< Esta 6 >
1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
The kyng ledde that nyyt with out sleep, and he comaundide the stories and the bookis of yeeris `of formere tymes to be brouyt to hym. And whanne tho weren red in his presense,
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
me cam to the place, where it was writun, hou Mardochee hadde teld the tresouns of Gabathan and Thares, oneste seruauntis, couetynge to strangle kyng Assuerus.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
And whanne the kyng hadde herd this, he seide, What onour and meede gat Mardochee for this feithfulnesse? And hise seruauntis and mynystris seiden to hym, Outirli he took no meede.
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
And anoon the kyng seide, Who is in the halle? Sotheli Aaman hadde entrid in to the ynnere halle of the kyngis hows, to make suggestioun to the kyng, that he schulde comaunde Mardochee to be hangid on the iebat, which was maad redi to him.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
And the children answeriden, Aaman stondith in the halle.
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
And the kyng seide, Entre he. And whanne he was comun yn, the kyng seide to hym, What owith to be don to the man, whom the kyng desirith onoure? Aaman thouyte in his herte, and gesside, that the kyng wolde onoure noon othere man no but hym silf;
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
and he answeride, The man, whom the kyng couetith to onoure,
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
owith to be clothid with the kyngis clothis, and to be set on the hors which is of the kyngis sadel, and to take the kyngis diademe on his heed;
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
and the firste of the princes and stronge men of the kyng holde his hors, and go bi the stretis of the citee, and crie, and seie, Thus he schal be onourid, whom euer the kyng wole onoure.
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
Therfor the kyng seide to hym, Haste thou, and whanne `a stoole and hors is takun, do thou, as thou hast spoke, to Mardochee the Jew, that sittith bifor the yatis of the paleis; be thou war, that thou leeue not out ony thing of these, whiche thou hast spoke.
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
Therfor Aaman took `a stoole and hors, and yede, and criede bifor Mardochee clothid in the strete of the citee, and set on `the hors, He is worthi this onour, whom euer the kyng wole onoure.
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
And Mardochee turnede ayen to the yate of the paleis, and Aaman hastide to go in to his hows, morenynge, and with the heed hilid.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
And he teld to Zares, his wijf, and to frendis alle thingis that hadden bifelde to hym. To whom the wise men, whiche he hadde in counsel, and his wijf, answeriden, If Mardochee, bifor whom thou hast bigunne to falle, is of the seed of Jewis, thou schalt not mowe ayenstonde hym, but thou schalt falle in his siyt.
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
Yit while thei spaken, the oneste seruauntis and chast of the kyng camen, and compelliden hym to go soone to the feeste, which the queen hadde maad redi.