< Esta 6 >

1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
The king passed that night without sleep, and so he ordered the histories and chronicles of former times to be brought to him. And when they were reading them before him,
2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
they came to that place where it had been written, how Mordecai had reported the treachery of Bigthan and Teresh the eunuchs, who desired to cut the throat of king Artaxerxes.
3 Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
When the king had heard this, he said, “What honor and reward has Mordecai been given for this fidelity?” His servants and ministers said to him, “He has received no compensation at all.”
4 Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
And immediately the king said, “Who is in the atrium?” For, you see, Haman was entering the inner atrium of the king’s house to suggest to the king that he should order Mordecai to be hanged on the gallows, which had been prepared for him.
5 Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
The servants answered, “Haman is standing in the atrium.” And the king said, “Let him enter.”
6 Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
And when he had entered, he said to him, “What ought to be done for the man whom the king wishes to honor?” But Haman, thinking in his heart and supposing that the king would honor no one else but himself,
7 Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
answered, “The man whom the king wishes to honor,
8 aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
ought to be clothed with the king’s apparel, and be set upon the horse that the king rides, and receive the royal crown upon his head.
9 Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
And let the first of the king’s rulers and sovereigns hold his horse, and, as they advance through the street of the city, proclaim before him and say, ‘Thus shall he be honored, whom the king decides to honor.’”
10 Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
And the king said to him, “Hurry, take the robe and the horse, and do as you have said to Mordecai the Jew, who sits in front of the gate of the palace. Be careful not to omit any of those things which you have mentioned.”
11 Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
And so Haman took the robe and the horse, and arraying Mordecai in the street of the city, and setting him on the horse, he went before him and cried out, “He is worthy of this honor, whom the king has decided to honor.”
12 Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
And Mordecai returned to the palace door. And Haman hurried to go to his house, mourning and hiding his head.
13 naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
And he explained to Zeresh his wife and to his friends all that had happened to him. And the wise men, whom he held in counsel, and his wife, answered him, “If Mordecai, before whom you have begun to fall, is from the offspring of the Jews, you will not be able to withstand him, but you will fall in his sight.”
14 Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.
As they were still speaking, the king’s eunuchs arrived and compelled him to go quickly to the feast, which the queen had prepared.

< Esta 6 >