< Esta 3 >

1 Baada ya matukio haya, Mfalme Ahasuero alimheshimu Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, akampandisha na kumpa kiti chake cha heshima cha juu sana kuliko wakuu wengine wote.
after [the] word: thing [the] these to magnify [the] king Ahasuerus [obj] Haman son: child Hammedatha [the] Agagite and to lift: exalt him and to set: make [obj] throne: seat his from upon all [the] ruler which with him
2 Maafisa wote wa mfalme waliokaa langoni mwa mfalme walipiga magoti na kumpa Hamani heshima, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru hili kuhusu Hamani. Lakini Mordekai hakumpigia magoti wala kumheshimu.
and all servant/slave [the] king which in/on/with gate [the] king to bow and to bow to/for Haman for so to command to/for him [the] king and Mordecai not to bow and not to bow
3 Kisha maafisa wa mfalme waliokuwa langoni mwa mfalme walimuuliza Mordekai, “Kwa nini hutii agizo la mfalme?”
and to say servant/slave [the] king which in/on/with gate [the] king to/for Mordecai why? you(m. s.) to pass: trespass [obj] commandment [the] king
4 Siku baada ya siku walizungumza naye lakini hakukubali. Kwa hiyo walimweleza Hamani kuona kama tabia ya Mordekai itaweza kuvumiliwa, kwa maana alikuwa amewaambia kuwa yeye ni Myahudi.
and to be (like/as to say they *Q(K)*) to(wards) him day: daily and day: daily and not to hear: hear to(wards) them and to tell to/for Haman to/for to see: see to stand: stand word Mordecai for to tell to/for them which he/she/it Jew
5 Wakati Hamani alipoona kuwa Mordekai hampigii magoti wala kumpa heshima alighadhibika.
and to see: see Haman for nothing Mordecai to bow and to bow to/for him and to fill Haman rage
6 Hata hivyo baada ya kujulishwa watu wa Mordekai ni akina nani, alibadili wazo la kumuua Mordekai peke yake. Badala yake Hamani alitafuta njia ya kuwaangamiza watu wote wa Mordekai, yaani, Wayahudi, walio katika ufalme wote wa Ahasuero.
and to despise in/on/with eye: appearance his to/for to send: reach hand in/on/with Mordecai to/for alone him for to tell to/for him [obj] people Mordecai and to seek Haman to/for to destroy [obj] all [the] Jew which in/on/with all royalty Ahasuerus people Mordecai
7 Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Mfalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza uitwao Nisani, walipiga puri (yaani kura) mbele ya Hamani ili kuchagua siku na mwezi. Kura ikaangukia kwenye mwezi wa kumi na mbili, yaani Adari.
in/on/with month [the] first he/she/it month Nisan in/on/with year two ten to/for king Ahasuerus to fall: allot Purim he/she/it [the] allotted to/for face: before Haman from day to/for day and from month to/for month (and to fall: fall [the] allotted upon three ten day to/for month *X*) two ten he/she/it month Adar
8 Kisha Hamani akamwambia Mfalme Ahasuero, “Wako watu fulani wameenea na kutawanyika miongoni mwa watu katika majimbo yote ya ufalme wako, ambao desturi zao ni tofauti na zile za watu wengine wote, nao hawatii sheria za mfalme. Haifai mfalme kuwavumilia watu hawa.
and to say Haman to/for king Ahasuerus there he people one to scatter and to separate between: among [the] people in/on/with all province royalty your and law their to change from all people and [obj] law [the] king nothing they to make: do and to/for king nothing be like to/for to rest them
9 Kama inampendeza mfalme, itolewe amri kuwaangamiza, nami nitaweka talanta 10,000 za fedha katika hazina ya mfalme kwa ajili ya watu watakaoshughulikia jambo hili.”
if upon [the] king pleasant to write to/for to perish them and ten thousand talent silver: money to weigh upon hand to make: do [the] work to/for to come (in): bring to(wards) treasury [the] king
10 Basi mfalme alichukua pete yake ya muhuri kutoka kwenye kidole chake na kumpa Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, adui wa Wayahudi.
and to turn aside: remove [the] king [obj] ring his from upon hand his and to give: give her to/for Haman son: child Hammedatha [the] Agagite to vex [the] Jew
11 Mfalme akamwambia Hamani, “Baki na fedha yako na uwatendee hao watu utakavyo.”
and to say [the] king to/for Haman [the] silver: money to give: give to/for you and [the] people to/for to make: do in/on/with him like/as pleasant in/on/with eye: appearance your
12 Kisha siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza waandishi wa mfalme waliitwa. Wakaandika barua kwa kila jimbo na katika kila lugha ya watu kama agizo la Hamani lilivyotoka kwa mfalme, kwa watawala wa majimbo mbalimbali, na wakuu wa watu mbalimbali. Hizi ziliandikwa kwa jina la Mfalme Ahasuero mwenyewe na kutiwa muhuri wa pete yake mwenyewe.
and to call: call to scribe [the] king in/on/with month [the] first in/on/with three ten day in/on/with him and to write like/as all which to command Haman to(wards) satrap [the] king and to(wards) [the] governor which upon province and province and to(wards) ruler people and people province and province like/as writing her and people and people like/as tongue: language his in/on/with name [the] king Ahasuerus to write and to seal in/on/with ring [the] king
13 Barua zilipelekwa na tarishi katika majimbo yote ya mfalme zikiwa na amri ya kuharibu, kuua na kuangamiza Wayahudi wote, wadogo kwa wakubwa, wanawake na watoto wadogo, siku moja, yaani siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, na pia kuteka nyara vitu vyao.
and to send: depart scroll: document in/on/with hand: by [the] to run: run to(wards) all province [the] king to/for to destroy to/for to kill and to/for to perish [obj] all [the] Jew from youth and till old child and woman in/on/with day one in/on/with three ten to/for month two ten he/she/it month Adar and spoil their to/for to plunder
14 Nakala ya andiko la amri ilipaswa kutolewa kama sheria katika kila jimbo, na kufahamishwa kwa watu wa kila taifa ili waweze kuwa tayari kwa siku ile.
copy [the] writing to/for to give: give law in/on/with all province and province to reveal: proclaim to/for all [the] people to/for to be ready to/for day [the] this
15 Kwa kuharakishwa na amri ya mfalme, matarishi walikwenda na andiko lilitolewa katika mji wa ngome ya Shushani. Mfalme na Hamani waliketi na kunywa, lakini mji wa Shushani ulifadhaika.
[the] to run: run to come out: come to hasten in/on/with word [the] king and [the] law to give: give in/on/with Susa [the] palace and [the] king and Haman to dwell to/for to drink and [the] city Susa to perplex

< Esta 3 >