< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
Be therefore imitators of God, as beloved children.
2 mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
Walk in love, even as Christ also loved us and gave himself up for us, an offering and a sacrifice to God for a sweet-smelling fragrance.
3 Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
But sexual immorality, and all uncleanness or covetousness, let it not even be mentioned among you, as becomes saints;
4 Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
nor filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not appropriate, but rather giving of thanks.
5 Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
Know this for sure, that no sexually immoral person, nor unclean person, nor covetous man (who is an idolater), has any inheritance in the Kingdom of Christ and God.
6 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
Let no one deceive you with empty words, for because of these things the wrath of God comes on the children of disobedience.
7 Kwa hiyo, msishirikiane nao.
Therefore do not be partakers with them.
8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
For you were once darkness, but are now light in the Lord. Walk as children of light,
9 (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
for the fruit of the Spirit is in all goodness and righteousness and truth,
10 nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
proving what is well pleasing to the Lord.
11 Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
Have no fellowship with the unfruitful deeds of darkness, but rather even reprove them.
12 Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
For it is a shame even to speak of the things which are done by them in secret.
13 Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
But all things, when they are reproved, are revealed by the light, for everything that reveals is light.
14 kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
Therefore he says, “Awake, you who sleep, and arise from the dead, and Christ will shine on you.”
15 Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
Therefore watch carefully how you walk, not as unwise, but as wise,
16 mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
redeeming the time, because the days are evil.
17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
Therefore, do not be foolish, but understand what the will of the Lord is.
18 Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
Do not be drunken with wine, in which is dissipation, but be filled with the Spirit,
19 Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
speaking to one another in psalms, hymns, and spiritual songs; singing and making melody in your heart to the Lord;
20 siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
giving thanks always concerning all things in the name of our Lord Jesus Christ to God, even the Father;
21 Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
subjecting yourselves to one another in the fear of Christ.
22 Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
Wives, be subject to your own husbands, as to the Lord.
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
For the husband is the head of the wife, as Christ also is the head of the assembly, being himself the savior of the body.
24 Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
But as the assembly is subject to Christ, so let the wives also be to their own husbands in everything.
25 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
Husbands, love your wives, even as Christ also loved the assembly and gave himself up for her,
26 kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
that he might sanctify her, having cleansed her by the washing of water with the word,
27 apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
that he might present the assembly to himself gloriously, not having spot or wrinkle or any such thing, but that she should be holy and without defect.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
Even so husbands also ought to love their own wives as their own bodies. He who loves his own wife loves himself.
29 Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
For no man ever hated his own flesh, but nourishes and cherishes it, even as the Lord also does the assembly,
30 Sisi tu viungo vya mwili wake.
because we are members of his body, of his flesh and bones.
31 “Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
“For this cause a man will leave his father and mother and will be joined to his wife. Then the two will become one flesh.”
32 Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
This mystery is great, but I speak concerning Christ and the assembly.
33 Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.
Nevertheless each of you must also love his own wife even as himself; and let the wife see that she respects her husband.