< Esta 4 >

1 Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
Lorsque Mardochée eut appris cela, il déchira ses vêtements, et se revêtit d’un sac, répandant de la cendre sur sa tête; et sur la place du milieu de la ville il criait d’une voix forte, témoignant l’amertume de son âme,
2 Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
Et au milieu de ces lamentations, s’avançant jusqu’à la porte du palais: car il n’était pas permis d’entrer revêtu d’un sac dans le palais du roi.
3 Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
Dans toutes les provinces aussi, dans les villes et dans les lieux dans lesquels l’édit cruel du roi était parvenu, il y avait parmi les Juifs un grand deuil, un jeûne, des cris déchirants, beaucoup se servant de sac et de cendre au lieu de lit.
4 Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
Or les jeunes filles d’Esther et les eunuques entrèrent, et le lui annoncèrent. En l’apprenant, elle fut consternée, et elle envoya un habit à Mardochée, afin qu’on lui ôtât son sac et qu’on le revêtît de cet habit; il ne voulut point le recevoir.
5 Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
Alors, ayant fait venir Athach, l’eunuque que le roi lui avait donné pour serviteur, elle lui ordonna d’aller vers Mardochée et d’apprendre de lui pourquoi il faisait cela.
6 Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
Or Athach, étant sorti, alla vers Mardochée, qui se tenait sur la place de la ville, devant la porte du palais.
7 Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
Mardochée lui apprit tout ce qui était arrivé, de quelle manière Aman avait promis de porter de l’argent dans les trésors du roi par le moyen du massacre des Juifs.
8 Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
Il lui donna aussi un exemplaire de l’édit qui était affiché dans Suse, afin qu’il le montrât à la reine, et qu’il l’avertît d’entrer chez le roi et de le prier pour son peuple.
9 Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
Etant revenu, Athach annonça à Esther tout ce que Mardochée lui avait dit.
10 Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
Esther lui répondit, et lui commanda de dire à Mardochée:
11 “Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
Tous les serviteurs du roi et toutes les provinces qui sont sous sa domination, savent que si un homme ou une femme, qui n’a pas été appelé, entre dans le vestibule intérieur du roi, il est sans aucun délai tué sur-le-champ, à moins que le roi ne tende son sceptre d’or vers lui en signe de clémence, et qu’ainsi il puisse vivre. Comment donc moi pourrai-je entrer vers le roi, moi qui, depuis déjà trente jours, n’ai pas été appelée auprès de lui?
12 Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
Ce qu’ayant entendu, Mardochée
13 Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
Manda de nouveau à Esther, disant: Ne pensez pas, parce que vous êtes dans la maison du roi, que vous sauverez seule votre vie, plutôt que tous les autres Juifs;
14 Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
Car, si maintenant vous gardez le silence, les Juifs seront délivrés par un autre moyen, et vous, et la maison de votre père, vous périrez. Et qui sait si vous n’êtes point parvenue à la dignité royale uniquement afin que vous fussiez préparée pour un pareil temps?
15 Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
Et Esther manda de nouveau à Mardochée ces mots:
16 “Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
Allez et assemblez tous les Juifs que vous trouverez dans Suse, et priez pour moi. Ne mangez et ne buvez point durant trois jours et trois nuits; et moi, je jeûnerai également avec mes filles, et alors j’entrerai auprès du roi, agissant contre la loi, n’ayant pas été appelée, et m’abandonnant à la mort et au péril.
17 Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.
C’est pourquoi Mardochée alla, et fit tout ce qu’Esther lui avait ordonné.

< Esta 4 >