< Waefeso 4 >

1 Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
I therefore, a prisoner in the Lord, urge you to lead a life worthy of the calling to which you have been called,
2 Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
with all humility and gentleness, with patience, bearing with one another in love;
3 Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
being eager to keep the unity of the Spirit in the bond of peace.
4 Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
There is one body, and one Spirit, even as you also were called in one hope of your calling;
5 Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
one Lord, one faith, one baptism,
6 Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
one God and Father of all, who is over all, and through all, and in all.
7 Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo.
But to each one of us was the grace given according to the measure of the gift of Christ.
8 Kwa hiyo husema: “Alipopaa juu zaidi, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa.”
Therefore he says, "When he ascended on high, he led captivity captive, and gave gifts to people."
9 (Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
Now this, "He ascended," what is it but that he also descended into the lower parts of the earth?
10 Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
He who descended is the one who also ascended far above all the heavens, that he might fill all things.
11 Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu,
He gave some to be apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, pastors and teachers;
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa
for the perfecting of the saints, to the work of serving, to the building up of the body of Christ;
13 mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.
until we all attain to the unity of the faith, and of the knowledge of the Son of God, to a mature person, to the measure of the stature of the fullness of Christ;
14 Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.
that we may no longer be children, tossed back and forth and carried about with every wind of doctrine, by the trickery of people, by cleverness in deceitful schemes;
15 Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo.
but speaking truth in love, we may grow up in all things into him, who is the head, Christ;
16 Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.
from whom all the body, being fitted and knit together through that which every joint supplies, according to the proper working of each individual part, makes the body increase to the building up of itself in love.
17 Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao.
This I say therefore, and testify in the Lord, that you no longer walk as the nations also walk, in the futility of their mind,
18 Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
being darkened in their understanding, alienated from the life of God, because of the ignorance that is in them, because of the hardening of their hearts;
19 Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.
who having become callous gave themselves up to lust, to work all uncleanness with greediness.
20 Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo.
But you did not learn Christ that way;
21 Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu.
if indeed you heard him, and were taught in him, even as truth is in Jesus:
22 Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu,
that you put away, as concerning your former way of life, the old self, that grows corrupt after the lusts of deceit;
23 ili mfanywe upya roho na nia zenu,
and that you be renewed in the spirit of your mind,
24 mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.
and put on the new self, who in the likeness of God has been created in righteousness and holiness of truth.
25 Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja.
Therefore, putting away falsehood, speak truth each one with his neighbor. For we are members of one another.
26 Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,
"Be angry, but do not sin." Do not let the sun go down on your anger,
27 wala msimpe ibilisi nafasi.
neither give place to the devil.
28 Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.
Let him who stole steal no more; but rather let him labor, working with his hands the thing that is good, that he may have something to give to him who has need.
29 Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.
Let no corrupt speech proceed out of your mouth, but such as is good for building up as the need may be, that it may give grace to those who hear.
30 Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
Do not grieve the Holy Spirit of God, in whom you were sealed for the day of redemption.
31 Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu.
Let all bitterness, wrath, anger, outcry, and slander, be put away from you, with all malice.
32 Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
And be kind to one another, tenderhearted, forgiving each other, just as God also in Christ forgave you.

< Waefeso 4 >