< Waefeso 3 >
1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
C'est dans ce but que je vous écris, moi Paul, le prisonnier de Jésus-Christ pour vous, Gentils;
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
si du moins vous avez entendu parler de la grâce, que, dans ses dispensations, Dieu m'a accordée en vue de vous.
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
C'est par une révélation que j'ai été initié au mystère dont j'ai dit quelques mots ci-dessus,
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
et vous pouvez apercevoir en les lisant, l'intelligence que j'en ai.
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
Il n'a pas été révélé en d'autres âges à l'humanité, comme il l'a été en ces derniers temps, par l'Esprit, aux saints apôtres de Christ et à ses prophètes,
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
à qui il a été dévoilé que les Gentils sont avec les Juifs membres du même corps, cohéritiers et coparticipants de la même promesse, en Jésus-Christ, par l'évangile.
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
J'ai été fait ministre de cet évangile par la faveur que la grâce de Dieu m'a accordée, et par l’efficacité de sa puissance.
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
C'est à moi, le moindre des saints, qu'a été faite cette faveur d'annoncer à tous les Gentils les richesses insondables de Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn )
et de les éclairer tous sur l'économie du mystère, qui avait été caché de tout temps en Dieu, le créateur de toutes choses, (aiōn )
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
afin qu'à la vue de l'Église, les principautés et les puissances dans les cieux connaissent aujourd'hui la sagesse infiniment variée de Dieu,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
selon le dessein éternel qu'il a réalisé en Jésus-Christ, notre Seigneur, (aiōn )
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
à qui nous devons la liberté de nous approcher de Dieu en toute assurance, par la foi que nous avons en lui.
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
C'est pourquoi je vous prie de ne pas vous laisser décourager par les afflictions que j'endure pour vous: elles sont votre gloire.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
C'est dans ce but que je fléchis les genoux devant le Père,
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
de qui vient à tout ce qui s'appelle «famille, » aux cieux et sur la terre, ce nom même de «famille.»
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
Qu'il veuille, selon les richesses de sa gloire, vous donner d'être puissamment fortifiés par son Esprit, pour le développement de l'homme intérieur,
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
en sorte que Christ habite en vos coeurs par la foi, afin qu'étant enracinés et fondés dans l'amour de Dieu,
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
vous soyez en état de comprendre avec tous les saints quelle en est la largeur et la longueur, la profondeur et la hauteur,
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
et de connaître l'amour de Christ, qui surpasse toute idée, afin que vous soyez parfaits en aspirant à toute la perfection de Dieu.
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
A Celui qui peut, par la puissance qui se déploie en nous, faire infiniment au delà de tout ce que nous demandons et pensons,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn )
à Lui soit la gloire dans l'Église et en Jésus-Christ, dans tous les âges, aux siècles des siècles! Amen! (aiōn )