< Waefeso 4 >

1 Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
I therefore, a prisoner for the sake of the Lord, exhort you to walk worthy of the vocation wherewith ye are called, with all humility and meekness;
2 Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
and with long-suffering forbear one another in love,
3 Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
endeavouring to keep the unity of the Spirit in the bond of peace: for there is but one body and one Spirit,
4 Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
even as ye are called in one hope of your calling;
5 Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
one Lord, one faith, one baptism,
6 Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
one God and Father of all, who is above all, and through all, and in all.
7 Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo.
But grace is given to each of us, according to the measure of the gift of Christ.
8 Kwa hiyo husema: “Alipopaa juu zaidi, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa.”
Wherefore it is said, "When he ascended on high, He led captivity captive, and gave gifts to men."
9 (Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
Now this expression "He ascended" what does it mean, but that He descended first into the lower parts of the earth?
10 Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
He that descended is the same also that ascended far above all heavens, that he might fill all things.
11 Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu,
And therefore He gave some to be apostles, some prophets, some evangelists, and some pastors and teachers; to qualify holy men for the work of the ministry,
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa
to the edifying of the body of Christ:
13 mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.
till we all arrive in the unity of the faith, and of the knowledge of the Son of God, at perfect maturity, even to the measure of the stature of the fulness of Christ.
14 Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.
That we may be no longer children fluctuating and carried about with every wind of doctrine, by the artful insinuations of men, and their crafty methods of deceiving;
15 Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo.
but holding the truth in love, may grow up in all things into Him, who is the head, even Christ:
16 Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.
from whom the whole body being fitly joined together and compacted by the aid of every joint, according to the operation proportioned to every part, maketh an increase to the edification of itself in love.
17 Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao.
This I say therefore, and charge you in the name of the Lord, that ye no longer walk as the rest of the Gentiles walk,
18 Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
in the vanity of their mind, darkened in their understanding, and alienated from the life of God, through the ignorance that is in them, by reason of the hardness of their heart:
19 Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.
who, being past feeling, have given themselves up to lasciviousness, to commit all uncleanness with greediness.
20 Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo.
But ye have not so learned Christ;
21 Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu.
if ye have indeed hearkened to Him, and been instructed in Him, as the truth is in Jesus; to put off the old man,
22 Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu,
which according to your former conversation was corrupted with deceitful lusts,
23 ili mfanywe upya roho na nia zenu,
and be renewed in the spirit of your mind;
24 mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.
and to put on the new man, which according to the image of God is created in righteousness, and true holiness.
25 Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja.
Wherefore putting away lying, speak ye every one truth to his neighbor; for we are all members of one society.
26 Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,
Be angry, and sin not: let not the sun go down upon your wrath;
27 wala msimpe ibilisi nafasi.
and give not the devil room to ensnare you.
28 Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.
Let him that stole steal no more; but rather let him labour, doing some good with his hands, that he may have something to bestow on him that hath need of it.
29 Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.
Let no corrupt word come out of your mouth; but what is good to useful edification, that it may benefit the hearers.
30 Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
And grieve not the holy Spirit of God whereby ye are sealed to the day of redemption.
31 Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu.
Let all bitterness, and wrath, and fury, and clamor, and calumny, be put away from you, with all malice: and be kind one to another,
32 Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
tender-hearted, forgiving one another, even as God in Christ forgiveth you.

< Waefeso 4 >