< Esta 2 >
1 Baadaye, wakati hasira ya Mfalme Ahasuero ilikuwa imetulia, alimkumbuka Vashti na kile alichokuwa amekifanya na alilokuwa ameamuru juu yake.
Sedan detta skedt var, när Konungens Ahasveros vrede hade saktat sig, kom han Vasthi ihåg, hvad hon gjort hade, och hvad om henne beslutet var.
2 Kisha watumishi waliomhudumia mfalme walipendekeza, “Na ufanyike utafiti kwa ajili ya wanawali mabikira wazuri wa sura kwa ajili ya mfalme.
Då sade Konungens svenner, som honom tjente: Man söke Konungenom upp dägeliga unga jungfrur;
3 Mfalme na ateue maafisa katika kila jimbo la himaya yake kuwaleta hao wanawali wote wazuri wa sura katika nyumba ya wanawake katika ngome ya mji wa Shushani. Kisha wawekwe chini ya utunzaji wa Hegai, towashi wa mfalme, msimamizi wa wanawake; na wapewe matunzo yote ya urembo.
Och Konungen beställe skådare i all land i sitt rike, att de låta komma tillhopa alla dägeliga unga jungfrur, intill den staden Susan i fruhuset, under Hegai hand, Konungens kamererares, hvilken qvinnorna vakta skulle, och få dem deras skrud;
4 Kisha yule ambaye atampendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti.” Shauri hili likampendeza mfalme, naye akalifuata.
Och hvilken pigan Konungenom täckes, den blifve Drottning i Vasthis stad. Det behagade Konungenom, och han gjorde så.
5 Basi katika mji wa ngome ya Shushani palikuwa na Myahudi wa kabila ya Benyamini, jina lake Mordekai mwana wa Yairi, mwana wa Shimei, mwana wa Kishi,
Då var en Judisk man i Susans stad, han het Mardechai, Jairs son, Simei sons, Kis sons, Jemini sons;
6 ambao walichukuliwa uhamishoni kutoka Yerusalemu na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, wakiwa miongoni mwa waliochukuliwa mateka pamoja na Mfalme Yekonia wa Yuda.
Den med bortförd var ifrå Jerusalem, då Jechonia, Juda Konung, bortförd var, hvilken NebucadNezar, Konungen i Babel, bortförde.
7 Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
Och han var förmyndare till Hadassa, denna är Esther, sins faderbroders dotter; förty hon hade hvarken fader eller moder, och hon var en fager och dägelig piga; och då hennes fader och moder blefvo döde, tog Mardechai henne för sin dotter.
8 Wakati agizo na amri ya mfalme lilitangazwa, wanawali wengi waliletwa kwenye ngome ya mji wa Shushani na kuwekwa chini ya uangalizi wa Hegai. Pia Esta alipelekwa katika jumba la mfalme na akakabidhiwa Hegai, aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake.
Då Konungens bud och beslut vardt kunnigt, och många pigor voro tillhopahemtade till staden Susan, under Hegai hand, vardt Esther ock tagen uti Konungshuset, under Hegai hand, qvinnovaktarens.
9 Msichana huyu alimpendeza na kupata kibali mbele zake. Mara moja akaanza kumpa matunzo ya uzuri na chakula maalum. Alimpa Esta vijakazi saba waliochaguliwa kutoka jumba la kifalme, na kumhamishia yeye pamoja na vijakazi wake katika sehemu bora zaidi katika nyumba ya wanawake.
Och pigan täcktes honom, och hon fann barmhertighet för honom; och han skyndade sig med hennes skrud, att han skulle få henne hennes del, och sju dägeliga pigor utaf Konungshuset dertill; och han satte henne med hennes pigor uti bästa rummet i fruhuset.
10 Esta alikuwa hajadhihirisha uraia wala kabila lake, kwa sababu Mordekai alikuwa amemkataza.
Och Esther sade honom intet utaf sitt folk, eller sitt slägte; förty Mardechai hade budit henne, att hon skulle icke sägat.
11 Kila siku Mordekai alikuwa akitembeatembea karibu na ua wa nyumba ya wanawake kujua Esta alivyoendelea na kuona yaliyokuwa yakitendeka kwake.
Och Mardechai spatserade hvar dag i gårdenom åt fruhuset, att han måtte förnimma, om väl ginge med Esther, och hvad med henne ske kunde.
12 Kabla zamu ya msichana haijafika ya kwenda kwa Mfalme Ahasuero, ilimbidi atimize miezi kumi na miwili ya matunzo ya urembo kama ilivyokuwa imepangwa. Kwa miezi sita walikuwa wajipake mafuta ya manemane, na miezi sita kujipaka manukato na vipodozi.
Då nu hvarjo pigones bestämda tid kom, att hon skulle komma till Konungen Ahasveros, sedan hon hade varit i tolf månader i fruprydning; förty deras prydelse måste så mycken tid hafva, nämliga sex månader med balsam och myrrham, och sex månader med godt speceri, så voro då qvinnorna tillprydda;
13 Basi hivi ndivyo ambavyo msichana angeingia kwa mfalme: Kila kitu alichohitaji aliruhusiwa kuchukua kutoka nyumba ya wanawake na kwenda navyo katika jumba la mfalme.
Och så gick då en piga in till Konungen; och hvilka hon ville, måste man få henne, som med henne gå skulle ifrå fruhuset till Konungshuset.
14 Jioni angekwenda pale na asubuhi kurudi sehemu nyingine ya nyumba ya wanawake katika utunzaji wa Shaashgazi, towashi wa mfalme ambaye alikuwa mkuu wa masuria. Hangeweza kurudi kwa mfalme mpaka apendezwe naye na kuagiza aitwe kwa jina lake.
Och när en om aftonen inkom, gick hon om morgonen ifrå honom in uti det andra fruhuset, under Saasgas hand, Konungens kamererares, frillovaktarens; och hon måste icke komma igen till Konungen, utan Konungenom täcktes, och han lät kalla henne vid namn.
15 Zamu ya Esta ilipofika kwenda kwa mfalme (msichana ambaye Mordekai alikuwa amemlea, binti wa Abihaili mjomba wake), Esta hakutaka vitu zaidi ya vile ambavyo Hegai, towashi wa mfalme aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake alivyokuwa amemshauri. Naye Esta alipata kibali kwa kila mtu aliyemwona.
Då nu Esthers tid kom, Abihails dotters, Mardechai faderbroders, den henne för dotter tagit hade, att hon skulle komma till Konungen, begärade hon intet annat, än det Hegai, Konungens kamererare, qvinnovaktaren, sade henne före. Och Esther fann nåd för alla dem, som sågo uppå henne.
16 Esta alipelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika makao ya mfalme mwezi wa kumi, yaani mwezi wa Tebethi, katika mwaka wake wa saba wa kutawala.
Men Esther vardt tagen till Konungen Ahasveros, uti Konungshuset, i tionde månadenom, den Thebeth kallas; i sjunde årena hans rikes.
17 Basi ikawa mfalme alivutiwa na Esta kuliko wanawake wengine wote, naye akapata upendeleo na kibali kuliko mabikira wengine. Kisha akamvika taji la kifalme kichwani mwake na kumfanya malkia badala ya Vashti.
Och Konungen fick Esther kär öfver alla qvinnor, och hon fann nåd och barmhertighet för honom, för alla jungfrur; och han satte Drottningakrono uppå hennes hufvud, och gjorde henne till Drottning i Vasthis stad.
18 Mfalme akafanya karamu kubwa, karamu ya Esta, kwa wakuu wake wote na maafisa. Mfalme alitangaza mapumziko katika majimbo yake yote na kugawa zawadi kwa ukarimu wa kifalme.
Och Konungen gjorde ett stort gästabåd, till alla sina Förstar och tjenare; det gästabådet var för Esthers skull; och lät landen hafva rolighet, och gaf ut Konungsliga skänker.
19 Wakati mabikira walikusanyika mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme.
Och då man annan gång församlade jungfrur, satt Mardechai vid Konungens dörr.
20 Lakini Esta alikuwa ameficha siri ya kabila lake na uraia wake, kama Mordekai alivyokuwa amemwambia, kwa maana aliendelea kufuata maelekezo ya Mordekai kama alivyokuwa akifanya alipokuwa akimlea.
Och Esther hade ännu icke sagt sitt slägte, eller folk, såsom Mardechai henne budit hade; ty Esther gjorde efter Mardechai ord, lika som då han hennes förmyndare var.
21 Wakati Mordekai alikuwa ameketi kwenye lango la mfalme, Bigthana na Tereshi, maafisa wawili wa mfalme waliokuwa walinzi wa lango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero.
På samma tiden, då Mardechai vid Konungens dörr satt, vordo två Konungens kamererare vrede, Bigthan och Theres, som dörrena vaktade, och hade i sinnet, att de ville slå uppå Konungen Ahasveros.
22 Lakini Mordekai aligundua hila hii na kumwambia Malkia Esta, ambaye baadaye alimwarifu mfalme, huku akimsifu Mordekai.
Det förnam Mardechai, och lät Drottningena Esther få veta det; och Esther sade det för Konungenom, på Mardechai vägnar.
23 Taarifa hiyo ilipochunguzwa na kuonekana kuwa kweli, maafisa hao wawili waliangikwa juu ya miti ya kunyongea. Haya yote yaliandikwa katika kitabu cha kumbukumbu mbele ya mfalme.
Och då man ransakade derefter, vardt det så funnet; och de vordo både hängde i trän; och det vardt beskrifvet i Chrönicon för Konungenom.