme que le roi veut récompenser? Et Aman disait en son cœur: Qui est-ce que le roi voudrait récompenser sinon moi?
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
Et Aman dit au roi: L'homme que le roi veut récompenser!…
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
il faut apporter un habillement royal dont le roi se revêt, et le cheval que le roi monte, et sur la tête duquel on place la couronne royale,
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
puis remettre l'habillement et le cheval à quelqu'un des Grands du roi, des nobles, et revêtir l'homme que le roi veut récompenser, et le promener monté sur le cheval dans les rues de la ville en criant devant lui: Ainsi est traité l'homme que le roi veut récompenser!
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
Et le roi dit à Aman: Vite, prends l'habillement et le cheval, comme tu as dit, et fais ainsi pour Mardochée, le Juif, qui est assis dans la porte du roi; n'omets aucun des points que tu as indiqués.
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
Alors Aman prit l'habillement et le cheval, et revêtit Mardochée et le conduisit par les rues de la ville en criant devant lui: Ainsi est traité l'homme que le roi veut récompenser!
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
Et Mardochée revint à la porte du roi, mais Aman regagna en hâte sa maison, triste et la tête voilée.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
Et Aman raconta à Zérès, sa femme, et à tous ses amis tout ce qui lui était arrivé. Alors ses sages et Zérès, sa femme, lui dirent: Si Mardochée, devant qui tu as commencé de tomber, est de la race des Juifs, tu ne l'emporteras pas sur lui, mais c'est toi qui tomberas devant lui.
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
Ils s'entretenaient encore avec lui, lorsque arrivèrent les eunuques du roi, qui se hâtèrent de conduire Aman au banquet préparé par Esther.

< Esta 6 >