< Esta 1 >

1 Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
India hoi Ethiopia totouh a ram 127 touh ka uk e Ahasuerus siangpahrang ni,
2 Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
Shushan khopui vah bawitungkhung dawk a tahungnae a kum thum nah,
3 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
Persia hoi Media ram e kâ ka tawn naw, ram ka ukkungnaw hoi kahrawikungnaw a kaw teh, a bawinaw hoi a sannaw hanlah pawi a to pouh.
4 Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
Hatnavah, a uknaeram tawntanae hoi a taluenae hah hnin 180 touh thung vah a pâtue.
5 Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
Hote ahnintha abaw toteh siangpahrang ni Shushan khopui dawk ka kamkhueng e tami kathoung kalen pueng hanlah siangpahrang takha um vah hnin sari touh thung pawi a to pouh.
6 Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
Ngunlaikawnaw bang e talung pangaw khomnaw dawkvah, lukkarei rui hoi, thung e, kapangaw, kahring, kaopaou, naw hoi thoseh, phai e lungphen ka paling, kaopaou, kapangaw, katamangnaw e van ta e sui ngun tahung tabennae naw hoi takha teh a pathoup.
7 Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
Siangpahrang a tawnta e patetlah misur teh suimanang dawk hoi a nei awh.
8 Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
Misur teh a nuencangcalah a nei awh teh apihai ngawt ka parui lah net awh hoeh. Tami pueng ni amamouh ngainae patetlah a sak nahanlah siangpahrang ni a im e kahrawikungnaw pueng koe a dei pouh.
9 Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
Hahoi, siangpahrangnu Vashti ni hai Ahasuerus siangpahrang im vah napuinaw hanlah pawi a to pouh van.
10 Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
A hnin sari hnin nah siangpahrang e a lungthin teh misur ni a nawm sak toteh, tuenla e sari touh, siangpahrang Ahasuerus hmalah thaw ouk ka tawk naw; Mehuman, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethar hoi Karkas tinaw hah,
11 kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
Siangpahrang ni Vashti teh a bawilukhung kâmuk hoi, tami puenghoi tami kalen naw koe a meihawinae patue hanlah siangpahrang hmalah thokhai hanelah kâ a poe.
12 Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
Hateiteh, siangpahrangnu Vashti teh tuenlanaw niyah tho hanlah siangpahrang ni kâpoe e lawk a dei pouh awh navah ngai hoeh. Hatdawkvah siangpahrang teh a lung puenghoi a khuek. A lungkhueknae hah hmaisaan patetlah a kaman.
13 Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
Hatdawkvah, siangpahrang ni hno kaawm e ka thai panuek e tami lungkaangnaw koe, bangkongtetpawiteh, kâlawk hoi lannae kong ka panuek e naw pueng hah siangpahrang ni pouknae ouk a pacei.
14 nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
A kut rahim thaw katawknaw teh; Karshena, Shethar, Admatha, Tarshish, Meres, Marsena, Memukan, Persia hoi Media ram tami kalen sari, siangpahrang pou kâhmo thainae kâ katawnnaw thungvah hmuenrasang poung koe ka tahung e bawinaw lah ao.
15 Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
Tuenlanaw ni patuen a thaisak awh ei, kai siangpahrang Ahasuerus e kâpoe e hah siangpahrangnu Vashti ni a ngâi hoeh dawkvah, aphung patetlah ahni hah bangtelamaw lawkceng han, telah a pacei navah,
16 Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
Memukan ni siangpahrang hoi tami kalen naw hmalah, Siangpahrangnu Vashti ni siangpahrang koe dueng yonnae sak hoeh, bawinaw hoi siangpahrang ni a uk e ramnaw pueng koehai a sak e lah ao.
17 Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
Bangkongtetpawiteh, siangpahrang Ahasuerus ni siangpahrangnu Vashti a kaw navah, tho pouh hoeh tie peng a kamthang dawkvah, siangpahrangnu e nuencang hah napuinaw pueng ni thai awh vaiteh a vanaw hah a hnephnap awh han.
18 Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
Siangpahrangnu ni a sak e Persia hoi Media bawinunaw ni a thai awh toteh, a kut rahim thaw ka tawk e bawinaw puenghai, hottelah bout dei awh vaiteh, minhmai khethoehnae hoi lungkhueknae hoeh a pung sak awh han.
19 “Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
Vashti hah siangpahrang Ahasuerus koevah bout kâen sak hoeh nahanlah ngainae awm pawiteh kâen hoeh nahanlah kâ pouh. Kâthung hoeh e kâpoenae ao thai nahanlah Persia hoi Midiannaw koe thun sak. Hahoi, Vashti hlak kahawi e napui hah siangpahrangnu lah lat telah atipouh awh.
20 Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
Hottelah, na sak pawiteh siangpahrang ni kâpoe e hah na uknaeram pueng dawk pathang torei teh, napuinaw pueng ni a vanaw hah a bari awh han, telah a ti.
21 Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
Hote lawk hah siangpahrang hoi a tami kalen naw ni a lung a kuep dawkvah siangpahrang ni Memukan ni a dei e patetlah a sak.
22 Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.
Siangpahrang uknae hoi ram tangkuem dawkvah a ma ca lahoi, miphun pueng a ma lawk lahoi, tongpa ni ma imthungkhu tangkuem dawk kâtawn hanlah ao tie lawk hah a pathang.

< Esta 1 >