< Waefeso 4 >

1 Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
Obsecro itaque vos ego vinctus in Domino, ut digne ambuletis vocatione, qua vocati estis,
2 Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
cum omni humilitate, et mansuetudine, cum patientia, supportantes invicem in charitate,
3 Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
soliciti servare unitatem Spiritus in vinculo pacis.
4 Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
Unum corpus, et unus Spiritus, sicut vocati estis in una spe vocationis vestrae.
5 Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
Unus Dominus, una fides, unum baptisma.
6 Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
Unus Deus et Pater omnium, qui est super omnes, et per omnia, et in omnibus nobis.
7 Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo.
Unicuique autem nostrum data est gratia secundum mensuram donationis Christi.
8 Kwa hiyo husema: “Alipopaa juu zaidi, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa.”
Propter quod dicit: Ascendens in altum captivam duxit captivitatem: dedit dona hominibus.
9 (Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
Quod autem ascendit, quid est, nisi quia et descendit primum in inferiores partes terrae?
10 Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
Qui descendit, ipse est et qui ascendit super omnes caelos, ut impleret omnia.
11 Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu,
Et ipse dedit quosdam quidem Apostolos, quosdam autem Prophetas, alios vero Evangelistas, alios autem pastores, et doctores
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa
ad consummationem sanctorum in opus ministerii, in aedificationem corporis Christi:
13 mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.
donec occurramus omnes in unitatem fidei, et agnitionis filii Dei, in virum perfectum, in mensuram aetatis plenitudinis Christi:
14 Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.
ut iam non simus parvuli fluctuantes, et circumferamur omni vento doctrinae in nequitia hominum, in astutia ad circumventionem erroris.
15 Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo.
Veritatem autem facientes in charitate, crescamus in illo per omnia, qui est caput Christus:
16 Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.
ex quo totum corpus compactum, et connexum per omnem iuncturam subministrationis, secundum operationem in mensuram uniuscuiusque membri, augmentum corporis facit in aedificationem sui in charitate.
17 Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao.
Hoc igitur dico, et testificor in Domino, ut iam non ambuletis, sicut et Gentes ambulant in vanitate sensus sui,
18 Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
tenebris obscuratum habentes intellectum, alienati a vita Dei per ignorantiam, quae est in illis, propter caecitatem cordis ipsorum,
19 Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.
qui desperantes, semetipsos tradiderunt impudicitiae, in operationem immunditiae omnis in avaritiam.
20 Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo.
Vos autem non ita didicistis Christum,
21 Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu.
si tamen illum audistis, et in ipso edocti estis, sicut est veritas in Iesu.
22 Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu,
Deponite vos secundum pristinam conversationem veterem hominem, qui corrumpitur secundum desideria erroris.
23 ili mfanywe upya roho na nia zenu,
Renovamini autem spiritu mentis vestrae,
24 mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.
et induite novum hominem, qui secundum Deum creatus est in iustitia, et sanctitate veritatis.
25 Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja.
Propter quod deponentes mendacium, loquimini veritatem unusquisque cum proximo suo: quoniam sumus invicem membra.
26 Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,
Irascimini, et nolite peccare: sol non occidat super iracundiam vestram.
27 wala msimpe ibilisi nafasi.
Nolite locum dare diabolo:
28 Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.
qui furabatur, iam non furetur: magis autem laboret, operando manibus suis, quod bonum est, ut habeat unde tribuat necessitatem patienti.
29 Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.
Omnis sermo malus ex ore vestro non procedat: sed siquis bonus ad aedificationem fidei ut det gratiam audientibus.
30 Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
Et nolite contristare Spiritum sanctum Dei: in quo signati estis in die redemptionis.
31 Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu.
Omnis amaritudo, et ira, et indignatio, et clamor, et blasphemia tollatur a vobis cum omni malitia.
32 Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
Estote autem invicem benigni, misericordes, donantes invicem sicut et Deus in Christo donavit vobis.

< Waefeso 4 >