< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
estote ergo imitatores Dei sicut filii carissimi
2 mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
et ambulate in dilectione sicut et Christus dilexit nos et tradidit se ipsum pro nobis oblationem et hostiam Deo in odorem suavitatis
3 Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
fornicatio autem et omnis inmunditia aut avaritia nec nominetur in vobis sicut decet sanctos
4 Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
aut turpitudo aut stultiloquium aut scurrilitas quae ad rem non pertinent sed magis gratiarum actio
5 Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
hoc enim scitote intellegentes quod omnis fornicator aut inmundus aut avarus quod est idolorum servitus non habet hereditatem in regno Christi et Dei
6 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
nemo vos seducat inanibus verbis propter haec enim venit ira Dei in filios diffidentiae
7 Kwa hiyo, msishirikiane nao.
nolite ergo effici participes eorum
8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
eratis enim aliquando tenebrae nunc autem lux in Domino ut filii lucis ambulate
9 (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
fructus enim lucis est in omni bonitate et iustitia et veritate
10 nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
probantes quid sit beneplacitum Deo
11 Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
et nolite communicare operibus infructuosis tenebrarum magis autem et redarguite
12 Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
quae enim in occulto fiunt ab ipsis turpe est et dicere
13 Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
omnia autem quae arguuntur a lumine manifestantur omne enim quod manifestatur lumen est
14 kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
propter quod dicit surge qui dormis et exsurge a mortuis et inluminabit tibi Christus
15 Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
videte itaque fratres quomodo caute ambuletis non quasi insipientes sed ut sapientes
16 mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
redimentes tempus quoniam dies mali sunt
17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
propterea nolite fieri inprudentes sed intellegentes quae sit voluntas Domini
18 Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
et nolite inebriari vino in quo est luxuria sed implemini Spiritu
19 Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
loquentes vobismet ipsis in psalmis et hymnis et canticis spiritalibus cantantes et psallentes in cordibus vestris Domino
20 siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
gratias agentes semper pro omnibus in nomine Domini nostri Iesu Christi Deo et Patri
21 Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
subiecti invicem in timore Christi
22 Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
mulieres viris suis subditae sint sicut Domino
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
quoniam vir caput est mulieris sicut Christus caput est ecclesiae ipse salvator corporis
24 Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
sed ut ecclesia subiecta est Christo ita et mulieres viris suis in omnibus
25 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
viri diligite uxores sicut et Christus dilexit ecclesiam et se ipsum tradidit pro ea
26 kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
ut illam sanctificaret mundans lavacro aquae in verbo
27 apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
ut exhiberet ipse sibi gloriosam ecclesiam non habentem maculam aut rugam aut aliquid eiusmodi sed ut sit sancta et inmaculata
28 Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
ita et viri debent diligere uxores suas ut corpora sua qui suam uxorem diligit se ipsum diligit
29 Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
nemo enim umquam carnem suam odio habuit sed nutrit et fovet eam sicut et Christus ecclesiam
30 Sisi tu viungo vya mwili wake.
quia membra sumus corporis eius de carne eius et de ossibus eius
31 “Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
propter hoc relinquet homo patrem et matrem suam et adherebit uxori suae et erunt duo in carne una
32 Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
sacramentum hoc magnum est ego autem dico in Christo et in ecclesia
33 Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.
verumtamen et vos singuli unusquisque suam uxorem sicut se ipsum diligat uxor autem ut timeat virum