< Esta 6 >

1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
Or, cette nuit-là, le Seigneur éloigna du roi le sommeil, et Artaxerxès dit à son serviteur d'apporter le livre de ses archives et de le lui lire.
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
Et il tomba sur ce qui était écrit concernant Mardochée, quand il avait fait connaître au roi le complot des deux eunuques qui le gardaient, et qui voulaient porter les mains sur lui.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
Et le roi dit: Quels honneurs, quelle grâce Mardochée a-t-il reçus de moi? Et les serviteurs répondirent: Tu n'as rien fait pour lui.
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
Pendant que le roi se rappelait le zèle de Mardochée, Aman entra dans le parvis, et le roi dit: Y a-t-il quelqu'un dans le parvis? Or, Aman arrivait pour demander au roi de pendre Mardochée à la potence qu'il avait dressée.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
Et les serviteurs du roi répondirent: Voilà Aman dans le parvis. Et le roi dit: Appelez-le.
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
Et le roi dit à Aman: Que ferai-je pour l'homme que je veux glorifier? Et Aman se dit: Qui donc le roi veut-il glorifier, si ce n'est moi?
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
Et il répondit: Pour l'homme que le roi veut glorifier,
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
Que les serviteurs du roi apportent la robe de fin lin dont il se revêt, et le cheval qu'il monte.
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
Que cela soit donné à l'un des amis du roi, parmi ceux du premier rang; qu'il habille l'homme que le roi aime, qu'il le fasse monter à cheval, que dans toutes les places de la ville il proclame ces mots: Ainsi sera-t-il fait à tout homme que le roi honore.
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
Et le roi dit à Aman: Tu as bien parlé; ainsi soit fait par toi au Juif Mardochée qui sert en mon parvis, et que rien ne soit négligé de ce que tu as dit.
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
Aman prit donc la robe, et le cheval, et il habilla Mardochée, et il le fit monter à cheval, et il parcourut toutes les rues de la ville, et il proclama ces mots: Ainsi sera-t-il fait à tout homme que le roi voudra honorer.
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
Et Mardochée revint au parvis, et Aman rentra en sa demeure avec un grand mal de tête.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
Et il fit à Zosara, sa femme, et à ses amis, le récit de ce qui était advenu; et ses amis et sa femme lui dirent: Si Mardochée est de la race des Juifs, tu as commencé à être humilié devant lui; tu tomberas; et tu ne pourras te défendre contre lui; car le Dieu vivant est avec lui.
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
Comme ils parlaient encore, les eunuques vinrent presser Aman de se rendre au repas qu'Esther avait préparé.

< Esta 6 >