< Waefeso 6 >
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema.
你們作子女的,要在主內聽從你們的父母,因為這是理所當然的。『
2 “Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi,
孝敬你的父親和母親──這是附有恩許的第一條誡命──
3 “upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
為使你得到幸福,並在地上延年益壽。』
4 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.
你們作父母的,不要惹你們的子女發怒;但要用主的規範和訓誡,教養他們。
5 Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo.
你們作奴僕的,要戰戰兢兢,以誠實的心,隨從你們肉身的主人,如同隨同基督一樣。
6 Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo.
不要只在人眼前服事,好像單討人的喜歡,而要像基督的僕人,從心裏遵行天主的旨意;
7 Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu.
甘心服事,好像服事主,而非服事人,
8 Mkijua kwamba Bwana atampa kila mtu thawabu kwa lolote jema alilotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.
因為你們知道:每一個人,或為奴的,或自主的,不論行了什麼善事,都要按他所行的領取主的賞報。
9 Nanyi mabwana, watendeeni watumwa wenu kwa jinsi iyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.
至於你們作主人的,要同樣對待奴僕,戒用恐嚇,因為你們知道,他們和你們在天上有同一個主,而且祂是不看情面的。
10 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
此外,你們務要在主內,藉祂的能力作堅強的人。
11 Vaeni silaha zote za Mungu ili kwamba mweze kuzipinga hila za ibilisi.
要穿上天主的全副武裝,為能抵抗魔鬼的陰謀,
12 Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. (aiōn )
因為我們戰鬥不是對抗血和肉,而是對抗率領者,對抗掌權者,對抗這黑暗世界的霸主,對抗天界裏邪惡的鬼神。 (aiōn )
13 Kwa hiyo vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja nanyi mkiisha kufanya yote, simameni imara.
為此,你們應拿起天主的全副武裝,為使你們在邪惡的日子能夠抵得住,並在獲得全勝之後,仍屹立不動。
14 Kwa hiyo simameni imara mkiwa mmejifunga kweli kiunoni na kuvaa dirii ya haki kifuani,
所以要站穩! 用真理作帶,束起你們的腰,穿上正義作甲,
15 nayo miguu yenu ifungiwe utayari tuupatao kwa Injili ya amani.
以和平的福音作準備走路的鞋,穿在腳上;
16 Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
上此外,還要拿起信德作盾牌,使你們能以此撲滅惡者的一切火箭;
17 Vaeni chapeo ya wokovu na mchukue upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu.
並戴上救恩當盔,拿著聖神作利劍,即天主的話,
18 Mkiomba kwa Roho siku zote katika sala zote na maombi, mkikesha kila wakati mkiwaombea watakatifu wote.
時時靠著聖神,以各種祈求和哀禱祈禱;且要醒寤不倦,為眾聖徒祈求,
19 Niombeeni na mimi pia, ili kila nifunguapo kinywa changu, nipewe maneno ya kusema, niweze kutangaza siri ya Injili kwa ujasiri,
也為我祈求,使我在開口的時候,賜我能說相稱的話,能放心大膽地傳揚福音的奧祕──
20 ambayo mimi ni balozi wake katika vifungo. Ombeni ili nipate kuhubiri kwa ujasiri kama inipasavyo.
為這福音我竟作了帶鎖鍊的使者──使我能放心大膽,我應該宣講的去宣講。
21 Tikiko, aliye ndugu mpendwa na mtumishi mwaminifu katika Bwana, atawaambia kila kitu, ili pia mpate kujua hali yangu na kile ninachofanya sasa.
今我有可愛的弟兄,且忠於主的服務者提希苛給你們報告一切,好使你們知道我的事和我現在做什麼。
22 Ninamtuma kwenu kwa ajili ya kusudi hili hasa, ili mpate kujua hali yetu, na awatie moyo.
我特意打發他到你們那裏去,為叫你們知道我們的情形,並叫他安慰你們的心。
23 Amani iwe kwa ndugu, na pendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo.
願平安、愛德和信德由天主父和主耶穌基督賜與眾弟兄!
24 Neema iwe na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo wa dhati. Amen.
恩寵與那些以永恆不變的愛愛我們的主耶穌基督的人同在!