< Esta 1 >

1 Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
Ahaşveroş Hoddu'dan Kûş'a uzanan bölgedeki yüz yirmi yedi ilin kralıydı.
2 Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
O sırada ülkeyi Sus Kalesi'ndeki tahtından yönetiyordu.
3 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
Krallığının üçüncü yılında bütün önderlerinin ve görevlilerinin onuruna bir şölen verdi. Pers ve Med ordu komutanları, ileri gelenler ve il valileri de oradaydı.
4 Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
Ahaşveroş tam yüz seksen gün süren şenliklerle krallığının sonsuz zenginliğini, büyüklüğünün görkemini ve yüceliğini gösterdi.
5 Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
Bunun ardından, sarayının avlusunda küçük büyük ayırmadan, Sus Kalesi'nde bulunan bütün halka yedi gün süren bir şölen verdi.
6 Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
Mermer sütunlar üzerindeki gümüş çemberlere mor ve beyaz renkli iplikten yapılmış sicimlerle bağlanmış beyaz ve lacivert kumaşlar asılmıştı. Somaki, mermer, sedef ve pahalı taşlar döşenmiş avluya altın ve gümüş sedirler yerleştirilmişti.
7 Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
Sarayın en iyi şarabı kralın cömertliğine yaraşır biçimde bol bol ve her biri değişik altın kupalar içinde sunuluyordu.
8 Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
Kralın buyruğu uyarınca, konuklar içki içmeye zorlanmadı. Kral saray hizmetkârlarına konukların dileklerini yerine getirmeleri için buyruk vermişti.
9 Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
O sırada Kraliçe Vaşti de Kral Ahaşveroş'un sarayındaki kadınlara bir şölen veriyordu.
10 Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
Yedinci gün, şarabın etkisiyle keyiflenen Kral Ahaşveroş, hizmetindeki yedi haremağasına –Mehuman, Bizta, Harvona, Bigta, Avagta, Zetar ve Karkas'a– Kraliçe Vaşti'yi başında tacıyla huzuruna getirmelerini buyurdu. Kraliçe Vaşti güzeldi. Kral halka ve önderlere onun ne kadar güzel olduğunu göstermek istiyordu.
11 kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
Ama Kraliçe Vaşti haremağalarının kraldan getirdiği buyruğu reddedip gitmedi. Bunun üzerine kral çok kızdı, öfkesinden küplere bindi.
13 Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
Kral yasaları bilen bilge kişilerle görüştü. Çünkü kralın, yasaları ve adaleti bilen kişilere danışması gelenektendi.
14 nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
Kendisine en yakın olan Karşena, Şetar, Admata, Tarşiş, Meres, Marsena ve Memukan onunla yüzyüze görüşebiliyorlardı. Pers ve Med İmparatorluğu'nun bu yedi önderi krallığın en üst yöneticileriydi.
15 Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
Kral Ahaşveroş onlara, “Kralın haremağaları aracılığıyla gönderdiği buyruğa uymayan Kraliçe Vaşti'ye yasaya göre ne yapmalı?” diye sordu.
16 Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
Memukan, kralın ve önderlerin önünde şu yanıtı verdi: “Kraliçe Vaşti yalnız krala karşı değil, bütün önderlere ve kralın bütün illerindeki halklara karşı suç işledi.
17 Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
Bütün kadınlar, kraliçenin davranışıyla ilgili haberi duyunca, ‘Kral Ahaşveroş Kraliçe Vaşti'nin huzuruna getirilmesini buyurdu, ama kraliçe gitmedi’ diyerek kocalarını küçümsemeye başlayacaklar.
18 Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
Bugün kraliçenin davranışını öğrenen Pers ve Medli soylu kadınlar da kralın soylu adamlarına aynı biçimde davranacak. Bu da alabildiğine kadınların küçümsemesine, erkeklerin de öfkelenmesine yol açacak.
19 “Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
Kral uygun görüyorsa ferman çıkarsın; bu ferman Persler'le Medler'in değişmeyen yasalarına eklensin. Buna göre Vaşti bir daha Kral Ahaşveroş'un huzuruna çıkmasın ve kral ondan daha iyi birini kraliçeliğe seçsin.
20 Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
Kralın fermanı büyük krallığının dört bir yanına ulaşınca, ister soylu ister halktan olsun, bütün kadınlar kocalarına saygı gösterecektir.”
21 Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
Bu sözler kralın ve önderlerinin hoşuna gitti. Kral, Memukan'ın önerisine uyarak,
22 Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.
krallığın bütün illerine yazılı buyruklar gönderdi. Her ile kendi işaretleriyle ve her halka kendi diliyle yazıldı. Her erkeğin kendi evinin egemeni olduğu her dilde vurgulandı.

< Esta 1 >