< Esta 6 >
1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
On that night the king was unable to sleep, so he gave orders to bring the books that recorded memorable deeds, and they were read before the king.
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
It was found recorded how Mordecai had furnished information regarding Bigthan and Teresh, two of the king’s attendants who guarded the entrance of the palace, who had attempted to kill King Ahasuerus.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
“What honor and dignity have been conferred on Mordecai for this?” the king asked. When the king’s pages who waited on him replied “Nothing has been done for him,”
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
the king said, “Who is in the court?” Now Haman had just entered the outer court of the king’s house to speak to the king about hanging Mordecai on the gallows that he had prepared for him.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
So the king’s pages said to him, “Haman is standing there, in the court.” The king said, “Let him enter.”
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
So Haman entered, and the king said to him, “What should be done for the man whom the king wishes to honor?” Haman said to himself, “Whom besides me could the king wish to honor?”
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
So he said to the king, “For the man whom the king wishes to honor
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
let a royal garment be brought, which the king has worn, and the horse on which the king has ridden and on whose head a royal diadem has been placed.
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
Then let the garment and the horse be placed in charge of one of the king’s noble officials. Let him clothe the man whom the king wishes to honor and let him lead that man on the horse through the city square, proclaiming before him, ‘This is what is done for the man whom the king wishes to honor.’”
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
Then the king said to Haman, “Make haste and take the garment and the horse, as you have said, and do this to Mordecai the Jew, who sits in the king’s gate. Omit nothing of all you have said.”
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
So Haman took the garment and the horse and clothed Mordecai, and made him ride through the city square and proclaimed before him, “This is what is done for the man whom the king wishes to honor.”
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
Mordecai returned to the king’s gate, but Haman hurried to his house, mourning, with his head covered.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
Haman recounted to Zeresh his wife and to all his friends everything that had happened to him. Then his wise men and Zeresh his wife said to him, “If Mordecai before whom you have already been humiliated is of the Jewish people, you can do nothing against him but will surely fall before him.”
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
While they were still talking with him, the king’s attendants came and quickly took Haman to the banquet that Esther had prepared.