< Esta 2 >
1 Baadaye, wakati hasira ya Mfalme Ahasuero ilikuwa imetulia, alimkumbuka Vashti na kile alichokuwa amekifanya na alilokuwa ameamuru juu yake.
Poslije toga, kad se utiša gnjev cara Asvira, on se opomenu Astine i što je uèinila i što je nareðeno za nju.
2 Kisha watumishi waliomhudumia mfalme walipendekeza, “Na ufanyike utafiti kwa ajili ya wanawali mabikira wazuri wa sura kwa ajili ya mfalme.
I rekoše momci carevi, sluge njegove: da potraže caru mladijeh djevojaka lijepijeh;
3 Mfalme na ateue maafisa katika kila jimbo la himaya yake kuwaleta hao wanawali wote wazuri wa sura katika nyumba ya wanawake katika ngome ya mji wa Shushani. Kisha wawekwe chini ya utunzaji wa Hegai, towashi wa mfalme, msimamizi wa wanawake; na wapewe matunzo yote ya urembo.
I neka odredi car pristave po svijem zemljama carstva svojega da skupe sve djevojke mlade i lijepe u Susan grad carski u ženski dvor pod ruku Igaja dvoranina careva, èuvara ženskoga, i neka im se daju potrebe za ljepotu.
4 Kisha yule ambaye atampendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti.” Shauri hili likampendeza mfalme, naye akalifuata.
Pa koja djevojka bude po volji caru, neka bude carica na Astinino mjesto. I to bi po volji caru, i uèini tako.
5 Basi katika mji wa ngome ya Shushani palikuwa na Myahudi wa kabila ya Benyamini, jina lake Mordekai mwana wa Yairi, mwana wa Shimei, mwana wa Kishi,
Bijaše u Susanu carskom gradu Judejac po imenu Mardohej, sin Jaira sina Simeja sina Kisova, od plemena Venijaminova,
6 ambao walichukuliwa uhamishoni kutoka Yerusalemu na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, wakiwa miongoni mwa waliochukuliwa mateka pamoja na Mfalme Yekonia wa Yuda.
Koji bi odveden u ropstvo iz Jerusalima s robljem koje bi odvedeno u ropstvo s Jehonijom carem Judinijem, kojega zarobi Navuhodonosor car Vavilonski.
7 Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.
On odgajaše Adasu, a to je Jestira, kæi strica njegova, jer ne imaše oca ni matere; a djevojka bijaše lijepa stasa i krasna lica, i po smrti oca joj i matere uze je Mardohej za kæer.
8 Wakati agizo na amri ya mfalme lilitangazwa, wanawali wengi waliletwa kwenye ngome ya mji wa Shushani na kuwekwa chini ya uangalizi wa Hegai. Pia Esta alipelekwa katika jumba la mfalme na akakabidhiwa Hegai, aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake.
I kad se razglasi rijeè careva i zapovijest, i mnogo se djevojaka skupi u Susan grad carski pod ruku Igajevu, bi i Jestira dovedena u dvor carev pod ruku Igaja èuvara ženskoga.
9 Msichana huyu alimpendeza na kupata kibali mbele zake. Mara moja akaanza kumpa matunzo ya uzuri na chakula maalum. Alimpa Esta vijakazi saba waliochaguliwa kutoka jumba la kifalme, na kumhamishia yeye pamoja na vijakazi wake katika sehemu bora zaidi katika nyumba ya wanawake.
I djevojka mu omilje i naðe milost u njega, te joj odmah dade potrebe za ljepotu i dio njezin, i sedam pristalijeh djevojaka iz carskoga doma, i namjesti je s njezinijem djevojkama na najljepše mjesto u ženskom domu.
10 Esta alikuwa hajadhihirisha uraia wala kabila lake, kwa sababu Mordekai alikuwa amemkataza.
Jestira ne kaza naroda svojega ni roda svojega, jer joj Mardohej bješe zabranio da ne kazuje.
11 Kila siku Mordekai alikuwa akitembeatembea karibu na ua wa nyumba ya wanawake kujua Esta alivyoendelea na kuona yaliyokuwa yakitendeka kwake.
A Mardohej hodaše svaki dan ispred trijema od ženskoga doma da bi doznao kako je Jestira i što æe biti od nje.
12 Kabla zamu ya msichana haijafika ya kwenda kwa Mfalme Ahasuero, ilimbidi atimize miezi kumi na miwili ya matunzo ya urembo kama ilivyokuwa imepangwa. Kwa miezi sita walikuwa wajipake mafuta ya manemane, na miezi sita kujipaka manukato na vipodozi.
A kad bi došao red na koju djevojku da uðe k caru Asviru, pošto bi joj se èinilo po ženskom zakonu dvanaest mjeseca jer toliko vremena trebaše da se uljepšavaju, šest mjeseca uljem od smirne a šest mjeseca mirisima i drugim stvarima za ljepotu žensku
13 Basi hivi ndivyo ambavyo msichana angeingia kwa mfalme: Kila kitu alichohitaji aliruhusiwa kuchukua kutoka nyumba ya wanawake na kwenda navyo katika jumba la mfalme.
Tada bi djevojka išla k caru, i što bi god rekla dalo bi joj se da s tijem ide iz ženske kuæe u dom carev.
14 Jioni angekwenda pale na asubuhi kurudi sehemu nyingine ya nyumba ya wanawake katika utunzaji wa Shaashgazi, towashi wa mfalme ambaye alikuwa mkuu wa masuria. Hangeweza kurudi kwa mfalme mpaka apendezwe naye na kuagiza aitwe kwa jina lake.
Uveèe bi ušla, a ujutru bi se vratila u drugu kuæu žensku pod ruku Sazgaza dvoranina careva, èuvara inoèkoga; više ne bi išla k caru, veæ ako bi je htio car, te bi bila pozvana po imenu.
15 Zamu ya Esta ilipofika kwenda kwa mfalme (msichana ambaye Mordekai alikuwa amemlea, binti wa Abihaili mjomba wake), Esta hakutaka vitu zaidi ya vile ambavyo Hegai, towashi wa mfalme aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake alivyokuwa amemshauri. Naye Esta alipata kibali kwa kila mtu aliyemwona.
I tako kad doðe red na Jestiru kæer Avihaila strica Mardohejeva, koju bješe uzeo za kæer, da uðe k caru, ona ne zaiska ništa nego što reèe Igaj dvoranin carev, èuvar ženski; i Jestira nalažaše milost u svakoga ko je viðaše.
16 Esta alipelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika makao ya mfalme mwezi wa kumi, yaani mwezi wa Tebethi, katika mwaka wake wa saba wa kutawala.
Tako bi Jestira odvedena k caru Asviru u carski dvor njegov desetoga mjeseca, koje je mjesec Tevet, sedme godine carovanja njegova.
17 Basi ikawa mfalme alivutiwa na Esta kuliko wanawake wengine wote, naye akapata upendeleo na kibali kuliko mabikira wengine. Kisha akamvika taji la kifalme kichwani mwake na kumfanya malkia badala ya Vashti.
I caru omilje Jestira mimo sve druge žene, i pridobi milost i ljubav njegovu mimo sve djevojke, te joj metnu carski vijenac na glavu i uèini je caricom na mjesto Astinino.
18 Mfalme akafanya karamu kubwa, karamu ya Esta, kwa wakuu wake wote na maafisa. Mfalme alitangaza mapumziko katika majimbo yake yote na kugawa zawadi kwa ukarimu wa kifalme.
I uèini car veliku gozbu svijem knezovima svojim i slugama svojim radi Jestire, i pokloni zemljama olakšice i razdade darove kako car može.
19 Wakati mabikira walikusanyika mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme.
A kad se drugom skupljahu djevojke, Mardohej sjeðaše na vratima carevijem.
20 Lakini Esta alikuwa ameficha siri ya kabila lake na uraia wake, kama Mordekai alivyokuwa amemwambia, kwa maana aliendelea kufuata maelekezo ya Mordekai kama alivyokuwa akifanya alipokuwa akimlea.
A Jestira ne kaza svojega roda ni naroda, kao što joj bješe zapovjedio Mardohej, i Jestira èinjaše što joj Mardohej govoraše, kao kad se odgajaše kod njega.
21 Wakati Mordekai alikuwa ameketi kwenye lango la mfalme, Bigthana na Tereshi, maafisa wawili wa mfalme waliokuwa walinzi wa lango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero.
U te dane, kad Mardohej sjeðaše na vratima carevijem, rasrdiše se Vihtan i Teres dva dvoranina careva izmeðu onijeh koji stražahu na pragu, i gledahu da dignu ruke na cara Asvira.
22 Lakini Mordekai aligundua hila hii na kumwambia Malkia Esta, ambaye baadaye alimwarifu mfalme, huku akimsifu Mordekai.
A to dozna Mardohej i javi carici Jestiri, a Jestira kaza caru u ime Mardohejevo.
23 Taarifa hiyo ilipochunguzwa na kuonekana kuwa kweli, maafisa hao wawili waliangikwa juu ya miti ya kunyongea. Haya yote yaliandikwa katika kitabu cha kumbukumbu mbele ya mfalme.
I kad se stvar izvidje i naðe, biše obješena ona obojica na drvo, i to se zapisa u knjigu dnevnika pred carem.