< Esta 4 >

1 Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
Lorsque Mardochée eut appris tout ce qui s'était passé, il déchira ses vêtements, se revêtit d'un sac de cendre, sortit au milieu de la ville et poussa de grands cris et des larmes amères.
2 Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
Il alla même jusqu'à la porte du roi, car personne ne peut entrer dans la porte du roi vêtu d'un sac.
3 Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
Dans toutes les provinces, partout où arrivèrent l'ordre du roi et son décret, il y eut parmi les Juifs un grand deuil, un jeûne, des pleurs et des gémissements, et beaucoup se couchèrent dans le sac et la cendre.
4 Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
Les servantes d'Esther et ses eunuques vinrent lui raconter cela, et la reine fut extrêmement peinée. Elle envoya des vêtements à Mardochée, pour remplacer son sac, mais il ne les reçut pas.
5 Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
Alors Esther appela Hathac, l'un des eunuques du roi, qu'elle avait désigné pour la servir, et lui ordonna d'aller voir Mardochée pour savoir ce que c'était et pourquoi.
6 Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
Hathac sortit donc vers Mardochée, sur la place de la ville qui était devant la porte du roi.
7 Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
Mardochée lui raconta tout ce qui lui était arrivé, et la somme exacte de l'argent qu'Haman avait promis de verser aux trésors du roi pour la destruction des Juifs.
8 Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
Il lui donna aussi la copie de l'écriture du décret qui avait été publié à Suse pour les détruire, afin de la montrer à Esther, de la lui déclarer et de l'inciter à aller voir le roi pour l'implorer et demander devant lui pour son peuple.
9 Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
Hathac vint et rapporta à Esther les paroles de Mardochée.
10 Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
Alors Esther parla à Hathac et lui donna un message pour Mardochée:
11 “Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
« Tous les serviteurs du roi et le peuple des provinces du roi savent que quiconque, homme ou femme, se présente au roi dans la cour intérieure sans être appelé, n'a qu'une seule loi, celle d'être mis à mort, sauf ceux à qui le roi tendrait le sceptre d'or pour qu'ils vivent. Je n'ai pas été appelé à entrer chez le roi depuis trente jours. »
12 Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
Ils rapportèrent les paroles d'Esther à Mardochée.
13 Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
Alors Mardochée leur demanda de rendre cette réponse à Esther: « Ne pense pas en toi-même que tu échapperas à la maison du roi, pas plus que tous les Juifs.
14 Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
Car si tu te tais maintenant, le secours et la délivrance viendront aux Juifs d'un autre endroit, mais toi et la maison de ton père périront. Qui sait si tu n'es pas venu dans le royaume pour un moment comme celui-ci? »
15 Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
Esther leur demanda alors de répondre à Mardochée:
16 “Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
« Allez, rassemblez tous les Juifs qui se trouvent à Suse, et jeûnez pour moi, sans manger ni boire pendant trois jours, nuit et jour. Moi et mes jeunes filles, nous jeûnerons aussi de la même manière. Ensuite, j'irai trouver le roi, ce qui est contraire à la loi; et si je péris, je péris. »
17 Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.
Mardochée s'en alla donc et fit tout ce qu'Esther lui avait ordonné.

< Esta 4 >