< Esta 4 >

1 Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
And whanne Mardochee hadde herd these thingis, he to-rente hise clothis, and he was clothid in a sak, and spreynt aische on the heed, and he criede with greet vois in the street of the myddis of the citee, and schewide the bitternesse of his soule,
2 Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
and he yede with this yellyng `til to the yatis of the paleis; for it was not leueful a man clothid with a sak to entre in to the halle of the kyng.
3 Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
Also in alle prouynces, citees, and places, to which the cruel sentence of the king was comun, was greet weilyng, fastyng, yellyng, and wepyng anentis the Jewis, and many Jewis vsiden sak and aische for bed.
4 Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
Sotheli the dameselis and onest seruauntis and chast of Hester entriden, and telden to hir; which thing sche herde, and was astonyed; and sche sente a cloth to Mardochee, that whanne the sak was takun a wei, he schulde clothe hym therynne; which cloth he nolde take.
5 Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
And aftir that Athac, the onest seruaunt and chast, `was clepid, whom the kyng hadde youe a mynystre to hir, sche comaundide, that he schulde go to Mardochee, and lerne of hym, whi he dide this thing.
6 Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
And Athac yede out, and yede to Mardochee stondynge in the street of the citee, bifor the dore of the paleis;
7 Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
which schewide to Athac alle thingis that bifelden, hou Aaman hadde bihiyt to bryng siluer in to tresours of the kyng for the deeth of Jewis.
8 Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
Also he yaf to Athac the copie of the comaundement, that hangide in Susa, to schewe to the queen, and to moneste hir for to entre to the kyng, and to biseche hym for hir puple.
9 Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
And Athac yede ayen, and telde to Hester alle thingis, whiche Mardochee hadde seid.
10 Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
And sche answeryde to hym, and seide, that he schulde seie to Mardochee, Alle the seruauntis of the kyng,
11 “Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
and alle prouyncis that ben vndur his lordschip, knowen, that whether a man ether a womman not clepid entrith in to the ynnere halle of the kyng, he schal be slayn anoon with outen ony tariyng, no but in hap the kyng holdith forth the goldun yerde `to hym for `the signe of merci, and he mai lyue so; therfor hou mai Y entre to the kyng, which am not clepid to hym now bi thritti daies?
12 Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
And whanne Mardochee hadde herd `this thing, he sente efte to Hester,
13 Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
and seide, Gesse thou not, that thou schalt delyuer oonli thi lijf, for thou art in the hows of the kyng, bifor alle Jewis;
14 Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
for if thou art stille now, Jewis schulen be delyuered bi another occasioun, and thou and the hows of thi fadir schulen perische; and who knowith, whether herfor thou camist to the rewme, that thou schuldist be maad redi in sich a tyme?
15 Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
And eft Hester sente these wordis to Mardochee,
16 “Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
Go thou, and gadere togidere alle Jewis, whiche thou fyndist in Susa, and preie ye for me; ete ye not, nether drynke ye in thre daies and thre nyytis, and Y with myn handmaydis schal fast in lijk maner; and thanne Y not clepid schal entre to the kyng, and Y schal do ayens the lawe, and Y schal bitake me to deth and to perel.
17 Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.
Therfor Mardochee yede, and dide alle thingis, whiche Hester hadde comaundid to hym.

< Esta 4 >