< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
Sêde pois imitadores de Deus, como filhos amados;
2 mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
E andae em amor, como tambem Christo nos amou, e se entregou a si mesmo por nós, em offerta e sacrificio a Deus, em cheiro suave.
3 Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
Mas a fornicação, e toda a immundicia ou avareza, nem ainda se nomeie entre vós, como convém a sanctos;
4 Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
Nem torpezas, nem parvoices, nem chocarrices, que não conveem; mas antes acções de graças.
5 Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
Porque bem sabeis isto: que nenhum fornicario, ou immundo, ou avarento, que é idolatra, tem herança no reino de Christo e de Deus.
6 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
Ninguem vos engane com palavras vãs; porque por estas coisas vem a ira de Deus sobre os filhos da desobediencia.
7 Kwa hiyo, msishirikiane nao.
Portanto não sejaes seus companheiros.
8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
Porque d'antes ereis trevas, mas agora sois luz no Senhor: andae como filhos da luz
9 (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
(Porque o fructo do Espirito consiste em toda a bondade, e justiça e verdade);
10 nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
Approvando o que é agradavel ao Senhor.
11 Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
E não communiqueis com as obras infructuosas das trevas, mas antes condemnae-as.
12 Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
Porque o que elles fazem em occulto até dizel-o é coisa torpe.
13 Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
Mas todas estas coisas se manifestam sendo condemnadas pela luz, porque tudo o que se manifesta é luz.
14 kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
Pelo que diz: Desperta, tu que dormes, e levanta-te d'entre os mortos, e Christo te esclarecerá.
15 Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
Portanto, vêde como andaes prudentemente, não como nescios, mas como sabios,
16 mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
Remindo o tempo; porquanto os dias são maus.
17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
Pelo que não sejaes insensatos, mas entendei qual seja a vontade do Senhor.
18 Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
E não vos embriagueis com vinho, em que ha dissolução, mas enchei-vos do Espirito;
19 Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
Fallando entre vós em psalmos, e hymnos, e canticos espirituaes: cantando e psalmodiando ao Senhor no vosso coração:
20 siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Dando sempre graças por todas as coisas a nosso Deus e Pae, em nome de nosso Senhor Jesus Christo:
21 Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
Sujeitando-vos uns aos outros no temor de Deus.
22 Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
Vós, mulheres, sujeitae-vos a vossos proprios maridos, como ao Senhor;
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
Porque o marido é a cabeça da mulher, como tambem Christo a cabeça da egreja: e elle é o salvador do corpo.
24 Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
De sorte que, assim como a egreja está sujeita a Christo, assim tambem as mulheres estejam em tudo sujeitas a seus proprios maridos.
25 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
Vós, maridos, amae as vossas proprias mulheres, como tambem Christo amou a egreja, e a si mesmo se entregou por ella,
26 kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
Para a sanctificar, purificando-a com a lavagem da agua, pela palavra,
27 apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
Para a apresentar a si mesmo egreja gloriosa, que não tivesse macula, nem ruga, nem coisa similhante, mas que fosse sancta e irreprehensivel.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
Assim devem os maridos amar a suas proprias mulheres, como a seus proprios corpos. Quem ama a sua propria mulher, ama-se a si mesmo.
29 Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
Porque nunca ninguem aborreceu a sua propria carne; antes a alimenta e sustenta, como tambem o Senhor á egreja;
30 Sisi tu viungo vya mwili wake.
Porque somos membros do seu corpo, da sua carne, e dos seus ossos.
31 “Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
Por isso deixará o homem seu pae e sua mãe, e se ajuntará com sua mulher; e serão dois n'uma carne.
32 Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
Grande é este mysterio: digo, porém, isto de Christo e da egreja.
33 Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.
Assim tambem vós cada um em particular ame a sua propria mulher como a si mesmo, e a mulher reverenceie o marido.